Isaya 17
1 Neno la unabii kuhusu Dameski: “Tazama, Dameski haitakuwa tena mji bali itakuwa lundo la magofu.
2 Miji ya Aroeri itaachwa na itaachiwa mifugo ambayo italala huko, bila yeyote wa kuyaogopesha.
3 Mji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu, nao uweza wa ufalme kutoka Dameski; mabaki ya Aramu yatakuwa kama utukufu wa Waisraeli,” asema Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni.
4 “Katika siku ile utukufu wa Yakobo utafifia, unono wa mwili wake utadhoofika.
5 Itakuwa kama mvunaji akusanyavyo nafaka na kuvuna nafaka kwa mikono yake, kama wakati mtu aokotapo masazo ya masuke katika Bonde la Warefai.
6 Hata hivyo baadhi ya masazo yatabaki, kama vile mti wa mzeituni unavyopigwa, kukiachwa zeituni mbili au tatu juu ya matawi kileleni, nne au tano katika matawi yanayozaa sana,” asema Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli.
7 Katika siku ile watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa yule Aliye Mtakatifu wa Israeli.
8 Hawataziangalia tena madhabahu, kazi za mikono yao, nao hawataheshimu nguzo za Ashera, na madhabahu za kufukizia uvumba zilizofanywa kwa mikono yao.
9 Katika siku ile miji yao iliyo imara, ambayo waliihama kwa sababu ya Waisraeli, itakuwa kama mahali palipoachwa pa vichaka na magugu. Nayo yote itakuwa ukiwa.
10 Mmemsahau Mungu Mwokozi wenu, hamkumkumbuka Mwamba aliye ngome yenu. Kwa hiyo, hata ingawa mlipandikiza mimea iliyo mizuri sana na kuotesha mizabibu ya kigeni,
11 hata kama siku ile unapoipandikiza, unaifanya iote na asubuhi ile ile unayoipanda, unaifanya ichipue, hata hivyo mavuno yatakuwa kama si kitu katika siku ile ya ugonjwa na maumivu yasiyoponyeka.
12 Ole! Ghadhabu ya mataifa mengi: wanaghadhibika kama bahari iliyochafuka! Ole! Makelele ya mataifa wanaovuma: wanavuma kama ngurumo za maji mengi!
13 Ingawa mataifa yanavuma kama ngurumo za maji yanayofanya mawimbi, wakati anayakemea yanakimbia mbali, yanafukuzwa mbele ya upepo kama makapi juu ya milima, kama jani likivingirishwa na dhoruba.
14 Wakati wa jioni, hofu ya ghafula! Kabla ya asubuhi, wametoweka! Hili ndilo fungu la wale wanaotupora, fungu la wale wanaotunyang’anya mali yetu.
Cross-references
112
- 1Amo 1:3–5, Zec 9:1, Isa 25:2, Gen 14:15, Jer 49:2, Mic 1:6, Isa 7:8, Jer 49:23–27
- 2Ezk 25:5, Jer 7:33, Mic 4:4, Zep 2:6, Deu 2:36, Num 32:34, Jer 48:19, Deu 3:12
- 3Isa 7:16, Isa 8:4, Hos 9:11, Isa 7:8, Mic 1:4–9, Hos 13:7–8, Isa 17:4, Isa 28:1–4
- 4Isa 10:16, Deu 32:15–27, Isa 10:4, Isa 9:8, Isa 24:16, Isa 24:13, Zep 2:11, Isa 9:21
- 5Mat 13:30, Jol 3:13, Jer 51:33, Rev 14:15–20, 2Sa 5:18, 2Sa 5:22, Mat 13:39–42, Isa 17:11
- 6Isa 24:13, Deu 4:27, Rom 9:27, Rom 11:4–6, Jdg 8:2, Oba 1:5, Rom 11:26, Isa 10:22
- 7Mic 7:7, Hos 6:1, Hos 3:5, 2Ch 31:1, Isa 24:14–15, Isa 29:18–19, Isa 29:24, 2Ch 30:10–11
- 8Isa 30:22, Isa 27:9, Isa 2:8, Mic 5:13–14, Isa 1:29, Zep 1:3, 2Ch 34:4, Hos 14:8
- 9Isa 27:10, Amo 3:11–15, Mic 7:13, Mic 6:16, Isa 28:1–4, Isa 6:11–13, Isa 7:16–20, Isa 24:1–12
- 10Jer 2:32, Isa 26:4, Psa 106:21, Deu 32:18, Hos 13:6–7, Deu 32:4, Psa 106:13, Psa 85:4
- 11Hos 8:7, Job 4:8, Mat 8:11–12, Hos 9:16, Psa 90:6, Gal 6:7–8, Hos 9:1–4, Hos 10:12–15
- 12Psa 18:4, Luk 21:25, Jer 6:23, Ezk 43:2, Rev 17:15, Rev 17:1, Isa 5:26–30, Psa 29:3
- 13Psa 9:5, Isa 41:15–16, Psa 1:4, Job 21:18, Isa 29:5, Isa 30:30–33, Mrk 4:39–41, Psa 46:5–11
- 142Ki 19:35, Pro 22:23, Jer 2:3, Jer 13:25, Hab 2:16–17, Zep 2:9–10, Ezk 39:10, Job 20:29