Isaya 60
1 “Ondoka, angaza, kwa kuwa nuru yako imekuja na utukufu wa Mwenyezi Mungu umezuka juu yako.
2 Tazama, giza litaifunika dunia, na giza nene litayafunika mataifa, lakini Mwenyezi Mungu atazuka juu yako na utukufu wake utaonekana juu yako.
3 Mataifa watakuja kwenye nuru yako na wafalme kwa mwanga wa mapambazuko yako.
4 “Inua macho yako na utazame pande zote: Wote wanakusanyika na kukujia, wana wako wanakuja toka mbali, nao binti zako wanabebwa mikononi.
5 Ndipo utatazama na kutiwa nuru, moyo wako utasisimka na kujaa furaha, mali iliyo baharini italetwa kwako, utajiri wa mataifa utakujilia.
6 Makundi ya ngamia yatajaa katika nchi yako, ngamia vijana wa Midiani na Efa. Nao watu wote wanaotoka Sheba watakuja, wakichukua dhahabu na uvumba na kutangaza sifa za Mwenyezi Mungu.
7 Makundi yote ya Kedari yatakusanyika kwako, kondoo dume wa Nebayothi watakutumikia, watakubalika kama sadaka juu ya madhabahu yangu, nami nitalipamba Hekalu langu tukufu.
8 “Ni nani hawa warukao kama mawingu, kama hua kuelekea kwenye viota vyao?
9 Hakika visiwa vinanitazama; merikebu za Tarshishi ndizo zinazotangulia, zikiwaleta wana wenu kutoka mbali, wakiwa na fedha na dhahabu zao, kwa heshima ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwa maana amekujalia utukufu.
10 “Wageni watazijenga upya kuta zako, na wafalme wao watakutumikia. Ingawa katika hasira nilikupiga, lakini katika upendeleo wangu nitakuonesha huruma.
11 Malango yako yatakuwa wazi siku zote, kamwe hayatafungwa, mchana wala usiku, ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa: wafalme wao wakiongoza maandamano ya ushindi.
12 Kwa maana taifa au ufalme ule ambao hautakutumikia utaangamia; utaharibiwa kabisa.
13 “Utukufu wa Lebanoni utakujilia, msunobari, mvinje pamoja na mteashuri, ili kupapamba mahali pangu patakatifu, nami nitapatukuza mahali pa miguu yangu.
14 Wana wa wale waliokutesa watakuja wakisujudu mbele yako; wote wanaokudharau watasujudu miguuni pako; nao watakuita Mji wa Mwenyezi Mungu, Sayuni ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.
15 “Ingawa umeachwa na kuchukiwa, bila yeyote anayesafiri ndani yako, nitakufanya kuwa fahari ya milele, na furaha ya vizazi vyote.
16 Utanyonya maziwa ya mataifa, na kunyonyeshwa matiti ya wafalme. Ndipo utakapojua kwamba Mimi, Mwenyezi Mungu, ni Mwokozi wako, Mkombozi wako, niliye Mwenye Nguvu wa Yakobo.
17 Badala ya shaba nitakuletea dhahabu, na fedha badala ya chuma. Badala ya mti nitakuletea shaba, na chuma badala ya mawe. Nitafanya amani kuwa mtawala wako, na haki kuwa mfalme wako.
18 Jeuri hazitasikika tena katika nchi yako, wala maangamizi au uharibifu ndani ya mipaka yako, lakini utaita kuta zako Wokovu, na malango yako Sifa.
19 Jua halitakuwa tena nuru yako mchana, wala mwangaza wa mwezi hautakuangazia, kwa maana Mwenyezi Mungu atakuwa nuru yako ya milele, naye Mungu wako atakuwa utukufu wako.
20 Jua lako halitazama tena, nao mwezi wako hautafifia tena; Mwenyezi Mungu atakuwa nuru yako milele, nazo siku zako za huzuni zitakoma.
21 Ndipo watu wako wote watakuwa waadilifu, nao wataimiliki nchi milele. Wao ni chipukizi nililolipanda, kazi ya mikono yangu, ili kuonesha utukufu wangu.
22 Aliye mdogo kwenu atakuwa elfu, mdogo kuliko wote atakuwa taifa lenye nguvu. Mimi ndimi Mwenyezi Mungu; katika wakati wake nitayatimiza haya upesi.”
Cross-references
169
- 1Eph 5:14, Eph 5:8, Jhn 8:12, Isa 52:1–2, Isa 60:19–20, Isa 58:8, Jhn 12:46, Mat 5:16
- 2Col 1:13, 1Pe 2:9, Act 17:30–31, Eph 4:17–20, Hag 2:7–9, 2Co 4:4–6, Rom 1:21–32, Mal 4:2
- 3Act 13:47, Isa 49:23, Rev 21:24, Isa 2:2–5, Mic 4:1–2, Psa 117:1–2, Zec 8:20–23, Jhn 12:32
- 4Isa 42:6, Isa 49:18, Isa 49:20–22, Gal 3:28–29, Isa 43:6, Act 13:44, Isa 66:11–12, Mat 8:11
- 5Isa 61:6, Isa 23:18, Act 10:45, Psa 98:7–9, Hos 3:5, Jer 33:9, Isa 60:11, Isa 24:14–15
- 6Mat 2:11, Psa 72:10, Psa 72:15, 1Pe 2:9, Gen 25:3–4, Jdg 6:5, Rev 5:9–10, 1Pe 2:5
- 7Isa 56:7, Gen 25:13, Heb 13:15–16, Job 42:8, Rom 12:1, Rom 15:16, Hag 2:7–9, Isa 60:13
- 8Rev 7:9, Luk 13:29, Heb 12:1, Isa 60:4, Isa 49:21, Isa 45:22, Gen 8:8–11
- 9Isa 55:5, Isa 2:16, Isa 11:11, Isa 51:5, Isa 66:19–20, Gal 4:26, Isa 49:1, Isa 42:10
- 10Isa 61:5, Isa 49:23, Rev 21:26, Isa 14:1–2, Rev 21:24, Zec 6:15, Isa 60:3, Isa 57:17–18
- 11Rev 21:25–26, Isa 60:5, Isa 60:18, Isa 62:10, Psa 149:8
- 12Isa 54:15, Zec 14:12–19, Psa 2:12, Isa 41:11, Dan 2:44–45, Isa 14:2, Mat 21:44, Rev 2:26–27
- 13Isa 35:2, 1Ch 28:2, Psa 132:7, Psa 96:6, Isa 66:1, Ezr 7:27, Hos 14:6–7, Isa 41:19–20
- 14Rev 3:9, Isa 49:23, Isa 45:14, Heb 12:22, Isa 1:26, Isa 62:12, Isa 14:1–2, Rev 3:12
- 15Isa 61:7, Jer 30:17, Isa 49:14–23, Jer 33:11, Isa 35:10, Isa 54:6–14, Isa 6:12, Rev 11:15–17
- 16Isa 49:23, Isa 66:11–12, Isa 66:14, Isa 61:6, Isa 43:3–4, Ezk 34:30, Isa 59:20
- 17Heb 11:40, Isa 30:26, Zec 12:8, Isa 1:26, 1Ki 10:21–27, Isa 32:1–2, 2Pe 3:13
- 18Isa 26:1, Isa 11:9, Zec 9:8, Psa 72:3–7, Isa 2:4, Mic 4:3, Rev 19:1–6
- 19Rev 21:23, Rev 22:5, Zec 2:5, Psa 36:9, Psa 3:3, Psa 62:7, Luk 2:32, Psa 4:2
- 20Rev 21:4, Psa 84:11, Isa 35:10, Psa 27:1, Mal 4:2, Isa 30:26, Isa 25:8, Rev 7:15–17
- 21Mat 15:13, Psa 37:22, Psa 37:11, Isa 29:23, Isa 61:3, Jhn 15:2, Psa 92:13, Isa 43:7
- 22Hab 2:3, Heb 10:36, Luk 18:7, Mat 13:31–32, 2Pe 3:8, Isa 66:8, Isa 5:19, Dan 2:44
Topics in this chapter
50
Arabians, Blindness, Box Tree, Branch, Camel, Character, Church, Commerce, Dove, Turtle, Dromedary, Eclipse, Ephah, Fear, Footstool, Frankincense, Gates, Gentiles, Glorifying God, Glory, God, Gold, Gospel, Holiness, Iron, Israel, Prophecies Concerning, Jesus, the Christ, Kedar, Liberality, Light, Midianites, Milk, Money, Moon, Nation, Nebaioth, Nurse, Peace, Pine, Righteous, Rulers, Salvation, Sheba, Sheep, Ship, Sun, Tarshish, Temple, Waiting, Zeal, Religious, Zion