Hosea 5
1 “Sikieni hili, enyi makuhani! Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli! Sikieni, ee nyumba ya mfalme! Hukumu hii ni dhidi yenu: Mmekuwa mtego huko Mispa, wavu uliotandwa juu ya Tabori.
2 Waasi wamezidisha sana mauaji. Mimi nitawatiisha wote.
3 Ninajua yote kuhusu Efraimu, Israeli hukufichika kwangu. Efraimu, sasa umegeukia ukahaba, Israeli amenajisika.
4 “Matendo yao hayawaachii kurudi kwa Mungu wao. Roho ya ukahaba iko ndani ya mioyo yao, hawamkubali Mwenyezi Mungu.
5 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao; Waisraeli, hata Efraimu, wanajikwaa katika dhambi zao; pia Yuda atajikwaa pamoja nao.
6 Wanapoenda na makundi yao ya kondoo na ng’ombe kumtafuta Mwenyezi Mungu, hawatampata; yeye amejiondoa kutoka kwao.
7 Wao si waaminifu kwa Mwenyezi Mungu; wamezaa watoto haramu. Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi zitawaangamiza wao pamoja na mashamba yao.
8 “Pigeni tarumbeta huko Gibea, na baragumu huko Rama. Pazeni kelele za vita huko Beth-Aveni; ongoza, ee Benyamini.
9 Efraimu ataachwa ukiwa katika siku ya kuadhibiwa. Miongoni mwa makabila ya Israeli ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaosogeza mawe ya mpaka. Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama mafuriko ya maji.
11 Efraimu amedhulumiwa, amekanyagwa katika hukumu kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.
12 Mimi ni kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa watu wa Yuda.
13 “Efraimu alipoona ugonjwa wake, naye Yuda vidonda vyake, ndipo Efraimu aligeukia Ashuru, na kuomba msaada kwa mfalme mkuu. Lakini hawezi kukuponya, hawezi kukuponya vidonda vyako.
14 Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu, kama simba mkubwa kwa Yuda. Nitawararua vipande vipande na kuondoka; nitawachukua mbali, na hakuna wa kuwaokoa.
15 Kisha nitarudi mahali pangu hadi watakapokubali kosa lao. Nao watautafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”
Cross-references
116
- 1Hos 9:8, Hos 6:9, Hab 1:15–17, Mic 7:2, Mic 3:9, Hos 4:1, Mal 2:1, Hos 10:15
- 2Hos 9:15, Isa 29:15, Hos 6:9, Rev 3:19, Jer 25:3–7, Jer 6:28, Jer 18:18, Luk 22:2–5
- 3Amo 3:2, Heb 4:13, Isa 7:17, Gen 48:19–20, Hos 5:9, 1Ki 14:14–16, Hos 4:17–18, Deu 33:17
- 4Hos 4:12, 1Jn 2:3–4, Jer 9:24, Hos 4:6, Jhn 8:55, Jhn 16:3, Hos 4:1, 2Th 2:11–12
- 5Hos 7:10, Amo 5:2, Luk 19:22, Ezk 23:31–35, Pro 24:16, Isa 28:1–3, Hos 14:1, Pro 11:21
- 6Pro 1:28, Jhn 7:34, Mic 6:6–7, Lam 3:44, Ezk 8:6, Pro 15:8, Isa 1:11–15, Jer 7:4
- 7Hos 6:7, Psa 144:11, Hos 2:4, Jer 3:20, Ezk 12:28, Psa 144:7, Isa 48:8, Zec 11:8
- 8Jol 2:1, Hos 9:9, Hos 4:15, 1Sa 15:34, Jer 4:5, Jdg 5:14, Hos 8:1, Isa 10:29
- 9Isa 46:10, Zec 1:6, Hos 9:11–17, Isa 28:1–4, Jhn 16:4, Amo 3:14–15, Isa 48:3, Hos 11:5–6
- 10Deu 19:14, Psa 32:6, Psa 93:3–4, Deu 27:17, Pro 17:14, Luk 6:49, 2Ki 16:7–9, Ezk 7:8
- 11Mic 6:16, Deu 28:33, 1Ki 12:26–33, 2Ki 15:16–20, 2Ki 15:29, Amo 5:11–12
- 12Isa 51:8, Job 13:28, Jon 4:7, Pro 12:4, Mrk 9:43–48, Isa 50:9
- 13Jer 30:12, Hos 7:11, Hos 10:6, 2Ki 15:19, Hos 12:1, Jer 30:14–15, Hos 8:9, Mic 1:9
- 14Mic 5:8, Psa 7:2, Hos 13:7–8, Psa 50:22, Amo 3:4–8, Amo 2:14, Isa 5:29, Job 10:16
- 15Isa 26:16, Jer 29:12–14, Psa 78:34, Deu 4:29–31, Psa 50:15, Lev 26:40–42, Jer 3:13, Jer 2:27
Topics in this chapter
28
Afflictions and Adversities, Assyria, Backsliders, Beth-Aven, Blindness, Confidence, Ephraim, Example, False Confidence, Holy Spirit, Idolatry, Impenitence, Jareb, Landmarks, Lion, Minister, Christian, Moth, Opportunity, Pride, Ramah, Repentance, Reprobacy, Rulers, Seekers, Sick, the, Sin, Tabor, Wicked (People)