Isaya 29
1 Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
2 Hata hivyo nitauzingira Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
3 Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kujenga ngome yakukuzingira.
4 Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanong’ona maneno yako toka mavumbini.
5 Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini; makundi ya watu wakatili watakuwa kama makapi yanayopeperushwa. Naam, ghafula, mara moja,
6 Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
7 Kisha makundi ya mataifa yote yanayopigana dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzingira kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
8 kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
9 Pigweni na butwaa na mshangae; jifanyeni vipofu wenyewe na msione; leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
10 Mwenyezi Mungu amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu ninyi manabii; amefunika vichwa vyenu ninyi waonaji.
11 Kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa muhuri katika kitabu. Mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa muhuri.”
12 Au mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
13 Bwana asema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
14 Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
15 Ole kwa wale wanaoenda kwenye vilindi virefu kumficha Mwenyezi Mungu mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
16 Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi”? Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote”?
17 Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
18 Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
19 Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Mwenyezi Mungu, wahitaji watafurahi ndani yake Aliye Mtakatifu wa Israeli.
20 Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
21 wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
22 Kwa hiyo hili ndilo Mwenyezi Mungu, aliyemkomboa Ibrahimu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
23 Watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
24 Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”
Cross-references
180
- 1Amo 4:4–5, 2Sa 5:9, Mic 6:6–7, Isa 66:3, Hos 9:4, Hos 8:13, Hos 5:6, Ezk 43:15–16
- 2Isa 5:25–30, Jer 32:28–32, Jer 39:4–5, Lam 2:5, Isa 37:3, Rev 19:17–18, Isa 10:5–6, Isa 10:32
- 3Luk 19:43–44, Ezk 21:22, 2Ki 25:1–4, Mat 22:7, 2Ki 18:17, 2Ki 24:11–12, 2Ki 19:32
- 4Isa 8:19, Psa 44:25, Isa 3:8, Isa 51:23, Isa 2:11–21, Lam 1:9
- 51Th 5:3, Isa 30:13, Isa 37:36, Isa 17:13–14, Isa 31:3, Psa 35:5, Isa 10:16–19, Job 21:18
- 6Mrk 13:8, Mat 24:7, 1Sa 2:10, Rev 11:19, Rev 16:18, Luk 21:11, 1Sa 12:17–18, Isa 28:2
- 7Job 20:8, Zec 12:9, Mic 4:11–12, Zec 12:3–5, Isa 17:14, Psa 73:20, Zec 14:12–15, Rev 20:8–9
- 8Psa 73:20, Isa 44:12, Isa 10:7–16, 2Ch 32:21
- 9Isa 51:21–22, Isa 19:14, Isa 49:26, Isa 33:13–14, Rev 17:6, Isa 28:7–8, Act 13:40–41, Mat 26:45
- 10Rom 11:8, Isa 44:18, 2Th 2:9–12, Isa 30:10, Isa 6:9–10, Act 28:26–27, 2Co 4:4, 1Sa 9:9
- 11Mat 13:11, Dan 12:4, Isa 8:16, Dan 12:9, Mat 11:25, Rev 6:1, Rev 5:1–9, Mat 16:17
- 12Jhn 7:15–16, Isa 29:18, Hos 4:6, Jer 5:4, Isa 28:12–13
- 13Ezk 33:31–33, Jer 12:2, Mrk 7:2–13, Mat 15:2–9, Jer 3:10, Isa 58:2–3, Pro 30:6, Jer 5:2
- 14Hab 1:5, 1Co 1:19–24, Isa 28:21, Jhn 9:39–41, Jer 49:7, Jhn 9:29–34, Job 5:13, Luk 10:24
- 15Ezk 8:12, Isa 47:10, Isa 30:1, Psa 94:7–9, Zep 1:12, Psa 59:7, Isa 28:15, Ezk 9:9
- 16Rom 9:19–21, Isa 64:8, Isa 45:9–11, Psa 94:8–9, Jer 18:1–10, Isa 24:1
- 17Isa 32:15, Mat 19:30, Heb 10:37, Psa 107:33, Zec 11:1–2, Ezk 20:46–47, Psa 107:35, Isa 55:13
- 18Mat 11:5, Isa 35:5, Pro 20:12, Eph 1:17–19, Mrk 7:37, Psa 119:18, Isa 32:3, Act 26:18
- 19Jas 2:5, Isa 61:1, Mat 11:29, Psa 25:9, Mat 5:5, Mat 11:5, Psa 37:11, Jas 1:9
- 20Mic 2:1, Isa 28:14–22, Isa 59:4, Luk 16:14, Isa 29:5, Isa 13:3, Luk 23:35, Mrk 2:6–7
- 21Amo 5:10–12, Jas 5:6, Act 3:14, Luk 11:53–54, Pro 28:21, Mic 2:6–7, Jer 26:2–8, Ezk 13:19
- 22Isa 45:17, Isa 51:2, Jer 30:10, Jol 2:27, 1Pe 1:18–19, Isa 54:4, Luk 1:68, Ezk 37:24
- 23Isa 19:25, Eph 2:10, Isa 8:13, Isa 45:11, Isa 49:20–26, Isa 60:21, Isa 5:16, Mat 6:9
- 24Isa 28:7, Luk 15:17–19, Heb 5:2, 1Ti 1:13–15, Rev 20:2–3, Act 6:7, Act 9:19–20, Act 2:37
Topics in this chapter
50
Ariel, Armies, Backsliders, Blasphemy, Blindness, Character, Church, Clay, Commandments, David, Deafness, Dream, Earthquakes, Fear, Formalism, God, Gospel, Humility, Hypocrisy, Infidelity, Isaiah, Israel, Prophecies Concerning, Jerusalem, Jesus, the Christ, Joy, Lebanon, Lion, Malice, Meekness, Minister, Christian, Miracles, Necromancy, Persecution, Poor, Presumption, Prophecy, Quotations and Allusions, Regeneration, Reprobacy, Rulers, Salvation, Scoffing, Siege, Sin, Sorcery, Thunder, Uncharitableness, Ventriloquism, Wisdom, Worship