Isaya 25
1 Ee Mwenyezi Mungu, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu umetenda mambo ya ajabu, mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
2 Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi, mji wenye ngome kuwa magofu, ngome imara ya wageni kuwa si mji tena, wala hautajengwa tena kamwe.
3 Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, miji ya mataifa katili itakuogopa wewe.
4 Umekuwa kimbilio la watu maskini, kimbilio la mhitaji katika taabu yake, hifadhi wakati wa dhoruba na kivuli wakati wa hari. Kwa maana pumzi ya wakatili ni kama dhoruba ipigayo ukuta
5 na kama joto la jangwani. Wewe wanyamazisha kelele ya wageni; kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu, ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.
6 Juu ya mlima huu Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni ataandaa karamu ya vinono kwa mataifa yote, karamu ya mvinyo wa zamani, nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.
7 Juu ya mlima huu ataharibu sitara ihifadhiyo mataifa yote, kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,
8 yeye atameza mauti milele. Bwana Mungu Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. Mwenyezi Mungu amesema hili.
9 Katika siku ile watasema, “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; tulimtumaini, naye akatuokoa. Huyu ndiye Mwenyezi Mungu, tuliyemtumaini; sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”
10 Mkono wa Mwenyezi Mungu utatulia juu ya mlima huu, bali Moabu atakanyagwa chini kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.
11 Watakunjua mikono yao katikati yake, kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee. Mungu atashusha kiburi chao licha ya ujanja wa mikono yao.
12 Atabomoa kuta ndefu za ngome yako na kuziangusha chini, atazishusha chini ardhini, hadi mavumbini kabisa.
Cross-references
96
- 1Exo 15:2, Psa 118:28, Num 23:19, Psa 98:1, Psa 40:5, Isa 61:10, Isa 28:29, Eph 1:11
- 2Isa 13:22, Isa 17:1, Isa 25:12, Nam 3:12–15, Isa 14:23, Deu 13:16, Rev 18:2–3, Rev 18:19
- 3Psa 46:10–11, Zec 14:16, Zec 14:9, Isa 49:23–26, Ezk 39:21–22, Isa 13:11, Rev 11:15–17, Isa 66:18–20
- 4Zep 3:12, Jas 2:5, Isa 32:2, Mat 7:25–27, Job 5:15–16, Isa 33:16, Psa 107:41, Psa 12:5
- 5Psa 74:3–23, Isa 30:30–33, Ezk 38:9–39:10, Isa 10:32–34, Isa 17:12–14, Jer 51:53–57, Dan 7:23–27, Isa 14:19
- 6Mat 8:11, Psa 63:5, Jer 31:12–13, Zec 9:16–17, Rev 19:9, Luk 22:30, Heb 12:22, Isa 2:2–3
- 7Eph 4:18, Mat 27:51, Isa 60:1–3, 2Co 3:13–18, Heb 10:19–21, Act 17:30, Eph 3:5–6, Eph 5:8
- 8Rev 21:4, Rev 7:17, 1Co 15:54, Hos 13:14, 1Co 15:26, Rev 20:14, Isa 35:10, 2Ti 1:10
- 9Psa 27:14, Gen 49:18, Mic 7:7, Isa 26:8–9, Rev 19:1–7, Isa 35:2, Psa 20:5, Rev 1:7
- 10Isa 25:6, Zep 2:9, Isa 18:4, Zep 3:15–17, Amo 2:1–3, Jer 48:2, Isa 26:6, Mic 4:13
- 11Isa 2:11, Isa 16:14, Isa 5:25, Isa 14:26, Isa 16:6, Dan 4:37, Jer 51:44, Col 2:15
- 12Isa 26:5, Rev 18:21, Jer 51:64, Isa 14:23, 2Co 10:4–5, Isa 13:19–22, Jer 51:58, Heb 11:30
Topics in this chapter
36
Afflictions and Adversities, Armies, Blessing, Church, Death, Faith, Fat, Fear, Fort, Glorifying God, God, Gospel, Immortality, Isaiah, Israel, Prophecies Concerning, Jesus, the Christ, Joy, Lees, Life, Manure, Peace, Poor, Praise, Prophecy, Psalms, Quotations and Allusions, Refining, Resurrection, Righteous, Salvation, Threshing, Truth, Waiting, War, Wine, Worship