Waebrania 12
1 Kwa sababu hii, kwa kuwa tumezungukwa na wingu kubwa namna hii la mashahidi, basi na tuweke kando kila kitu kinachotuzuia na ile dhambi inayotuzinga kwa urahisi, nasi tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa kwa ajili yetu.
2 Basi na tumtazame sana Isa mwanzilishi na mkamilishaji wa imani yetu, yeye ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake alistahimili msalaba, bila kujali aibu ya huo msalaba, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.
3 Mtafakarini sana yeye aliyestahimili upinzani mkuu namna hii kutoka kwa watu wenye dhambi, ili msije mkachoka na kukata tamaa.
4 Katika kushindana kwenu dhidi ya dhambi, bado hamjapigana kiasi cha kumwaga damu yenu.
5 Nanyi mmesahau yale maneno ya kuwaonya yanayowataja ninyi kuwa wana, yakisema: “Mwanangu, usidharau adhabu ya Mwenyezi Mungu, wala usikate tamaa akikukemea,
6 kwa sababu Mwenyezi Mungu huwaadibisha wale anaowapenda, na humwadhibu kila mmoja anayemkubali kuwa mwana.”
7 Vumilieni taabu kwa ajili ya kufunzwa adabu. Mungu anawatendea ninyi kama watoto wake, kwa maana ni mtoto yupi asiyeadibishwa na mzazi wake?
8 Kama hakuna kuadibishwa (ambalo ni fungu la watoto wote), basi ninyi ni watoto haramu, wala si watoto halali.
9 Tena, sisi sote tunao baba wa kimwili, waliotuadibisha nasi tukawaheshimu kwa ajili ya hilo. Je, si inatupasa kujinyenyekeza zaidi kwa Baba wa roho zetu ili tuishi?
10 Baba zetu walituadibisha kwa kitambo kidogo kama wao wenyewe walivyoona vyema, lakini Mungu hutuadibisha kwa faida yetu ili tupate kushiriki utakatifu wake.
11 Kuadibishwa wakati wowote hakuonekani kuwa kitu cha kufurahisha bali chenye maumivu kinapotekelezwa. Lakini baadaye huzaa matunda ya haki na amani kwa wale waliofunzwa nayo.
12 Kwa hiyo, itieni nguvu mikono yenu iliyo dhaifu na magoti yenu yaliyolegea.
13 Sawazisheni mapito ya miguu yenu, ili kitu kilicho kiwete kisidhoofishwe bali kiponywe.
14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote na huo utakatifu, ambao bila kuwa nao hakuna mtu atakayemwona Bwana.
15 Chungeni sana mtu yeyote asiikose neema ya Mungu, na kwamba shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.
16 Chungeni miongoni mwenu asiwepo mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, ambaye kwa ajili ya mlo mmoja aliuza haki ya uzaliwa wake wa kwanza.
17 Baadaye kama mnavyofahamu, alipotaka kurithi ile baraka, alikataliwa, maana hakupata nafasi ya kutubu, ingawa aliitafuta kwa machozi.
18 Hamjaufikia mlima ule uwezao kuguswa na ambao unawaka moto; wala kwenye giza, utusitusi na dhoruba;
19 kwenye mlio wa tarumbeta, au kwenye sauti isemayo maneno ya kutisha kiasi ambacho wale walioisikia waliomba wasiambiwe neno jingine zaidi,
20 kwa sababu hawangeweza kustahimili neno lile lililoamriwa: “Hata mnyama akigusa mlima huu, atapigwa mawe.”
21 Waliyoyaona yalikuwa ya kutisha kiasi kwamba Musa alisema, “Ninatetemeka kwa hofu.”
22 Lakini ninyi mmekuja Mlima Sayuni, Yerusalemu ya mbinguni, mji wa Mungu aliye hai. Mmekuja penye kusanyiko kubwa la malaika maelfu kwa maelfu wasiohesabika wanaoshangilia,
23 kwenye jumuiya ya waumini ya wazaliwa wa kwanza wa Mungu, ambao majina yao yameandikwa mbinguni. Mmekuja kwa Mungu, mhukumu wa watu wote, kwenye roho za wenye haki waliokamilishwa,
24 kwa Isa mpatanishi wa agano jipya, na kwa damu iliyonyunyizwa, ile inenayo mambo mema kuliko damu ya Habili.
25 Angalieni msije mkamkataa yeye anenaye. Ikiwa wao hawakuepuka adhabu walipomkataa yeye aliyewaonya hapa duniani, sisi je, tutaokokaje tusipomsikiliza yeye anayetuonya kutoka mbinguni?
26 Wakati ule sauti yake ilitetemesha dunia, lakini sasa ameahidi, “Kwa mara moja tena nitatetemesha si nchi tu bali na mbingu pia.”
27 Maneno haya “kwa mara moja tena” yanaonesha kuondoshwa kwa vile vitu vinavyoweza kutetemeshwa, yaani vile vitu vilivyoumbwa, kwa kusudi vile vitu visivyoweza kutetemeshwa vibaki.
28 Kwa hiyo, kwa kuwa tunapokea ufalme ambao hauwezi kutetemeshwa, basi na tuwe na shukrani, na hivyo tumwabudu Mungu kwa namna inayompendeza, kwa unyenyekevu na uchaji,
29 kwa kuwa “Mungu wetu ni moto ulao.”
Cross-references
225
- 12Ti 4:7, 1Co 9:24–27, Php 2:16, Luk 21:34, Heb 10:35–39, Php 3:10–14, Gal 5:7, 1Pe 2:1
- 2Mic 7:7, 1Pe 3:18, 1Pe 2:23–24, Heb 1:3, Php 1:6, Eph 5:2, Heb 9:28, Tit 2:13–14
- 3Gal 6:9, 2Co 4:16, Rev 2:3, 1Co 15:58, Heb 12:2, Heb 3:1, Jhn 15:18–24, 2Co 4:1
- 41Co 10:13, Heb 10:32–34, Rev 2:13, Mat 24:9, 2Ti 4:6–7, Heb 12:2, Rev 12:11, Rev 18:24
- 5Pro 3:11–12, Job 5:17–18, Rev 3:19, 1Co 11:32, Psa 94:12, Jas 1:12, 2Co 4:8–9, Psa 119:109
- 6Rev 3:19, Pro 3:12, Psa 119:75, Pro 13:24, Psa 94:12, 2Sa 7:14, Jer 10:24, Heb 12:7–8
- 7Pro 19:18, Deu 8:5, Pro 13:24, Pro 29:15, Pro 29:17, Pro 23:13–14, 2Sa 7:14, Job 34:31–32
- 8Heb 12:6, 1Pe 5:9–10, Psa 73:1, Psa 73:14–15
- 9Num 16:22, Num 27:16, Isa 42:5, Jhn 3:6, Job 12:10, Zec 12:1, Isa 38:16, Exo 20:12
- 102Pe 1:4, Lev 11:44–45, Tit 2:14, Eph 5:26–27, Ezk 36:25–27, Lev 19:2, Psa 17:15, Col 1:22
- 11Rom 5:3–5, 2Co 4:17, Heb 12:5–6, 1Pe 1:6, Heb 12:10, Psa 118:18, Isa 32:17, Pro 19:18
- 12Isa 35:3, Heb 12:3, Job 4:3–4, 1Th 5:14, Ezk 21:7, Ezk 7:17, Heb 12:5, Dan 5:6
- 13Pro 4:26–27, Gal 6:1, Isa 35:3, Isa 35:6, Isa 40:3–4, Jas 5:16, Jud 1:22–23, Luk 3:5
- 142Co 7:1, 1Pe 1:15–16, 1Th 4:7, Mat 5:8–9, 1Pe 3:11, Rom 12:18, Pro 16:7, Rom 14:19
- 15Heb 3:12, Deu 29:18, Gal 5:4, 2Co 6:1, 2Jn 1:8, 1Co 15:33, Heb 4:1, Pro 4:23
- 16Gen 25:31–34, 1Co 6:15–20, Heb 13:4, Rev 22:15, Mrk 7:21, 1Th 4:3–7, Act 15:29, Eph 5:5
- 17Pro 1:24–31, Mat 25:11–12, Mat 7:23, Heb 6:8, Heb 10:26–29, Gen 27:30–41, Luk 13:24–27, Jer 6:30
- 18Deu 4:11, Exo 24:17, Deu 5:22–26, Exo 20:18, 2Co 3:9, Rom 6:14, Exo 19:12–22, 2Ti 1:7
- 19Deu 18:16, 1Co 15:52, Exo 20:1–19, Deu 4:12, Deu 4:33, Deu 5:3–22, Exo 20:22, Exo 19:16–19
- 20Exo 19:12–13, Gal 2:19, Deu 33:2, Gal 3:10, Exo 19:16, Rom 3:19–20
- 21Exo 19:16, Deu 9:19, Isa 6:3–5, Psa 119:120, Rev 1:17, Exo 19:19, Dan 10:17, Dan 10:8
- 22Php 3:20, Gal 4:26, Psa 48:2, Rev 14:1, Isa 51:11, Rev 21:2, Heb 11:10, Rev 3:12
- 23Jas 1:18, Heb 11:40, Luk 10:20, Rev 20:15, Rev 14:4, Exo 4:22, Gen 18:25, Psa 94:2
- 24Heb 9:15, Heb 11:28, Heb 8:6, Heb 11:4, Mat 23:35, 1Ti 2:5, Gen 4:10, Mat 26:28
- 25Heb 8:5, Heb 2:1–3, Deu 30:17, Zec 7:11, Pro 13:18, Heb 11:7, Exo 20:22, Pro 8:33
- 26Hag 2:6–7, Isa 13:13, Exo 19:18, Isa 2:19, Jol 3:16, Psa 114:6–7, Heb 12:27, Hab 3:10
- 27Mat 24:35, 1Co 7:31, Rev 21:1, Rev 11:15, 2Pe 3:10–11, Ezk 21:27, Psa 102:26–27
- 28Rom 12:1–2, Psa 2:11, Heb 13:15, Dan 2:44, Heb 4:16, Heb 10:22–23, Rev 1:6, Psa 19:14
- 29Deu 4:24, Deu 9:3, 2Th 1:8, Isa 66:15, Heb 10:27, Exo 24:17, Dan 7:9, Psa 97:3
Topics in this chapter
76
Abel, Adoption, Afflictions and Adversities, Angel (A Spirit), Assurance, Atonement, Backsliders, Bastard, Birthright, Blessing, Blood, Chastisement, Children, Church, Cities, Constancy, Covenant, Cross, Darkness, Decision, Despondency, Diligence, Earthquakes, Esau, Escape, Example, Faith, Fear, Firstborn, Forgetting God, Games, Gluttony, God, Gospel, Heaven, Holiness, Impenitence, Influence, Jacob, Jesus, the Christ, Judgment, Judgments, Lameness, Law, Meekness, Parents, Patience, Peace, Persecution, Perseverance, Prophecy, Punishment, Quotations and Allusions, Race, Repentance, Reprobacy, Resignation, Reward, Righteous, Sanctification, Shame, Sin, Sprinkling, Straight, Symbols and Similitudes, Temptation, Throne, Thunder, Trumpet, Types, Unbelief, Vision, Watchfulness, Worldliness, Worship, Zion