Isaya 42
1 “Huyu hapa mtumishi wangu, ninayemtegemeza, mteule wangu, ninayependezwa naye; nitaweka Roho yangu juu yake, naye ataleta haki kwa mataifa.
2 Hatapaza sauti wala kupiga kelele, wala hataipaza sauti yake barabarani.
3 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima. Kwa uaminifu ataleta haki,
4 hatazimia roho wala kukata tamaa, hadi atakaposimamisha haki juu ya dunia. Visiwa vitaweka tumaini lao katika sheria yake.”
5 Hili ndilo asemalo Mungu, Mwenyezi Mungu, yeye aliyeziumba mbingu na kuzitanda, aliyeitandaza dunia na vyote vinavyotoka humo, awapaye watu wake pumzi, na uzima kwa wale wanaoenda humo:
6 “Mimi, Mwenyezi Mungu, nimekuita katika haki; nitakushika mkono wako. Nitakulinda na kukufanya kuwa agano kwa ajili ya watu na nuru kwa Mataifa,
7 kuwafungua macho wale wasioona, kuwaacha huru kutoka kifungoni wale waliofungwa, na kuwafungua kutoka gerezani wale wanaokaa gizani.
8 “Mimi ndimi Mwenyezi Mungu; hilo ndilo Jina langu! Sitampa mwingine utukufu wangu wala sanamu sifa zangu.
9 Tazama, mambo ya kwanza yametokea, nami natangaza mambo mapya; kabla hayajatokea nawatangazia habari zake.”
10 Mwimbieni Mwenyezi Mungu wimbo mpya, sifa zake toka miisho ya dunia, ninyi mshukao chini baharini, na vyote vilivyomo, enyi visiwa na wote wanaoishi humo.
11 Jangwa na miji yake na vipaze sauti zao; makazi anamoishi Kedari na yashangilie. Watu wa Sela waimbe kwa furaha, na wapige kelele kutoka vilele vya milima.
12 Wampe Mwenyezi Mungu utukufu, na kutangaza sifa zake katika visiwa.
13 Mwenyezi Mungu ataenda kama mtu mwenye nguvu, kama shujaa atachochea shauku yake, kwa kishindo ataamsha ukelele wa vita, naye atashinda adui zake.
14 “Kwa muda mrefu nimenyamaza; nimekaa kimya na kujizuia. Lakini sasa, kama mwanamke wakati wa kujifungua, ninapiga kelele, ninatweta na kushusha pumzi.
15 Nitaharibu milima na vilima na kukausha mimea yako yote; nitafanya mito kuwa visiwa na kukausha mabwawa.
16 Nitawaongoza vipofu kwenye njia ambayo hawajaijua, kwenye mapito wasiyoyazoea nitawaongoza; nitafanya giza kuwa nuru mbele yao, na kufanya mahali palipoparuza kuwa laini. Haya ndio mambo nitakayofanya; mimi sitawaacha.
17 Lakini wale wanaotumaini sanamu, wanaoviambia vinyago, ‘Ninyi ndio miungu yetu,’ watarudishwa nyuma kwa aibu kubwa.
18 “Sikieni, enyi viziwi; tazameni, enyi vipofu, mpate kuona!
19 Ni nani aliye kipofu isipokuwa mtumishi wangu, na kiziwi kama mjumbe ninayemtuma? Ni nani aliye kipofu kama yeye aliyejitoa kwangu, aliye kipofu kama mtumishi wa Mwenyezi Mungu?
20 Mmeona vitu vingi, lakini hamkuzingatia; masikio yenu yako wazi, lakini hamsikii chochote.”
21 Ilimpendeza Mwenyezi Mungu kwa ajili ya haki yake kufanya sheria yake kuwa kuu na tukufu.
22 Lakini hili ni taifa lililoibwa na kutekwa nyara, wote wamenaswa katika mashimo, au wamefichwa katika magereza. Wamekuwa nyara, wala hapana yeyote awaokoaye. Wamefanywa mateka, wala hapana yeyote asemaye, “Warudishe.”
23 Ni nani miongoni mwenu atakayesikiliza hili, au atakayezingatia kwa makini katika wakati ujao?
24 Ni nani aliyemtoa Yakobo kuwa mateka, na Israeli kwa wateka nyara? Je, hakuwa yeye, Mwenyezi Mungu, ambaye tumetenda dhambi dhidi yake? Kwa kuwa hawakufuata njia zake, hawakutii sheria zake.
25 Hivyo akawamwagia hasira yake inayowaka, ukali wa vita. Iliwazunguka kwa miali ya moto, lakini hata hivyo hawakuelewa; iliwateketeza, lakini hawakuyatia moyoni.
Cross-references
198
- 1Mat 12:18–21, Luk 3:22, Isa 52:13, Isa 61:1, Isa 43:10, Php 2:7, Mat 17:5, Mat 3:16–17
- 2Mat 12:16–20, 2Ti 2:24, 1Pe 2:23, Mat 11:29, Luk 17:20, Zec 9:9
- 3Ezk 34:16, Jer 31:25, Isa 40:11, Psa 147:3, Mat 11:28, Jhn 5:30, Isa 11:3–4, Rev 19:11
- 4Isa 55:5, Isa 53:2–12, Gen 49:10, Psa 22:27, Isa 52:13–15, Isa 9:7, Mat 12:21, Isa 11:9–12
- 5Isa 40:22, Isa 45:12, Jer 10:12, Zec 12:1, Isa 48:13, Psa 104:2–35, Isa 44:24, Psa 102:25–26
- 6Jhn 8:12, Luk 2:32, Isa 26:3, Act 13:47, Isa 49:8, Isa 49:6, 1Pe 2:9, Isa 60:1–3
- 7Eph 1:17–18, Isa 61:1, Isa 35:5, Isa 49:9, 2Ti 2:26, Mat 11:5, Heb 2:14–15, Luk 24:45
- 8Isa 48:11, Isa 43:11, Exo 34:14, Exo 20:3–5, Psa 83:18, Exo 3:13–15, Exo 4:5, Jhn 5:23
- 9Isa 43:19, Isa 46:9–10, Jhn 13:19, 2Pe 1:19–21, Isa 44:7–8, Jos 23:14–15, Jos 21:45, 1Ki 8:15–20
- 10Psa 33:3, Isa 42:4, Rom 15:9–11, Psa 40:3, Psa 98:1–4, Rev 5:9, Isa 49:13, Psa 96:11
- 11Isa 32:16, Isa 60:7, Psa 72:8–10, Isa 41:18–19, Isa 35:6, Isa 21:16, Isa 16:1, Psa 120:5
- 12Rom 15:9–11, Psa 117:1–2, Isa 66:18–19, Isa 24:15–16, Isa 42:4, Rev 7:9–12, Rev 5:9–10, Psa 22:27
- 13Exo 15:1–3, Psa 78:65, Isa 59:16–19, Amo 1:2, Zep 3:8, Psa 110:5–6, Jer 25:30, Zep 1:18
- 14Jer 44:22, Ecc 8:11–12, 2Pe 3:15, Psa 83:1–2, 2Pe 3:9–10, Jer 15:6, Luk 18:7, Job 32:18
- 15Isa 50:2, Nam 1:4–6, Isa 44:27, Rev 20:11, Isa 2:12–16, Jer 4:24, Rev 16:12, Isa 49:11
- 16Isa 30:21, Luk 3:5, Isa 35:8, Isa 60:19–20, Isa 40:4, Luk 1:78–79, Eph 5:8, Isa 32:3
- 17Psa 97:7, Isa 44:11, Isa 1:29, Isa 45:16–17, Isa 44:17, Exo 32:4, Exo 32:8, Hab 2:18–20
- 18Isa 43:8, Isa 29:18, Pro 20:12, Mrk 7:34–37, Isa 35:5, Exo 4:11, Luk 7:22, Rev 3:17–18
- 192Co 4:4, Jer 5:21, Ezk 12:2, Jhn 9:41, Isa 41:8, Isa 6:9, Mat 15:14–16, Rom 2:17–23
- 20Deu 29:2–4, Isa 48:6–8, Mrk 6:19–20, Ezk 33:31, Jer 42:2–5, Psa 107:43, Jer 6:10, Isa 1:3
- 21Rom 3:31, Heb 8:10, Mat 5:17–20, Rom 7:12, Isa 42:4, Psa 40:8, Isa 46:12–13, Isa 1:24–27
- 22Psa 102:20, Jer 50:17, Isa 51:23, Isa 24:22, Psa 50:22, Isa 42:7, Isa 52:4–5, Jer 51:34–35
- 23Isa 48:18, Act 3:22–23, Lev 26:40–42, 1Pe 4:2–3, Jer 3:13, Deu 4:29–31, Jer 3:4–7, Mat 21:28–31
- 24Isa 59:1–2, Lam 1:14, Isa 30:15, 2Ch 36:17, Jer 5:15, Isa 47:6, Lam 1:18, Jdg 2:14
- 25Isa 57:11, Hos 7:9, Mal 2:2, Ezk 7:8–9, Nam 1:6, Rev 9:18–21, Jer 5:3, Deu 32:22
Topics in this chapter
37
Afflictions and Adversities, Anger, Arabians, Backsliders, Blindness, Chastisement, Church, Darkness, Depravity of Man, Election, Flax, Gentiles, Gifts From God, Glorifying God, Glory, God, Gospel, Heaven, Holy Spirit, Idolatry, Impenitence, Isaiah, Jesus, the Christ, Justification, Kedar, Man, Mariners (Sailors), Meekness, Praise, Prophecy, Quotations and Allusions, Reed, Regeneration, Self-Will, Trinity, Waiting, Wisdom