Isaya 51
1 “Nisikilizeni, ninyi mnaofuatia haki na mnaomtafuta Mwenyezi Mungu: Tazameni mwamba ambako mlichongwa, na mahali pa kuvunjia mawe ambako mlichimbwa;
2 mwangalieni Ibrahimu, baba yenu, na Sara, ambaye aliwazaa. Wakati nilimwita alikuwa mmoja tu, nami nikambariki na kumfanya kuwa wengi.
3 Hakika Mwenyezi Mungu ataifariji Sayuni, naye atayaangalia kwa huruma magofu yake yote; atayafanya majangwa yake yawe kama Edeni, nazo sehemu zake zisizolimika ziwe kama bustani ya Mwenyezi Mungu. Shangwe na furaha zitakuwa ndani yake, shukrani na sauti za kuimba.
4 “Nisikilizeni, watu wangu; nisikieni, taifa langu: Torati itatoka kwangu; haki yangu itakuwa nuru kwa mataifa.
5 Haki yangu inakaribia mbio, wokovu wangu unakuja, nao mkono wangu utaleta hukumu kwa mataifa. Visiwa vitanitegemea na kungojea mkono wangu kwa matumaini.
6 Inueni macho yenu mbinguni, mkaitazame dunia chini; mbingu zitatoweka kama moshi, dunia itachakaa kama vazi, na wakazi wake kufa kama inzi. Bali wokovu wangu utadumu milele, haki yangu haitakoma kamwe.
7 “Nisikieni, ninyi mnaojua lililo sawa, ninyi watu ambao mna sheria yangu mioyoni mwenu: Msiogope mashutumu ya wanadamu wala msitiwe hofu na matukano yao.
8 Kwa maana nondo atawala kama vazi, nao funza atawatafuna kama sufu. Lakini haki yangu itadumu milele, wokovu wangu kwa vizazi vyote.”
9 Amka, Amka! Jivike nguvu, ewe mkono wa Mwenyezi Mungu, Amka, kama siku zilizopita, kama vile vizazi vya zamani. Si ni wewe uliyemkata Rahabu vipande vipande, uliyemchoma huyo mnyama mkubwa?
10 Si ni wewe uliyekausha bahari, maji ya kilindi kikuu, uliyefanya barabara katika vilindi vya bahari ili waliokombolewa wapate kuvuka?
11 Wale waliolipiwa fidia na Mwenyezi Mungu watarudi. Wataingia Sayuni wakiimba; furaha ya milele itakuwa taji juu ya vichwa vyao. Furaha na shangwe zitawapata, huzuni na kulia kwa uchungu kutatoweka.
12 “Mimi, naam mimi, ndimi niwafarijie ninyi. Ninyi ni nani hata kuwaogopa wanadamu wanaokufa, wanadamu ambao ni majani tu,
13 kwamba mnamsahau Mwenyezi Mungu Muumba wenu, aliyezitanda mbingu na kuiweka misingi ya dunia, kwamba mnaishi katika hofu siku zote kwa sababu ya ghadhabu ya mdhalimu, ambaye nia yake ni kuangamiza? Iko wapi basi ghadhabu ya mdhalimu?
14 Wafungwa waliojikunyata kwa hofu watawekwa huru karibuni; hawatafia kwenye gereza lao, wala hawatakosa chakula.
15 Kwa maana Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wako, ambaye huisukasuka bahari ili mawimbi yake yangurume: Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni ndilo jina lake.
16 Nimeweka maneno yangu kinywani mwako na kukufunika kwa uvuli wa mkono wangu: Mimi niliyeweka mbingu mahali pake, niliyeweka misingi ya dunia, niwaambiaye Sayuni, ‘Ninyi ni watu wangu.’ ”
17 Amka, amka! Simama, ee Yerusalemu, wewe uliyekunywa kutoka mkono wa Mwenyezi Mungu kikombe cha ghadhabu yake, wewe uliyekunywa hata machujo yake, kikombe kile cha kunywea kiwafanyacho watu kuyumbayumba.
18 Kati ya wana wote aliowazaa hapakuwa na hata mmoja wa kumwongoza; kati ya wana wote aliowalea hapakuwa hata mmoja wa kumshika mkono.
19 Majanga haya mawili yamekuja juu yako: ni nani awezaye kukufariji? Maangamizi, uharibifu, njaa na upanga: ni nani awezaye kukutuliza?
20 Wana wako wamezimia, wamelala kwenye mwanzo wa kila barabara, kama swala aliyenaswa kwenye wavu. Wamejazwa na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na makaripio ya Mungu wako.
21 Kwa hiyo sikiliza hili, wewe uliyeteswa, uliyelewa, lakini si kwa mvinyo.
22 Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi wako, Mungu wako, yeye ambaye huwatetea watu wake: “Tazama, nimeondoa mkononi mwako kikombe kilichokufanya uyumbayumbe; kutoka kikombe hicho, kikombe cha kunywa cha ghadhabu yangu, kamwe hutakunywa tena.
23 Nitakiweka mikononi mwa watesi wako, wale waliokuambia, ‘Anguka kifudifudi ili tuweze kutembea juu yako.’ Ukaufanya mgongo wako kama ardhi, kama njia yao ya kupita.”
Cross-references
178
- 1Isa 51:7, Psa 94:15, Psa 105:3–4, Heb 12:14, Rom 9:30–32, Rom 14:19, Isa 48:12, Eph 2:11–12
- 2Ezk 33:24, Rom 4:1–5, Gal 3:9–14, Heb 11:8–12, Isa 29:22, Gen 18:11–13, Gen 24:1, Gen 24:35
- 3Isa 49:13, Isa 52:9, Jol 2:3, Jer 31:25, Zep 3:14–20, Jer 33:11–13, Jer 31:12–14, Gen 13:10
- 41Pe 2:9, 1Co 9:21, Isa 2:3, Isa 42:6, Isa 49:6, Psa 78:1, Mic 4:2, Exo 33:13
- 5Rom 10:17–18, Isa 46:13, Isa 60:9, Rom 10:6–10, Isa 42:4, 2Co 5:10, Jol 3:12, Luk 24:47
- 6Mat 24:35, Psa 102:25–26, Heb 1:10–12, Isa 34:4, Rev 6:12–14, Jhn 3:15–16, 2Pe 3:10–12, Jhn 10:27–29
- 7Mat 5:11, Psa 37:31, Ezk 2:6, 1Pe 4:14, Act 5:41, Isa 51:1, Jer 1:17, Tit 2:11–12
- 8Isa 51:6, Isa 50:9, Isa 66:24, Job 4:19, Hos 5:12, Luk 1:50, Isa 46:13, Job 13:28
- 9Psa 74:13–14, Isa 52:1, Psa 89:10, Isa 27:1, Isa 30:7, Ezk 29:3, Psa 44:1, Job 26:12
- 10Isa 43:16, Isa 50:2, Isa 63:11–12, Exo 14:21–22, Exo 15:13, Isa 42:15, Psa 74:13
- 11Isa 25:8, Rev 21:4, Rev 7:17, Isa 35:10, 2Th 2:16, Isa 61:7, Jer 33:11, Isa 60:19–20
- 12Psa 118:6, 1Pe 1:24, Isa 2:22, Jhn 14:26–27, Jhn 14:18, 2Co 1:3–5, Jas 1:10–11, Isa 66:13
- 13Psa 104:2, Isa 45:12, Isa 40:22, Isa 17:10, 1Co 1:20, Isa 44:24, Isa 48:13, Job 9:8
- 14Isa 48:20, Zec 9:11, Isa 52:2, Act 12:7–8, Isa 49:10, Jer 38:6–13, Ezr 1:5, Lam 3:53–54
- 15Jer 31:35, Isa 54:5, Amo 9:5–6, Jer 10:16, Isa 47:4, Psa 114:3–5, Isa 51:10, Psa 74:13
- 16Isa 59:21, Isa 49:2, Jhn 17:8, Deu 18:18, Jer 31:33, Isa 66:22, Zec 13:9, Isa 50:4
- 17Isa 52:1, Rev 14:10, Isa 51:9, 1Co 15:34, Psa 60:3, Job 21:20, Eph 5:14, Psa 75:8
- 18Isa 49:21, Psa 88:18, Isa 45:1, Psa 142:4, Mrk 8:23, Mat 15:14, Mat 9:36, Isa 41:13
- 19Isa 47:9, Amo 7:2, Lam 1:12, Job 2:11, Ecc 4:1, Isa 61:2, Jer 9:17–21, Isa 14:30
- 20Rev 16:9–11, Lam 2:11–12, Isa 49:26, Ezk 12:13, Rev 14:10, Lam 1:15, Isa 51:21, Isa 29:9
- 21Isa 54:11, Isa 51:17, Isa 29:9
- 22Pro 22:23, Isa 51:17, Isa 62:8, Jer 50:34, Isa 49:25, Psa 35:1, 1Sa 25:39, Mic 7:9
- 23Jos 10:24, Zec 12:2, Psa 65:11–12, Rev 17:18, Rev 11:2, Pro 11:8, Pro 21:18, Rev 13:16–17
Topics in this chapter
42
Abraham, Afflictions and Adversities, Arm, Backsliders, Blessing, Bull, Call, Captive, Church, Cowardice, Cup, Death, Depravity of Man, Dragon, Drunkenness, Earth, Eden, Forgetting God, God, Gospel, Heaven, Holiness, Holy Spirit, Humility, Israel, Prophecies Concerning, Jesus, the Christ, Joy, Justification, Life, Moth, Net, Persecution, Praise, Rahab, Ransom, Righteous, Salvation, Seekers, War, Wicked (People), Word of God, Zion