Isaya 27
1 Katika siku ile, Mwenyezi Mungu ataadhibu kwa upanga wake, upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu; ataadhibu Lewiathani yule nyoka apitaye kwa mwendo laini, Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda; atamuua yule mnyama mkubwa wa baharini.
2 Katika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
3 Mimi, Mwenyezi Mungu, ninalitunza, ninalinywesha maji mfululizo. Ninalichunga usiku na mchana ili mtu yeyote asije akalidhuru.
4 Mimi sijakasirika. Laiti michongoma na miiba ingenikabili! Ningepambana dhidi yake katika vita, ningeichoma moto yote.
5 Au niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio, wao na wafanye amani nami, naam, wafanye amani nami.”
6 Katika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi, Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua, naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
7 Je, Mwenyezi Mungu amempiga vile alivyowapiga wale waliompiga? Je, yeye ameuawa vile walivyouawa wale waliomuua yeye?
8 Kwa vita na kwa kumfukuza unapingana naye: kwa mshindo wake mkali anamfukuza, kama siku ile uvumapo upepo wa mashariki.
9 Kwa hili, basi, hatia ya Yakobo itafanyiwa upatanisho, nalo hili litakuwa matunda ya utimilizo wa kuondolewa kwa dhambi yake: Wakati atayafanya mawe yote ya madhabahu kuwa kama mawe ya chokaa yaliyopondwa vipande vipande, hakuna nguzo za Ashera au madhabahu za kufukizia uvumba zitakazobaki zimesimama.
10 Mji wenye ngome umebaki ukiwa, makazi yaliyotelekezwa, yaliyoachwa kama jangwa. Huko ndama hulisha, huko hujilaza, wanakwanyua matawi yake.
11 Wakati vijiti vyake vimekauka, huvunjwa nao wanawake huja na kuwasha navyo moto. Kwa kuwa hili ni taifa lisilo na ufahamu, kwa hiyo yeye aliyewafanya hana huruma juu yao, Muumba wao hawaoneshi fadhili.
12 Katika siku ile Mwenyezi Mungu atapura kutoka matiririko ya Mto Frati hadi Kijito cha Misri, nanyi ee Waisraeli, mtakusanywa mmoja mmoja.
13 Katika siku ile tarumbeta kubwa italia. Wale waliokuwa wakiangamia katika nchi ya Ashuru, nao wale waliokuwa uhamishoni katika nchi ya Misri watakuja na kumwabudu Mwenyezi Mungu katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.
Cross-references
102
- 1Isa 51:9, Isa 66:16, Ezk 29:3, Rev 12:3–13:2, Psa 104:26, Rev 20:2, Job 26:13, Psa 74:13–14
- 2Jer 2:21, Num 21:17, Psa 80:8–19, Luk 20:9–18, Mat 21:33–46, Isa 5:1–7
- 3Isa 58:11, Jhn 15:1–2, 1Sa 2:9, Psa 121:3–5, Ezk 34:11, Ezk 37:14, Isa 55:10–11, Isa 46:9
- 4Isa 10:17, Heb 6:8, Mat 3:12, Psa 85:3, 2Sa 23:6, Nam 1:3–7, Isa 12:1, Ezk 16:63
- 5Isa 25:4, Job 22:21, Eph 2:16–17, Hos 2:18–20, Isa 57:19, Jos 10:6, Isa 45:24, Isa 56:2
- 6Isa 37:31, Hos 14:5–6, Rom 11:16–26, Hos 2:23, Psa 92:13–15, Isa 54:1–3, Zec 2:11, Jer 30:19
- 7Isa 37:36–38, Nam 3:19, Isa 10:20–25, Isa 14:22–23, Isa 17:3, Jer 30:11–16, Jer 50:33–34, Jer 50:40
- 8Hos 4:1, Ezk 19:12, Jer 4:11, Jer 10:24, Jer 30:11, Jer 46:28, Hos 6:1–2, Jer 2:17–37
- 9Rom 11:27, Isa 48:10, Isa 17:8, Dan 11:35, Heb 12:9–11, Isa 4:4, 1Co 11:32, 2Ki 25:9
- 10Isa 17:2, Isa 32:13–14, Isa 17:9, Jer 26:18, Mic 3:12, Jer 26:6, Isa 25:2, Lam 5:18
- 11Isa 43:1, Isa 43:7, Jer 8:7, Isa 44:24, Isa 1:3, Mat 3:10, Jer 4:22, Ezk 9:10
- 12Gen 15:18, Isa 56:8, Neh 1:9, Deu 30:3–4, Amo 9:9, Isa 11:11–16, Jer 3:14, Psa 72:8
- 13Mat 24:31, Lev 25:9, Isa 19:23–25, Heb 12:22, Luk 4:18, Isa 11:16, Zec 14:16, 1Ch 15:24