Ezekieli 2
1 Akaniambia, “Mwanadamu, simama kwa miguu yako nami nitasema nawe.”
2 Alipokuwa akiongea nami, Roho wa Mungu akanijia na kunisimamisha wima, nikamsikia akisema nami.
3 Akaniambia: “Mwanadamu, ninakutuma kwa Waisraeli, taifa ambalo limeniasi mimi; wao na baba zao wameniasi hadi leo.
4 Watu ninaokutuma kwao ni wakaidi na wabishi. Waambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mungu Mwenyezi.’
5 Kama watasikiliza au hawatasikiliza, kwa kuwa wao ni nyumba ya uasi, watajua nabii amekuwa miongoni mwao.
6 Nawe mwanadamu, usiwaogope wao wala maneno yao. Usiogope, ijapo michongoma na miiba vinakuzunguka na unaishi katikati ya nge. Usiogope yale wasemayo wala usitishwe nao, ijapo wao ni nyumba ya uasi.
7 Lazima uwaambie maneno yangu, ikiwa watasikiliza au hawatasikiliza, kwa kuwa wao ni waasi.
8 Lakini wewe mwanadamu, sikiliza ninalokuambia. Usiasi kama hiyo nyumba ya uasi. Fungua kinywa chako na ule nikupacho.”
9 Ndipo nikatazama, nami nikaona mkono ulionyooshwa kunielekea. Nao ulikuwa na kitabu,
10 ambacho alikikunjua mbele yangu. Pande zote mbili kilikuwa kimeandikwa maneno ya maombolezo, na vilio na ole.
Cross-references
79
- 1Dan 10:11, Ezk 3:17, Ezk 4:1, Ezk 3:1, Ezk 5:1, Ezk 3:4, Mat 16:13–16, Act 9:6
- 2Ezk 3:24, Num 11:25–26, Ezk 3:12, Rev 11:11, Ezk 36:27, 1Sa 16:13, Dan 8:18, Neh 9:30
- 3Jer 3:25, 1Sa 8:7–8, Deu 9:24, Dan 9:5–13, Neh 9:33–35, Rom 10:15, Psa 106:28, Ezk 3:4–8
- 4Ezk 3:7, Isa 48:4, Jer 5:3, Jer 6:15, Psa 95:8, Mat 10:16, 1Ki 22:14, Act 20:26–27
- 5Ezk 33:33, Ezk 3:27, Jhn 15:22, Mat 10:12–15, Ezk 2:7, Act 13:46, Luk 10:10–12, Rom 3:3
- 6Jer 1:8, Isa 51:12, 1Pe 3:14, 2Ti 1:7, Luk 10:19, Mic 7:4, Jer 1:17, Mat 10:28
- 7Jer 23:28, Ezk 2:5, Ezk 3:10, Ezk 3:17, Jer 1:7, Jer 1:17, Mat 28:20, Jer 26:2
- 8Rev 10:9, Jer 15:16, Isa 50:5, Ezk 3:1–3, Ezk 3:10, 1Pe 5:3, 1Ti 4:14–16, Num 20:10–13
- 9Ezk 8:3, Rev 10:8–11, Dan 10:10, Ezk 3:1, Rev 5:1–5, Dan 10:16–18, Dan 5:5, Jer 1:9
- 10Rev 8:13, Isa 30:8–11, Isa 3:11, Jer 36:29–32, Rev 11:14, Hab 2:2, Rev 9:12