Isaya 61
1 Roho wa Bwana Mungu Mwenyezi yu juu yangu, kwa sababu Mwenyezi Mungu amenipaka mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwafariji waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao;
2 kutangaza mwaka wa Mwenyezi Mungu uliokubaliwa, na siku ya kisasi ya Mungu wetu, kuwafariji wote wanaoomboleza,
3 na kuwapa mahitaji wale wanaohuzunika katika Sayuni, ili kuwapa taji za uzuri badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa. Nao wataitwa mialoni ya haki, pando la Mwenyezi Mungu, ili kuonesha utukufu wake.
4 Watajenga upya magofu ya zamani na kupatengeneza mahali palipoachwa ukiwa zamani; watafanya upya miji iliyoharibiwa, iliyoachwa ukiwa kwa vizazi vingi.
5 Wageni watayachunga makundi yenu, wageni watafanya kazi katika mashamba yenu, na kutunza mashamba yenu ya mizabibu.
6 Nanyi mtaitwa makuhani wa Mwenyezi Mungu, mtaitwa watumishi wa Mungu wetu. Mtakula utajiri wa mataifa, nanyi katika utajiri wao mtajisifu.
7 Badala ya aibu yao watu wangu watapokea sehemu maradufu, na badala ya fedheha watafurahia katika urithi wao; hivyo watarithi sehemu maradufu katika nchi yao, nayo furaha ya milele itakuwa yao.
8 “Kwa maana Mimi, Mwenyezi Mungu, napenda haki, na ninachukia unyang’anyi na uovu. Katika uaminifu wangu nitawapa malipo yao na kufanya agano la milele nao.
9 Wazao wao watajulikana miongoni mwa mataifa, na uzao wao miongoni mwa makabila ya watu. Wale wote watakaowaona watatambua kuwa ni taifa ambalo Mwenyezi Mungu amelibariki.”
10 Ninafurahia sana katika Mwenyezi Mungu, nafsi yangu inashangilia katika Mungu wangu. Kwa maana amenivika mavazi ya wokovu, na kunipamba kwa joho la haki, kama vile bwana arusi apambavyo kichwa chake kama kuhani, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vito vyake vya thamani.
11 Kwa maana kama vile ardhi ifanyavyo chipukizi kuota, na bustani isababishavyo mbegu kuota, ndivyo Bwana Mungu Mwenyezi atafanya haki na sifa zichipuke mbele ya mataifa yote.
Cross-references
79
- 1Luk 4:18–19, Luk 7:22, Isa 42:7, Mat 11:5, Psa 147:3, Isa 42:1, Zec 9:11–12, Act 10:38
- 2Mat 5:4, Isa 34:8, Isa 57:18, Luk 4:19, 2Th 2:16–17, Jhn 16:20–22, 1Th 2:16, Jer 31:13
- 3Psa 30:11, Jer 17:7–8, Jhn 16:20, Isa 61:10, Psa 45:7, Ecc 9:8, 1Pe 2:9, Psa 23:5
- 4Isa 58:12, Amo 9:14–15, Ezk 36:33–36, Ezk 36:23–26, Isa 49:6–8
- 5Isa 60:10–14, Isa 14:1–2, Eph 2:12–20
- 6Exo 19:6, 1Pe 2:9, 1Pe 2:5, Isa 60:5–7, Isa 66:21, Rev 5:10, 2Co 11:23, Rev 20:6
- 7Job 42:10, Zec 9:12, Isa 40:2, Isa 60:19–20, Psa 16:11, 2Ki 2:9, Isa 51:11, 2Co 4:17
- 8Psa 11:7, Jer 9:24, Zec 8:16–17, Jer 32:40, Gen 17:7, Isa 55:3, Psa 37:28, Psa 25:8–12
- 9Isa 44:3, Psa 115:14, Gen 22:18, Act 3:26, Isa 65:23, Rom 9:3–4, Zec 8:13
- 10Rev 19:7–8, Psa 132:9, Php 3:9, Psa 132:16, Rev 21:2, Rom 5:11, Isa 49:18, Rom 14:17
- 111Pe 2:9, Mrk 4:26–32, Isa 58:11, Isa 55:10–11, Isa 62:7, Isa 45:8, Isa 62:1, Psa 85:11
Topics in this chapter
34
Afflictions and Adversities, Anointing, Bride, Bridegroom, Captivity, Church, Covenant, Garment, Glorifying God, God, Gospel, Holiness, Holy Spirit, Hypocrisy, Israel, Prophecies Concerning, Jesus, the Christ, Joy, Jubilee, Justification, Liberty, Marriage, Minister, Christian, Praise, Priest, Prisoners, Quotations and Allusions, Repentance, Robbery, Robe, Salvation, Seekers, Symbols and Similitudes, Theft and Thieves, Trinity