Mathayo 15
1 Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa Torati wakamjia Isa kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
2 “Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
3 Isa akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
4 Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
5 Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
6 basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
7 Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
8 “ ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
9 Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’ ”
10 Isa akaita umati wa watu waliokuwa hapo, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
11 kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
12 Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”
13 Akawajibu, “Kila mmea ambao Baba yangu wa mbinguni hakuupanda utang’olewa.
14 Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”
15 Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”
16 Isa akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?
17 Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?
18 Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.
19 Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.
20 Haya ndio yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
21 Isa aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.
22 Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”
23 Lakini Isa hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”
24 Isa akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”
25 Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Isa, akasema, “Bwana, nisaidie!”
26 Isa akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
27 Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwa meza za bwana zao.”
28 Ndipo Isa akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.
29 Isa akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.
30 Umati mkubwa wa watu wakamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.
31 Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.
32 Kisha Isa akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninahurumia umati huu wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga watu wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”
33 Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kulisha umati mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”
34 Isa akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
35 Isa akaagiza watu wote waketi chini.
36 Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akamshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
37 Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
38 Idadi ya watu walikuwa wanaume elfu nne, bila kuhesabu wanawake na watoto.
39 Baada ya kuaga umati wa watu, Isa aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.
Cross-references
268
- 1Luk 5:30, Act 23:9, Mat 23:2, Luk 5:21, Mrk 3:22, Mat 5:20, Luk 5:17, Mrk 7:1–23
- 2Mrk 7:2, Luk 11:38, Col 2:8, Col 2:20–23, Mrk 7:5, 1Pe 1:18
- 3Col 2:23, Tit 1:14, Mrk 7:6–8, Col 2:8, Mrk 7:13, Mat 7:3–5
- 4Exo 20:12, Exo 21:17, Lev 20:9, Deu 5:16, Deu 21:18–21, Pro 23:22, Lev 19:3, Mat 19:19
- 5Mrk 7:10–13, Act 5:29, Mat 23:16–18, Act 4:19, Amo 7:15–17, Lev 27:9–34, Pro 20:25
- 61Ti 5:8, Jer 8:8, Mrk 7:13, Psa 119:126, Hos 4:6, 1Ti 5:16, Psa 119:139, Rom 3:31
- 7Mrk 7:6, Mat 23:23–29, Act 28:25–27, Mat 7:5
- 8Isa 29:13, Ezk 33:31, Act 8:21, 1Pe 3:10, Jer 12:2, Pro 23:26, Heb 3:12, Jhn 1:47
- 9Isa 29:13, Mrk 7:7, 1Ti 1:4, Tit 1:14, Col 2:18–22, 1Ti 4:6–7, Heb 13:9, Isa 58:1–3
- 10Mrk 7:14–15, Luk 20:45–47, Col 1:9, Luk 24:45, Mat 13:19, Isa 55:3, Isa 6:9, Mat 24:15
- 11Mrk 7:15, Mat 15:18–20, Jas 3:5–8, Mat 12:34–37, 1Ti 4:4–5, Act 10:14–15, Rom 14:17, Luk 11:38–41
- 121Ki 22:13–14, 1Co 10:32–33, Mat 17:27, Gal 2:5, Jas 3:17, 2Co 6:3
- 13Jhn 15:2, Isa 60:21, Jhn 15:6, Isa 61:3, Psa 92:13, Mat 13:40–41, 1Co 3:12–15, 1Co 3:9
- 14Luk 6:39, Isa 56:10, Mat 23:16–24, Mal 2:8, Isa 9:16, Isa 42:19, Jer 5:31, 2Pe 2:1
- 15Mat 13:36, Mrk 7:17, Jhn 16:29, Mrk 4:34
- 16Mat 16:9, Mrk 7:18, Mrk 9:32, Mat 15:10, Luk 9:45, Mat 13:51, Isa 28:9–10, Luk 18:34
- 17Luk 6:45, 1Co 6:13, Mat 7:19–20, Col 2:21–22, 2Ki 10:27, Jas 3:6
- 18Pro 15:28, Mat 12:34, Jas 3:6–10, Mat 15:11, Pro 15:2, Pro 10:32, Pro 6:12, 1Sa 24:13
- 19Mrk 7:21–23, Gal 5:19–21, Jer 17:9, Tit 3:2–6, Jas 1:13–15, Pro 4:23, Gen 6:5, Rom 3:10–19
- 20Mrk 7:3–4, Eph 5:3–6, Luk 11:38–40, Mat 15:2, Rev 21:8, 1Co 3:16–17, 1Co 6:18–20, Mat 23:25–26
- 21Mrk 7:24–30, Mat 11:21–23, Jos 13:6, Jos 19:28–29, Jdg 1:31, Mat 10:5–6, Gen 49:13, Jos 11:8
- 22Mat 9:27, Mrk 7:25–26, Mat 17:15, Psa 45:12, Psa 4:1, Ezk 3:6, Luk 18:38–39, Luk 17:13
- 23Mat 14:15, Gen 42:7, Mrk 10:47–48, Lam 3:8, Psa 28:1, Deu 8:2
- 24Mat 10:5–6, Rom 15:8, Act 13:46, Jer 50:6–7, Ezk 34:5–6, Act 3:25–26, Ezk 34:16, Luk 15:4–6
- 25Gen 32:26, Mat 14:33, Mrk 9:22, Mat 20:31, Hos 12:4, Mat 8:2, Luk 18:1–8, Mrk 9:24
- 26Mrk 7:27–28, Mat 7:6, Php 3:2, Eph 2:12, Gal 2:15, Rev 22:15, Rom 9:4, Act 22:21–22
- 27Luk 16:21, Eph 3:8, 1Ti 1:13–15, Rom 10:12, Luk 15:18–19, Job 40:4–5, Luk 23:40–42, Mat 5:45
- 28Mrk 9:23–24, Mat 8:13, Psa 145:19, Mrk 5:34, Mat 9:22, Rom 4:19–20, Jhn 4:50–53, Mat 8:10
- 29Mat 4:18, Jhn 6:1, Mat 5:1, Mat 15:29–31, Jhn 21:1, Jos 12:3, Isa 9:1, Mrk 7:31–37
- 30Luk 6:17–19, Act 5:15–16, Mat 14:35–36, Act 19:11–12, Isa 35:5–6, Psa 103:3, Mrk 1:32–34, Luk 7:21–22
- 31Mat 9:8, Luk 18:43, Psa 50:23, Luk 7:16, Gen 32:28, Mat 18:8, Luk 17:15–18, Psa 50:15
- 32Mat 9:36, Luk 12:29–30, Act 27:33, Mrk 8:1–10, Mat 14:14–21, Luk 7:13, Heb 4:15, Mat 6:32–33
- 33Mrk 8:4–5, Mat 14:15, Mrk 6:37, Luk 9:13, Jhn 6:5–9, 2Ki 4:42–44, Num 11:21–22
- 34Mat 16:9–10, Jhn 21:9–10, Luk 24:41–42
- 35Jhn 6:10, Mrk 6:39–40, Luk 9:14–16, Mat 14:19–21
- 36Luk 22:19, Rom 14:6, Jhn 6:11, Act 27:35, 1Ti 4:3–4, 1Co 10:31, 1Sa 9:13, Jhn 6:23
- 37Mrk 8:19–21, Mat 14:20–21, Luk 1:53, Mat 16:9–10, Mat 15:33, Psa 107:9, Mrk 8:8–9
- 39Mrk 8:10, Mat 14:22
Topics in this chapter
58
Ablution, Adultery, Afflictions and Adversities, Apostles, Basket, Blasphemy, Blindness, Chiding, Children, Commandments, Crime, David, Demons, Depravity of Man, Doctrines, Dog (Sodomite?), Dumb (Deafness, Mute), Eating, Ecclesiasticism, Faith, False Teachers, Fish, Formalism, Frugality, Galilee, Glorifying God, God, Government, Hand, Heart, Holy Spirit, Homicide, Humility, Hypocrisy, Intercession, Jesus, the Christ, Lameness, Loaves, Magdala, Minister, Christian, Miracles, Mother, Peter, Pharisees, Prayer, Purification, Quotations and Allusions, Reprobacy, Scribe (S), Sidon, Sin, Syro-Phoenician, Teachers, Theft and Thieves, Tradition, Tyre, Wicked (People), Word of God