Waebrania 11
1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, na udhahiri wa mambo yasiyoonekana.
2 Maana baba zetu wa kale walipongezwa kwa haya.
3 Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vyote vinavyoonekana havikuumbwa kutoka kwa vitu vinavyoonekana.
4 Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu bora kuliko Kaini. Kwa imani alishuhudiwa kuwa mwenye haki, Mungu mwenyewe akazishuhudia sadaka zake. Kwa imani bado ananena ingawa amekufa.
5 Kwa imani Idrisi alitwaliwa kutoka maisha haya, kiasi kwamba hakuonja mauti. Hakuonekana, “kwa sababu Mungu alimchukua”. Kwa kuwa kabla hajatwaliwa alikuwa ameshuhudiwa kuwa ni mtu aliyempendeza Mungu.
6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana yeyote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wanaomtafuta kwa bidii.
7 Kwa imani, Nuhu alipoonywa na Mungu kuhusu mambo ambayo hayajaonekana bado, kwa kumcha Mungu alitengeneza safina ili kuokoa jamaa yake. Kwa imani yake aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.
8 Kwa imani Ibrahimu, alipoitwa aende mahali Mungu angempa baadaye kuwa urithi, alitii na akaenda, ingawa hakujua anakoenda.
9 Kwa imani alifanya maskani yake katika nchi ya ahadi kama mgeni katika nchi ya kigeni; aliishi katika mahema, kama Isaka na Yakobo walivyofanya, waliokuwa pia warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
10 Kwa maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi ya kudumu, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.
11 Kwa imani Ibrahimu, ingawa alikuwa mzee wa umri, naye Sara mwenyewe aliyekuwa tasa, alipokea uwezo wa kuwa baba kwa sababu alimhesabu Mungu aliyemwahidi kuwa mwaminifu na kwamba angetimiza ahadi yake.
12 Hivyo kutokana na huyu mtu aliyekuwa sawa na mfu, wakazaliwa wazao wengi kama nyota za mbinguni na kama mchanga wa pwani usiohesabika.
13 Watu hawa wote wakafa katika imani bila kuzipokea zile ahadi, lakini waliziona kwa mbali na kuzishangilia. Nao walikubali kwamba walikuwa wageni na wasiokuwa na maskani hapa duniani.
14 Watu wasemao mambo kama haya, wanaonesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
15 Kwa kweli kama wangekuwa wanafikiri kuhusu nchi waliyoiacha, wangepata nafasi ya kurudi huko.
16 Lakini badala yake walitamani nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa amekwisha kuandaa mji kwa ajili yao.
17 Kwa imani Ibrahimu, alipojaribiwa na Mungu, alimtoa Isaka kuwa dhabihu. Yeye aliyekuwa amezipokea ahadi za Mungu alikuwa tayari kumtoa mwanawe, aliyekuwa mwanawe pekee awe dhabihu,
18 hata ingawa Mungu alikuwa amemwambia Ibrahimu, “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwa Isaka.”
19 Ibrahimu alihesabu kuwa Mungu angeweza kumfufua Isaka kutoka kwa wafu. Na kusema kwa mfano, alimpata tena Isaka kutoka kwa wafu.
20 Kwa imani Isaka aliwabariki Yakobo na Esau kuhusu maisha yao ya baadaye.
21 Kwa imani Yakobo alipokuwa anakufa, alimbariki kila mmoja wa mtoto wa Yusufu, akamwabudu Mungu akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.
22 Kwa imani, Yusufu alipokaribia mwisho wa maisha yake, alinena habari za kutoka kwa Waisraeli huko Misri na akatoa maagizo kuhusu mifupa yake.
23 Kwa imani, wazazi wa Musa walimficha kwa miezi mitatu baada ya kuzaliwa, kwa sababu waliona kuwa si mtoto wa kawaida, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24 Kwa imani, Musa alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25 Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu, kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa muda mfupi.
26 Aliona kushutumiwa kwa ajili ya Al-Masihi ni utajiri mkubwa kuliko hazina za Misri, maana alikuwa anatazamia kupata thawabu baadaye.
27 Kwa imani Musa aliondoka Misri bila kuogopa ghadhabu ya mfalme. Alivumilia kwa sababu alimwona yeye asiyeonekana kwa macho.
28 Kwa imani akaadhimisha Pasaka na kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wazaliwa wa Israeli.
29 Kwa imani, watu walivuka Bahari ya Shamu kama vile juu ya nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo, walitoswa ndani ya maji.
30 Kwa imani kuta za Yeriko zilianguka, baada ya watu kuzizunguka kwa siku saba.
31 Kwa imani, Rahabu, yule kahaba, hakuangamizwa pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi.
32 Basi niseme nini zaidi? Sina wakati wa kusema habari za Gideoni, Baraka, Samsoni, Yefta, Daudi, Samweli na manabii,
33 ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitekeleza haki, na wakapokea ahadi za Mungu; walifunga vinywa vya simba,
34 wakazima makali ya miali ya moto, na wakaepuka kuuawa kwa upanga; udhaifu wao uligeuka kuwa nguvu; pia walikuwa hodari vitani na kuyafukuza majeshi ya wageni.
35 Wanawake walipokea watu wao waliokuwa wamekufa, wakafufuliwa. Lakini wengine waliteswa, nao wakakataa kufunguliwa, ili wapate ufufuo ulio bora zaidi.
36 Wengine walidhihakiwa na kupigwa, hata walifungwa minyororo na kutiwa gerezani.
37 Walipigwa kwa mawe; walipasuliwa vipande viwili kwa msumeno; waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na mbuzi, wakiwa maskini, wakiteswa na kutendwa mabaya,
38 watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao. Walizunguka majangwani na milimani, katika mapango na katika mahandaki ardhini.
39 Hawa wote walishuhudiwa vyema kwa sababu ya imani yao, lakini hakuna hata mmoja wao aliyepokea yale yaliyoahidiwa.
40 Kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea kitu kilicho bora zaidi ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.
Cross-references
264
- 12Co 5:7, 2Co 4:18, Rom 8:24–25, Heb 11:7, Heb 10:22, 1Pe 1:7–8, Psa 27:13, Heb 11:27
- 2Heb 11:39, Heb 11:4
- 3Psa 33:6, Jhn 1:3, 2Pe 3:5, Rom 4:17, Act 17:24, Rev 4:11, Heb 1:2, Rom 1:19–21
- 4Gen 4:3–5, 1Jn 3:11–12, Heb 12:24, Gen 4:10, Pro 15:8, Mat 23:35, Jud 1:11, Heb 9:22
- 5Gen 5:21–24, Jud 1:14, 2Ki 2:11, Heb 11:6, Rev 11:9–12, Psa 89:48, 1Th 2:4, 2Ki 2:16–17
- 6Pro 8:17, Jer 29:13–14, Mat 6:33, Psa 105:3–4, 1Ch 28:9, Luk 12:31, Psa 119:10, Heb 7:25
- 7Gen 6:13–7:1, 1Pe 3:20, Ezk 14:14, Rom 4:13, Luk 17:26, Rom 3:22, Gal 5:5, Php 3:9
- 8Act 7:2–4, Gen 12:1–4, Gen 15:7–8, Mat 7:24–25, Gen 22:18, Gen 12:7, Jas 2:14–16, Isa 41:2
- 9Gen 12:8, Gen 13:18, Gen 13:3, Act 7:5–6, Heb 6:17, Gen 26:3–4, Gen 18:9, Gen 35:27
- 10Heb 13:14, Php 3:20, 2Co 5:1, Heb 12:22, Jhn 14:2, Heb 3:4, Rev 21:2, Rev 21:10–27
- 11Rom 4:20–21, Heb 10:23, Gen 18:11–14, Gen 21:1–2, Luk 1:36, 1Pe 3:5–6, Gen 17:17–19
- 12Gen 22:17, Gen 32:12, Gen 15:5, Hos 1:10, Jer 33:22, Gen 26:4, Rev 20:8, Isa 10:22
- 13Gen 23:4, Psa 39:12, Heb 11:27, Jhn 8:56, Rom 8:24, 1Ch 29:14–15, 1Pe 2:11, Heb 11:39
- 142Co 4:18–5:7, Heb 11:16, Rom 8:23–25, Heb 13:14, Php 1:23
- 15Gen 24:6–8, Gen 12:10
- 16Heb 13:14, Php 3:20, Heb 11:10, Jhn 14:2, Mat 25:34, Heb 2:11, Heb 12:22, 2Ti 4:18
- 17Gen 22:16, Jas 2:21–24, Gen 22:1–12, 1Pe 1:6–7, Jas 5:11, Rev 3:10, Pro 17:3, 1Pe 4:12
- 18Gen 21:12, Rom 9:7, Gen 17:19
- 19Mat 9:28, Rom 4:17–21, Gen 22:13, Eph 3:20, Gen 22:4–5, Heb 11:11–12, Heb 9:24, Rom 5:14
- 20Gen 27:27–40, Gen 28:2–3
- 21Gen 47:31–48:1, Gen 48:5–22
- 22Exo 13:19, Gen 50:24–25, Jos 24:32, Act 7:16
- 23Exo 1:22, Exo 1:16, Exo 2:2–10, Heb 13:6, Mat 10:28, Isa 8:12–13, Isa 41:14, Psa 118:6
- 24Exo 2:10–11, Act 7:21–24
- 25Psa 84:10, 2Ti 2:3–10, Job 36:21, 1Pe 4:12–16, 2Co 5:17, Job 20:5, 1Pe 1:6–7, 1Pe 2:10
- 26Heb 10:35, Heb 11:6, Mat 5:12, 1Pe 4:14, Psa 89:50–51, Heb 2:2, Rev 3:18, 2Co 6:10
- 272Co 4:18, Heb 11:13, Exo 2:14–15, Heb 11:1, Exo 14:10–13, Jas 5:11, Exo 4:19, Exo 10:28–29
- 28Exo 12:21–30, Heb 9:19, Heb 12:24, 1Pe 1:2, Exo 12:3–14
- 29Psa 78:13, Exo 14:13–15:21, Psa 106:9–11, Isa 63:11–16, Hab 3:8–10, Isa 51:9–10, Jos 2:10, Psa 66:6
- 30Jos 6:3–20, 2Co 10:4–5
- 31Jas 2:25, Jos 6:22–25, Mat 1:5, Jos 2:1–24, Mat 1:1, Jos 1:1, 1Pe 3:20, 1Pe 2:8
- 321Sa 1:20, 1Sa 16:1, 1Sa 16:13, Jdg 13:1–16, Jdg 11:1–12, Jhn 21:25, Rom 4:1, Act 13:20
- 33Psa 144:1–2, Heb 6:12–15, Heb 10:36, 2Ti 4:17, Heb 11:4–8, Psa 144:10, Jdg 14:5–6, 1Pe 5:8
- 341Sa 17:51–52, 2Ki 6:16–18, Psa 144:10, Jdg 15:8, 2Co 12:9–10, 2Ch 32:20–22, 2Sa 10:15–19, 2Ki 6:32
- 351Ki 17:22–24, 2Ki 4:27–37, Php 3:11, Act 9:41, Act 24:15, 1Co 15:54, Act 23:6, Jhn 11:40–45
- 36Jer 20:2, Gen 39:20, Jer 37:15–21, 2Ch 30:10, Mat 23:34, Heb 10:34, 2Ch 16:10, Jer 20:7
- 372Ch 24:21, Jer 26:23, 1Ki 19:10, 1Ki 21:13–15, 2Ki 1:8, Act 7:52, 1Ki 21:10, Lam 4:13–14
- 381Ki 18:4, 1Sa 22:1, 1Ki 19:9, Isa 57:1, 1Sa 24:1–3, 1Ki 17:3, Psa 142:1–7, 1Sa 26:1
- 39Luk 10:23–24, Heb 11:13, Heb 11:2, 1Pe 1:12
- 40Rev 6:11, Heb 10:11–14, Heb 8:6, Heb 7:19, Heb 5:9, Heb 9:8–15, Heb 9:23, Rom 3:25–26
Topics in this chapter
82
Abed-Nego, Abel, Abraham, Adoption, Amusements and Worldly Pleasures, Antediluvians, Ark, Atonement, Backsliders, Barak, Beauty, Blood, Builder, Cain, Call, Canaan, Cave, Cities, Dead (People), Death, Decision, Dens, Desire, Diligence, Egyptians, Elder, Enoch, Esau, Faith, Fear, Fight of Faith, Flood, Gideon, God, Harlot (Prostitute), Heart, Heaven, Hope, Immortality, Influence, Isaac, Jacob, Jephthah, Jericho, Jesus, the Christ, Joseph, Justification, Law, Lion, Martyrdom, Moses, Noah, Obedience, Offerings, Patriotism, Persecution, Pleasure, Prayer, Prophets, Quotations and Allusions, Rahab, Red Sea, Religion, Resurrection, Reward, Righteous, Samson, Samuel, Sarah, Saw, Seekers, Self-Denial, Sprinkling, Stoning, Temptation, Translation, Unbelief, War, Word of God, Worldliness, Young Men, Zeal, Religious