Isaya 59
1 Hakika mkono wa Mwenyezi Mungu si mfupi hata usiweze kuokoa, wala sikio lake si zito hata lisiweze kusikia.
2 Lakini maovu yenu yamewatenga ninyi na Mungu wenu, dhambi zenu zimewaficha ninyi uso wake, ili asisikie.
3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu kwa hatia. Midomo yenu imenena uongo, nazo ndimi zenu zimenong’ona mambo maovu.
4 Hakuna hata mmoja anayedai kwa haki; hakuna hata mmoja anayetetea kwa haki. Wanategemea mabishano matupu na kusema uongo, huchukua mimba ya magomvi na kuzaa uovu.
5 Huangua mayai ya nyoka wenye sumu kali na kutanda wavu wa buibui. Yeyote alaye mayai yao atakufa, nalo moja likianguliwa, nyoka hutoka humo.
6 Utando wao wa buibui haufai kwa mavazi; hawawezi kujifunika kwa kile walichokitengeneza. Matendo yao ni matendo maovu, vitendo vya jeuri vipo mikononi mwao.
7 Miguu yao hukimbilia kwenye dhambi, ni myepesi kumwaga damu isiyo na hatia. Mawazo yao ni mawazo maovu; uharibifu na maangamizi huonekana katika njia zao.
8 Hawajui njia ya amani, hakuna haki katika mapito yao. Wameyageuza kuwa njia za upotovu, hakuna apitaye njia hizo atakayeifahamu amani.
9 Hivyo uadilifu uko mbali nasi, nayo haki haitufikii. Tunatazamia nuru, kumbe! Yote ni giza, tunatazamia mwanga, lakini tunatembea katika giza nene.
10 Tunapapasa ukuta kama vipofu, tunapapasa katika njia zetu kama watu wasio na macho. Adhuhuri tunajikwaa kama wakati wa gizagiza; kati ya wenye nguvu, tuko kama wafu.
11 Wote tunanguruma kama dubu; tunalia kwa maombolezo kama hua. Tunatafuta haki, kumbe hakuna kabisa; tunatafuta wokovu, lakini uko mbali.
12 Kwa sababu makosa yetu ni mengi machoni pako, na dhambi zetu zinashuhudia dhidi yetu. Makosa yetu yako pamoja nasi daima, nasi tunayatambua maovu yetu:
13 Uasi na udanganyifu dhidi ya Mwenyezi Mungu, kumgeuzia Mungu wetu kisogo, tukichochea udhalimu na maasi, tukinena uongo ambao mioyo yetu imeuhifadhi.
14 Hivyo uadilifu umerudishwa nyuma, nayo haki inasimama mbali, kweli imejikwaa njiani, uaminifu hauwezi kuingia.
15 Kweli haipatikani popote, na yeyote aepukaye uovu huwa mawindo. Mwenyezi Mungu alitazama, naye akachukizwa kwamba hapakuwa na haki.
16 Aliona kuwa hapakuwa hata mtu mmoja, akashangaa kwamba hapakuwa hata mtu mmoja wa kuingilia kati. Hivyo mkono wake mwenyewe ndio uliomfanyia wokovu, nayo haki yake mwenyewe ndiyo iliyomtegemeza.
17 Alivaa haki kama dirii kifuani mwake, na chapeo ya wokovu kichwani mwake, alivaa mavazi ya kisasi naye akajifunga wivu kama joho.
18 Kulingana na kile walichokuwa wametenda, ndivyo atakavyolipa ghadhabu kwa watesi wake na kisasi kwa adui zake, atavilipa visiwa sawa na wanavyostahili.
19 Kuanzia magharibi, watu wataliogopa jina la Mwenyezi Mungu na kuanzia mawio ya jua, watauheshimu utukufu wake. Adui atakapokuja kama mafuriko, Roho wa Mwenyezi Mungu atainua kiwango dhidi yake na kumshinda.
20 “Mkombozi atakuja Sayuni, kwa wale wa Yakobo wanaozitubu dhambi zao,” asema Mwenyezi Mungu.
21 “Bali mimi, hili ndilo agano langu nao,” asema Mwenyezi Mungu. “Roho wangu Mtakatifu, aliye juu yenu, na maneno yangu niliyoyaweka vinywani vyenu, havitaondoka vinywani mwenu, wala kutoka vinywani mwa watoto wenu, wala kutoka vinywani mwa wazao wao, kuanzia sasa na hata milele,” asema Mwenyezi Mungu.
Cross-references
165
- 1Jer 32:17, Isa 50:2, Num 11:23, Isa 65:24, Heb 7:25, Gen 18:14, Mat 13:15, Isa 58:9
- 2Pro 15:29, Jer 5:25, Mic 3:4, Isa 1:15, Deu 31:17–18, Ezk 39:23–24, Deu 32:19–20, Isa 57:17
- 3Isa 1:15, Ezk 13:8, Jer 2:34, Jer 2:30, Isa 1:21, Mic 7:2, Jer 7:8, Ezk 7:23
- 4Job 15:35, Mic 7:2–5, Jas 1:15, Jer 7:8, Jer 7:4, Mic 2:1, Pro 4:16, Isa 59:16
- 5Mat 3:7, Isa 14:29, Job 8:14, Pro 23:32, Mat 12:34
- 6Isa 57:12, Jer 6:7, Rev 3:17–18, Hab 1:2–4, Isa 28:18–20, Job 8:14–15, Mic 2:8, Gen 6:11
- 7Pro 6:17, Rom 3:15–17, Pro 1:16, Mrk 7:21–22, Ezk 9:9, Rev 17:6, Pro 24:9, Jer 22:17
- 8Isa 57:20–21, Rom 3:17, Luk 1:79, Isa 5:7, Psa 58:1–2, Jer 5:1, Hos 4:1–2, Mat 23:23
- 9Isa 5:30, Job 30:26, Lam 5:16–17, Mic 1:12, Amo 5:18–20, Jer 14:19, Hab 1:13, Jer 8:15
- 10Deu 28:29, Job 5:14, Lam 3:6, Pro 4:19, Isa 8:15, Jer 13:16, Jhn 12:35, Lam 4:14
- 11Isa 38:14, Ezk 7:16, Job 30:28–29, Hos 7:14, Psa 38:8, Isa 59:9, Jer 8:15, Psa 85:9
- 12Ezr 9:6, Jer 14:7, Hos 5:5, Isa 1:4, Hos 4:2, Ezk 5:6, 1Th 2:15–16, Hos 7:10
- 13Mrk 7:21–22, Jas 3:6, Heb 3:12, Hos 6:7, Ezk 6:9, Jer 2:19–21, Jer 3:20, Isa 32:6
- 14Ecc 3:16, Hab 1:4, Amo 5:11, Jer 5:27–28, Mic 3:9–11, Jer 5:31, Isa 10:1–2, Isa 5:23
- 15Mic 7:2, Heb 11:36–38, Jer 7:28, 1Jn 3:11–12, Jer 5:1–2, Psa 5:9, Psa 12:1–2, Rom 8:36
- 16Ezk 22:30, Psa 106:23, Psa 98:1, Isa 64:7, Isa 41:28, Mrk 6:6, Isa 52:10, Isa 63:3–5
- 17Eph 6:17, Eph 6:14, 1Th 5:8, Rom 13:12–14, Isa 11:5, Heb 10:30, Job 29:14, Jhn 2:17
- 18Jer 17:10, Isa 63:6, Rom 2:6, Mat 16:27, Nam 1:2, Psa 62:12, Psa 21:8–9, Isa 66:15
- 19Dan 7:27, Psa 113:3, Rev 12:15–17, Zec 4:6, Psa 22:27, Rev 17:14–15, Mal 1:11, Zep 3:8–9
- 20Rom 11:26–27, Tit 2:11–14, Ezk 18:30–31, Act 3:19, Heb 12:14, Oba 1:17–21, Jol 2:32, Deu 30:1–10
- 21Jer 31:31–34, Heb 10:16, Ezk 36:25–27, Jer 32:38–41, Heb 8:6–13, 2Co 3:17–18, Isa 51:16, Isa 44:3
Topics in this chapter
40
Anthropomorphisms, Arm, Bear, Breastplate, Character, Church, Cockatrice, Conscience, Covenant, Falsehood, Fear, God, Hand, Helmet, Holy Spirit, Homicide, Isaiah, Jesus, the Christ, Judgment, Justice, Malice, Persecution, Prayer, Prophecy, Punishment, Quotations and Allusions, Repentance, Righteous, Rulers, Salvation, Seekers, Sin, Soldiers, Spider, Truth, Viper, Wicked (People), Word of God, Zeal, Religious, Zion