Marko 8
1 Katika siku hizo, umati mkubwa wa watu walikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Isa akawaita wanafunzi wake akawaambia,
2 “Ninahurumia umati huu wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.
3 Nikiwaaga waende nyumbani bila kula, watazimia njiani kwa sababu baadhi yao wametoka mbali.”
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
5 Isa akawauliza, “Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Tuna mikate saba.”
6 Akawaambia watu waketi chini. Akaichukua ile mikate saba na kushukuru, baadaye akaimega na kuwapa wanafunzi wake ili wawagawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo.
7 Walikuwa pia na visamaki vichache, Isa akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu.
8 Wale watu walikula na kutosheka. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
9 Watu waliokula walikuwa wapata elfu nne. Baada ya kuwaaga,
10 aliingia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda sehemu za Dalmanutha.
11 Mafarisayo wakaja, wakaanza kumhoji Isa. Ili kumtega, wakamwomba awaoneshe ishara kutoka mbinguni.
12 Akahuzunika moyoni, akawaambia, “Kwa nini kizazi hiki kinataka ishara? Amin nawaambieni, hakitapewa ishara yoyote.”
13 Kisha akawaacha, akarudi kwenye mashua, akavuka hadi ng’ambo.
14 Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate ya kutosha. Walikuwa na mkate mmoja tu kwenye mashua.
15 Isa akawaonya: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na ya Herode.”
16 Wakajadiliana wao kwa wao, na kusema, “Anasema hivi kwa sababu hatukuleta mikate.”
17 Isa, akifahamu majadiliano yao, akawauliza: “Mbona mnajadiliana kuhusu kutokuwa na mikate? Je, bado hamtambui wala hamwelewi? Je, mbona mioyo yenu ni migumu kiasi hicho?
18 Je, mna macho lakini mnashindwa kuona, na mna masikio lakini mnashindwa kusikia? Je, hamkumbuki?
19 Nilipoimega ile mikate mitano kwa watu elfu tano, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa mabaki?” Wakamjibu, “Kumi na viwili.”
20 “Je, nilipoimega ile mikate saba kwa watu elfu nne, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa mabaki?” Wakamjibu, “Saba.”
21 Ndipo akawauliza, “Je, bado hamwelewi?”
22 Wakafika Bethsaida na baadhi ya watu wakamleta mtu mmoja kipofu wakamsihi Isa amguse.
23 Isa akamshika mkono huyo kipofu akampeleka nje ya kijiji. Baada ya kuyatemea mate macho ya yule kipofu na kumwekea mikono, Isa akamuuliza, “Unaona chochote?”
24 Yule kipofu akaangalia, akasema, “Ninaona watu, wanaonekana kama miti inayotembea.”
25 Isa akamwekea tena mikono machoni. Kisha macho yake yakafunguka, kuona kwake kukarejea naye akaona kila kitu dhahiri.
26 Isa akamtuma nyumbani mwake, akamwambia, “Hata kijijini usiingie.”
27 Isa na wanafunzi wake wakaelekea vijiji vya Kaisaria-Filipi. Walipokuwa njiani, Isa akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
28 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yahya, wengine husema ni Ilya, na bado wengine husema wewe ni mmoja wa manabii.”
29 Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Al-Masihi.”
30 Isa akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
31 Ndipo akaanza kuwafundisha wanafunzi wake kuwa Mwana wa Adamu lazima atapata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa Torati, na kwamba itampasa auawe lakini baada ya siku tatu afufuliwe.
32 Aliyasema haya waziwazi. Ndipo Petro akamchukua kando na akaanza kumkemea.
33 Lakini Isa akageuka na kuwaangalia wanafunzi wake, na akamkemea Petro. Akasema, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
34 Ndipo akawaita umati ule wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
35 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili atayaokoa.
36 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake?
37 Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
38 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”
Cross-references
225
- 1Mat 15:32–39, Mrk 6:34–44
- 2Mat 9:36, Mic 7:19, Psa 103:13, Psa 145:15, Heb 5:2, Luk 7:13, Mrk 5:19, Heb 4:15
- 3Isa 40:31, Jdg 8:4–6, 1Sa 14:28–31, 1Sa 30:10–12
- 4Mat 15:33, Mrk 6:52, Psa 78:19–20, Mrk 6:36–37, 2Ki 7:2, Num 11:21–23, Jhn 6:7–9, 2Ki 4:42–44
- 5Mat 14:15–17, Mrk 6:38, Mat 15:34, Luk 9:13
- 6Col 3:17, Mat 14:18–19, Mat 15:35–36, Jhn 6:10–11, 1Co 10:30–31, Rom 14:6, Jhn 6:23, Jhn 2:5
- 7Mat 14:19, Luk 6:41, Luk 24:41–42, Jhn 21:5, Jhn 21:8–9
- 8Mat 16:10, Psa 145:16, Psa 107:8–9, Mrk 8:19–20, 2Ki 4:42–44, 2Ki 4:2–7, Jhn 6:32–35, Luk 1:53
- 10Mat 15:39
- 11Mat 12:38, Jhn 4:48, 1Co 10:9, Exo 17:7, 1Co 1:22–23, Mal 3:15, Luk 11:16, Deu 6:16
- 12Mat 12:39–40, Mat 16:4, Mrk 7:34, Jhn 12:37–43, Luk 11:29–30, Luk 22:67–70, Mrk 3:5, Mrk 6:6
- 13Act 18:6, Jhn 8:21, Psa 81:12, Hos 4:17, Luk 8:37, Mat 7:6, Hos 9:12, Jhn 12:36
- 14Mat 16:5
- 151Co 5:6–8, Mat 16:6, Mat 16:11–12, Mrk 12:13, Luk 12:1–2, Pro 19:27, Lev 2:11, Exo 12:18–20
- 16Luk 20:5, Luk 9:46, Mat 16:7–8
- 17Mrk 6:52, Heb 5:11–12, Mrk 2:8, Isa 63:17, Mrk 3:5, Mat 16:8–9, Luk 24:25, Mat 15:17
- 18Act 28:26–27, Mat 13:14–15, Jer 5:21, Mrk 4:12, Ezk 12:2, Jhn 12:40, Isa 6:9–10, Isa 42:18–20
- 19Mrk 6:38–44, Mat 14:17–21, Luk 9:12–17, Jhn 6:5–13
- 20Mat 15:34–38, Mrk 8:1–9
- 21Mrk 6:52, Psa 94:8, Mrk 8:17, 1Co 15:34, Jhn 14:9, 1Co 6:5, Mrk 8:12, Mat 16:11–12
- 22Mat 11:21, Mrk 6:45, Luk 10:13, Mrk 2:3, Mat 8:15, Jhn 1:44, Mat 9:29, Jhn 12:21
- 23Mrk 7:33, Jhn 9:6–7, Mrk 5:23, Act 9:8, Isa 51:18, Isa 44:2, Rev 3:18, Jer 31:32
- 24Isa 29:18, 1Co 13:9–12, Isa 32:3, Jdg 9:36
- 25Php 1:6, Pro 4:18, 2Pe 3:18, 1Pe 2:9, Mat 13:12
- 26Mat 8:4, Mrk 8:23, Mrk 7:36, Mat 9:30, Mrk 5:43, Mat 12:16
- 27Mat 16:13–20, Luk 9:18–20
- 28Jhn 1:21, Mat 14:2, Mrk 9:11–13, Mal 4:5, Luk 9:7–9, Mrk 6:14–16, Mat 16:14
- 291Jn 4:15, Mat 16:15–16, 1Jn 5:1, Luk 9:20, Jhn 11:27, Act 9:20, Jhn 4:42, Jhn 1:41–49
- 30Mat 16:20, Luk 9:21, Mrk 9:9, Mrk 7:36, Mat 8:4, Mrk 8:26
- 31Mrk 10:33–34, Jhn 2:19, Luk 24:26, 1Sa 10:19, Mrk 9:31–32, Act 7:35, Mat 16:21–28, Luk 17:25
- 32Mat 16:22, Jhn 16:25, Jhn 16:29, Jhn 18:20, Luk 10:40, Jhn 13:6–8, Mrk 4:38
- 33Mat 4:10, Php 3:19, 1Jn 2:15, Jas 3:15–18, Gen 3:4–6, Mat 6:31–32, Rom 8:5–8, Psa 141:5
- 34Mat 10:38, Luk 14:26–27, Jhn 10:27, Gal 5:24, 1Ki 14:8, Gal 2:20, 1Jn 3:16, Num 14:24
- 352Ti 2:11–13, 1Co 9:23, Luk 17:33, Mat 16:25, 2Ti 1:8, Mat 10:39, Jhn 12:25–26, Luk 9:24
- 36Mat 16:26, Luk 9:25, Psa 49:17, Jas 1:9–11, Php 3:7–9, Luk 12:19–20, Heb 11:24–26, Rom 6:21
- 37Psa 49:7–8, 1Pe 1:18–19
- 38Luk 12:8–9, Rom 1:16, 1Jn 2:23, Jas 4:4, Luk 9:26, Mat 10:32–33, Mat 26:64, 2Ti 1:8
Parallel passages
1
- Peter's Confession of ChristMat 16:13–20, Mrk 8:27–30, Luk 9:18–21
Topics in this chapter
36
Angel (A Spirit), Apostles, Backsliders, Bethsaida, Blindness, Bread, Caesarea Philippi, Commandments, Cross, Dalmanutha, Food, God, Government, Hypocrisy, Jesus, the Christ, Judgment, Leaven (Yeast), Life, Miracles, Paradox, Peter, Prayer, Presumption, Prudence, Reproof, Righteous, Self-Denial, Self-Righteousness, Shame, Sign, Spitting, Stoicism, Thankfulness, Unbelief, Wicked (People), Worldliness