Sefania 3
1 Ole mji wa wadhalimu, waasi na waliotiwa unajisi!
2 Hautii mtu yeyote, haukubali maonyo. Haumtumaini Mwenyezi Mungu, haukaribii karibu na Mungu wake.
3 Maafisa wake ni simba wanaonguruma, watawala wake ni mbwa-mwitu wa jioni, ambao hawabakizi chochote kwa ajili ya asubuhi.
4 Manabii wake ni wenye kiburi, ni wadanganyifu. Makuhani wake hunajisi patakatifu na kuihalifu sheria.
5 Mwenyezi Mungu aliye ndani yake ni mwenye haki, hafanyi kosa. Asubuhi kwa asubuhi hutoa haki yake, kila kukipambazuka huitimiza, bali mtu dhalimu hana aibu.
6 “Nimeyaangamiza mataifa, ngome zao zimebomolewa. Nimeziacha barabara ukiwa, hakuna anayepita humo. Miji yao imeharibiwa; hakuna mmoja atakayeachwa: hakuna hata mmoja.
7 Niliuambia huo mji, ‘Hakika utaniogopa na kukubali maonyo!’ Ndipo makao yake hayatafutiliwa mbali, wala adhabu zangu zote hazitakuja juu yake. Lakini walikuwa bado na shauku kutenda kwa upotovu katika yote waliyofanya.”
8 Mwenyezi Mungu anasema, “Kwa hiyo ningojee mimi, siku nitakayosimama kuteka nyara. Nimeamua kukusanya mataifa, kukusanya falme na kumimina ghadhabu yangu juu yao, hasira yangu kali yote. Dunia yote itateketezwa kwa moto wa hasira yangu yenye wivu.
9 “Ndipo nitatakasa midomo ya mataifa, kwamba wote waweze kuliitia jina la Mwenyezi Mungu na kumtumikia kwa pamoja.
10 Kutoka ng’ambo ya mito ya Kushi watu wangu wanaoniabudu, watu wangu waliotawanyika, wataniletea sadaka.
11 Siku hiyo hutaaibishwa kwa ajili ya makosa yote uliyonitendea, kwa sababu nitawaondoa kutoka mji huu wale wote wanaoshangilia katika kiburi chao. Kamwe hutajivuna tena katika kilima changu kitakatifu.
12 Lakini nitakuachia ndani yako wapole na wanyenyekevu, ambao wanatumaini jina la Mwenyezi Mungu.
13 Mabaki ya Israeli hayatafanya kosa; hawatasema uongo, wala udanganyifu hautakuwa katika vinywa vyao. Watakula na kulala wala hakuna yeyote atakayewaogopesha.”
14 Imba, ee Binti Sayuni; paza sauti, ee Israeli! Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, ee Binti Yerusalemu!
15 Mwenyezi Mungu amekuondolea adhabu yako, amewarudisha nyuma adui zako. Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Israeli, yu pamoja nawe; kamwe hutaogopa tena madhara yoyote.
16 Katika siku hiyo watauambia Yerusalemu, “Usiogope, ee Sayuni; usiiache mikono yako ilegee.
17 Mwenyezi Mungu, Mungu wako, yu pamoja nawe, yeye ni Shujaa mwenye nguvu anayeokoa. Atakufurahia kwa furaha kubwa, atakutuliza kwa pendo lake, atakufurahia kwa kuimba.”
18 “Huzuni katika sikukuu zilizoamriwa nitaziondoa kwenu; hizo ni mzigo na fedheha kwenu.
19 Wakati huo nitawaadhibu wote waliokudhulumu; nitaokoa vilema na kukusanya wale waliotawanywa. Nitawapa sifa na heshima katika kila nchi ambayo waliaibishwa.
20 Wakati huo nitawakusanya; wakati huo nitawaleta nyumbani. Nitawapa sifa na heshima miongoni mwa mataifa yote ya dunia wakati nitakapowarudishia mateka yenu mbele ya macho yenu hasa,” asema Mwenyezi Mungu.
Cross-references
160
- 1Jer 6:6, Isa 59:13, Isa 30:12, Ezk 22:7, Mal 3:5, Zec 7:10, Lev 1:16, Isa 5:7
- 2Jer 5:3, Jer 22:21, Psa 73:28, Jer 7:23–28, Psa 78:22, Isa 43:22, Neh 9:26, Pro 5:12
- 3Hab 1:8, Jer 5:6, Ezk 22:25–27, Jer 22:17, Pro 28:15, Mic 3:9–11, Ezk 22:6, Isa 1:23
- 4Ezk 22:26, Hos 9:7, Lam 2:14, Mal 2:8, Isa 9:15, Jer 23:25–27, Isa 56:10–12, Jer 5:31
- 5Deu 32:4, Psa 145:17, Lam 3:23, Zep 3:15, Isa 28:19, Deu 23:14, Isa 12:6, Zep 3:17
- 6Zep 2:5, 1Co 10:6, Isa 37:24–26, 1Co 10:11, Jer 25:9–11, Lev 26:31, Isa 10:1–34, Isa 37:11–13
- 7Hos 9:9, Jer 36:3, Mic 2:1–2, Zep 3:2, Jer 7:7, Jer 25:5, Isa 63:8, Jer 8:6
- 8Zep 1:18, Jol 3:2, Mic 7:7, Psa 27:14, 2Pe 3:10, Hab 2:3, Jol 3:9–16, Rev 16:14
- 9Gen 11:1, Psa 22:27, Isa 19:18, Zec 2:11, Psa 86:9–10, Hab 2:14, Act 2:4–13, Zec 8:20–23
- 10Psa 68:31, Isa 11:11, Isa 18:1, Rom 15:16, 1Pe 1:1, Isa 49:20–23, Act 24:17, Isa 18:7
- 11Isa 54:4, Isa 11:9, Jol 2:26–27, Isa 61:7, Mat 3:9, Dan 9:16, Rom 9:33, 1Pe 2:6
- 12Nam 1:7, Isa 14:32, Zec 13:8–9, Isa 61:1–3, Isa 50:10, Mat 5:3, Jas 2:5, Mat 12:21
- 13Rev 14:5, Mic 4:7, Isa 60:21, Zep 2:7, Mic 4:4, Ezk 34:13–15, Jhn 1:47, Isa 17:2
- 14Isa 12:6, Mic 4:8, Zec 2:10–11, Isa 65:18–19, Psa 95:1–2, Zec 9:9–10, Psa 100:1–2, Isa 65:13–14
- 15Isa 51:22, Isa 60:18, Zep 3:5, Isa 40:1–2, Amo 9:15, Gen 30:23, Ezk 39:29, Isa 33:22
- 16Heb 12:12, Isa 35:3–4, Eph 3:13, Isa 41:10, Gal 6:9, 2Co 4:1, Rev 2:3, Isa 44:2
- 17Psa 149:4, Psa 147:11, Heb 7:25, Isa 62:4–5, Jer 32:41, Isa 12:2, Zep 3:15, Deu 30:9
- 18Psa 42:2–4, Jer 23:3, Zep 3:20, Lam 2:6–7, Lam 1:4, Ezk 36:24, Jer 31:8–9, Psa 63:1–2
- 19Isa 49:25–26, Isa 60:14, Jer 30:16, Zep 3:15, Mic 7:10, Ezk 34:16, Isa 61:7, Mic 4:6–7
- 20Jer 29:14, Mal 3:12, Isa 60:15, Isa 56:5, Amo 9:14, Jol 3:1, Zep 3:19, Ezk 34:16