Isaya 62
1 Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hadi haki yake itakapoangaza kama mapambazuko, wokovu wake kama mwanga wa moto.
2 Mataifa wataona haki yako, nao wafalme wote wataona utukufu wako; wewe utaitwa kwa jina jipya lile ambalo kinywa cha Mwenyezi Mungu kitatamka.
3 Utakuwa taji la fahari mkononi mwa Mwenyezi Mungu, taji la kifalme mkononi mwa Mungu wako.
4 Hawatakuita tena Aliyeachwa, wala nchi yako kuiita Ukiwa. Bali utaitwa Hefsiba, nayo nchi yako itaitwa Beula, kwa maana Mwenyezi Mungu atakufurahia, nayo nchi yako itaolewa.
5 Kama vile kijana aoavyo mwanamwali, ndivyo Mwashi wako atakavyokuoa; kama bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi wake, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.
6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, ee Yerusalemu, hawatanyamaza mchana wala usiku. Ninyi wenye kumwita Mwenyezi Mungu, msitulie,
7 msimwache apumzike hadi atakapoufanya imara Yerusalemu na kuufanya uwe sifa ya dunia.
8 Mwenyezi Mungu ameapa kwa mkono wake wa kuume na kwa mkono wake wenye nguvu: “Kamwe sitawapa tena adui zenu nafaka zenu kama chakula chao; kamwe wageni hawatakunywa tena divai mpya ambayo mmeitaabikia,
9 lakini wale waivunao nafaka wataila na kumsifu Mwenyezi Mungu, nao wale wakusanyao zabibu watainywa divai yake katika nyua za patakatifu pangu.”
10 Piteni, piteni katika malango! Tengenezeni njia kwa ajili ya watu. Jengeni, jengeni njia kuu! Ondoeni mawe. Inueni bendera kwa ajili ya mataifa.
11 Mwenyezi Mungu ametoa tangazo hadi miisho ya dunia: “Mwambie Binti Sayuni, ‘Tazama, mwokozi wako anakuja! Tazama ujira wake uko pamoja naye, na malipo yake yanafuatana naye!’ ”
12 Wataitwa Watu Watakatifu, Waliokombolewa na Mwenyezi Mungu; nawe utaitwa Aliyetafutwa, Mji Usioachwa Tena.
Cross-references
88
- 1Isa 62:6–7, Pro 4:18, Psa 102:13–16, Isa 32:15–17, Luk 2:30–32, 1Pe 2:9, Heb 7:25, Php 2:15–16
- 2Isa 62:12, Gen 17:5, Isa 65:15, Rev 2:17, Isa 66:12, Isa 60:1–3, Isa 49:23, Gen 17:15
- 3Isa 28:5, Zec 9:16, 1Th 2:19, Luk 2:14
- 4Zep 3:17, Hos 2:19–20, Isa 62:12, Isa 54:5–7, Jer 32:41, 1Pe 2:10, Isa 61:10, Psa 149:4
- 5Isa 62:4, Isa 65:19, Heb 12:2, Isa 49:18–22, Psa 45:11–16, Jer 32:41, Sng 3:11
- 6Isa 52:8, Ezk 3:17–21, Psa 134:1–2, 1Th 5:17, Jer 6:17, Luk 11:5–13, Heb 13:17, Isa 56:10
- 7Jer 33:9, Zep 3:19–20, Isa 60:18, Luk 18:1–8, Mat 6:9–10, Isa 61:11–62:3, Rev 11:15, Mat 6:13
- 8Isa 65:21–23, Jdg 6:3–6, Deu 28:33, Deu 28:31, Ezk 20:5, Lev 26:16, Jer 5:17, Isa 1:7
- 9Deu 16:11, Deu 12:12, Deu 12:7, Deu 16:14, Deu 14:23–29
- 10Isa 57:14, Isa 40:3, Heb 12:13, Isa 49:22, Isa 11:10, Mat 22:9, Isa 11:12, Exo 17:15
- 11Zec 9:9, Mat 21:5, Jhn 12:15, Rev 22:12, Isa 40:9–10, Rom 10:11–18, Psa 98:1–3, Isa 49:4
- 121Pe 2:9, Deu 26:19, Isa 62:4, Deu 28:9, Isa 35:9, Deu 7:6, Psa 107:2, Isa 42:16
Topics in this chapter
28
Anthropomorphisms, Arm, Beulah, Canaan, Church, Crown, God, Hand, Hephzi-Bah, House of God, Intercession, Israel, Prophecies Concerning, Jerusalem, Jesus, the Christ, Lamp, Marriage, Minister, Christian, Name, Patriotism, Prayer, Righteous, Righteousness, Salvation, Standard, Virgin, Watchman, Zeal, Religious, Zion