Isaya 14
1 Mwenyezi Mungu atamhurumia Yakobo, atamchagua Israeli tena, na kuwakalisha katika nchi yao wenyewe. Wageni wataungana nao na kujiunga na nyumba ya Yakobo.
2 Mataifa watawachukua na kuwaleta mahali pao wenyewe. Nayo nyumba ya Israeli itamiliki mataifa kama watumishi na wajakazi katika nchi ya Mwenyezi Mungu. Watawafanya watekaji wao kuwa mateka, na kuwatawala waliowadhulumu.
3 Katika siku Mwenyezi Mungu atakapokuondolea mateso, udhia na utumwa wa kikatili,
4 utaichukua dhihaka hii dhidi ya mfalme wa Babeli: Tazama jinsi mtesi alivyofikia mwisho! Tazama jinsi ghadhabu yake kali ilivyokoma!
5 Mwenyezi Mungu amevunja fimbo ya mwovu, fimbo ya utawala ya watawala,
6 ambayo kwa hasira waliyapiga mataifa kwa mapigo yasiyo na kikomo, nao kwa ghadhabu kali waliwatiisha mataifa kwa jeuri pasipo huruma.
7 Nchi zote ziko kwenye mapumziko na kwenye amani, wanabubujika kwa kuimba.
8 Hata misunobari na mierezi ya Lebanoni inashangilia mbele yako na kusema, “Basi kwa kuwa umeangushwa chini, hakuna mkata miti atakayekuja kutukata.”
9 Kuzimu kumetaharuki kukulaki unapokuja, kunaamsha roho za waliokufa ili kukupokea, wote waliokuwa viongozi katika ulimwengu, kunawafanya wainuke kwenye viti vyao vya kifalme: wale wote waliokuwa wafalme juu ya mataifa.
10 Wote wataitikia, watakuambia, “Wewe pia umekuwa dhaifu, kama sisi tulivyo; wewe umekuwa kama sisi.”
11 Majivuno yako yote yameshushwa hadi Kuzimu, pamoja na kelele ya vinubi vyako, mafunza yametanda chini yako, na minyoo imekufunika.
12 Tazama jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, ewe nyota ya asubuhi, mwana wa mapambazuko! Umetupwa chini duniani, wewe uliyepata kuangusha mataifa!
13 Ulisema moyoni mwako, “Nitapanda juu hadi mbinguni, nitakiinua kiti changu cha utawala juu ya nyota za Mungu; nitaketi nimetawazwa juu ya mlima wa kusanyiko, kwenye vimo vya juu sana vya Mlima Mtakatifu.
14 Nitapaa juu kupita mawingu, nitajifanya kama Yeye Aliye Juu Sana.”
15 Lakini umeshushwa chini hadi Kuzimu, hadi kwenye vina vya shimo.
16 Wale wanaokuona wanakukazia macho, wanatafakari hatima yako: “Je, huyu ndiye yule aliyetikisa dunia na kufanya falme zitetemeke,
17 yule aliyeifanya dunia kuwa jangwa, aliyeipindua miji yake, na ambaye hakuwaachia mateka wake waende nyumbani?”
18 Wafalme wote wa mataifa wamelala kwa heshima kila mmoja katika kaburi lake.
19 Lakini wewe umetupwa nje ya kaburi lako kama tawi lililokataliwa, umefunikwa na waliouawa pamoja na wale waliochomwa kwa upanga, wale wanaoshuka hadi kwenye mawe ya shimo. Kama mzoga uliokanyagwa chini ya nyayo,
20 Hutajumuika nao kwenye mazishi, kwa kuwa umeharibu nchi yako na kuwaua watu wako. Mzao wa mwovu hatatajwa tena kamwe.
21 Andaa mahali pa kuwachinjia wanawe kwa ajili ya dhambi za baba zao, wasije wakainuka ili kuirithi nchi na kuijaza dunia kwa miji yao.
22 Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni asema, “Nitainuka dhidi yao, nitalikatilia mbali jina lake kutoka Babeli pamoja na watu wake walionusurika, watoto wake na wazao wake,” asema Mwenyezi Mungu.
23 “Nitaifanya kuwa mahali pa bundi, na kuwa nchi ya matope; nitaifagia kwa ufagio wa maangamizi,” asema Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni.
24 Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni ameapa, “Hakika, kama vile nilivyopanga, ndivyo itakavyokuwa, nami kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyosimama.
25 Nitamponda Mwashuru katika nchi yangu, juu ya milima yangu nitawakanyagia chini. Nira yake itaondolewa kutoka kwa watu wangu, nao mzigo wake utaondolewa kutoka mabegani mwao.”
26 Huu ndio mpango uliokusudiwa kwa ajili ya ulimwengu wote, huu ni mkono ulionyooshwa juu ya mataifa yote.
27 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni amekusudia, ni nani awezaye kumzuia? Mkono wake umenyooshwa, ni nani awezaye kuurudisha?
28 Neno hili lilikuja mwaka ule Mfalme Ahazi alipofariki:
29 Msifurahi, enyi Wafilisti wote, kwamba fimbo iliyowapiga imevunjika; kutoka mzizi wa huyo nyoka atachipuka nyoka mwenye sumu kali, uzao wake utakuwa joka lirukalo, lenye sumu kali.
30 Maskini kuliko maskini wote watapata malisho, nao wahitaji watalala salama. Lakini mzizi wako nitauangamiza kwa njaa, nayo njaa itawaua walionusurika.
31 Piga yowe, ee lango! Bweka, ee mji! Yeyukeni, enyi Wafilisti wote! Wingu la moshi linakuja toka kaskazini, wala hakuna atakayechelewa katika safu zake.
32 Ni jibu gani litakalotolewa kwa wajumbe wa taifa hilo? “Mwenyezi Mungu ameifanya imara Sayuni, na ndani yake watu wake walioonewa watapata kimbilio.”
Cross-references
222
- 1Psa 102:13, Zec 1:17, Eph 2:12–19, Zec 8:22–23, Isa 54:7–8, Mal 1:11, Zec 2:11–12, Jer 12:15–16
- 2Isa 61:5, Isa 60:14, Jer 30:16, Isa 60:9–12, Dan 7:25–27, Rev 18:20–24, Dan 7:18, Isa 49:23
- 3Jer 30:10, Isa 32:18, Ezr 9:8–9, Jer 46:27–28, Zec 8:8, Isa 12:1, Deu 28:65–68, Isa 11:10
- 4Isa 49:26, Isa 14:6, Jer 51:34–35, Jer 27:6–7, Lam 4:1, Rev 18:16, Dan 7:19–25, Isa 13:19
- 5Psa 125:3, Isa 9:4, Isa 10:5, Jer 48:15–17, Isa 14:29
- 6Dan 7:19–21, Jas 2:13, Jer 50:31, Rev 17:16–17, Rev 18:8–10, Isa 21:1–10, Dan 4:35, Pro 21:30
- 7Psa 126:1–3, Psa 98:7–9, Psa 96:11–13, Isa 49:13, Pro 11:10, Rev 18:20, Rev 19:1–6, Jer 51:48
- 8Ezk 31:16, Isa 55:12–13, Zec 11:2
- 9Ezk 32:21–32, Jer 50:8, Pro 15:24
- 10Psa 49:6–14, Ezk 32:21, Ecc 2:16, Psa 82:6–7, Psa 49:20, Luk 16:20–23
- 11Dan 5:25–30, Mrk 9:43–48, Job 24:19–20, Dan 5:1–4, Job 21:11–15, Isa 66:24, Ezk 32:19–20, Job 17:13–14
- 12Ezk 28:13–17, Luk 10:18, Rev 12:7–10, Rev 8:10, Rev 22:16, Isa 34:4, 2Pe 1:19, 2Pe 2:4
- 13Dan 8:10–12, Ezk 28:2, Ezk 28:12–16, 2Th 2:4, Dan 5:22–23, Ezk 29:3, Isa 2:2, Psa 48:2
- 14Isa 47:8, Gen 3:5, 2Th 2:4, Isa 37:23–24
- 15Mat 11:23, Act 12:22–23, Ezk 32:23, Luk 10:15, Rev 19:20, Ezk 28:8–9, Isa 14:3–11
- 16Jer 50:23, Psa 58:10–11, Jer 51:20–23, Psa 64:9, Psa 52:7, Isa 14:4–5
- 17Jol 2:3, 2Ch 28:8–15, Isa 13:19–22, Isa 45:13, Ezr 1:2–4, Isa 64:10, Isa 58:6, Ezk 6:14
- 18Job 30:23, 2Ch 24:25, 2Ch 24:16, Isa 22:16, Ezk 32:18–32, Ecc 6:3, Ecc 12:5
- 19Jer 41:9, Jer 41:7, Jer 16:6, Isa 22:16–18, Jer 8:1–2, 2Ki 9:25, Ezk 32:23, 1Ki 21:19
- 20Job 18:19, Psa 21:10, Psa 109:13, Psa 37:28, Psa 137:8–9, Isa 1:4, Isa 13:15–19, Job 18:16
- 21Hab 2:8–12, Mat 23:35, Lev 26:39, Exo 20:5, Isa 27:6
- 22Pro 10:7, 1Ki 14:10, Jer 50:29–35, Job 18:16–19, Jer 51:56–57, Isa 13:5, Isa 43:14, Jer 50:26–27
- 23Zep 2:14, Rev 14:8, Isa 13:21–22, 1Ki 14:10, Isa 34:11–15, 2Ki 21:13, Rev 18:21–23, Rev 18:2
- 24Pro 19:21, Isa 46:10–11, Job 23:13, Jer 29:11, Act 4:28, Eph 1:9, Mat 11:25, Amo 8:7
- 25Isa 9:4, Isa 37:36–38, Nam 1:13, Isa 10:16–19, Isa 30:30–33, Isa 14:5, Isa 10:32–34, Isa 10:12
- 26Isa 23:9, Zep 3:6–8, Isa 5:25, Exo 15:12
- 27Isa 43:13, Job 23:13, 2Ch 20:6, Pro 21:30, Job 9:12, Pro 19:21, Rom 8:28, Psa 33:11
- 282Ki 16:20, Isa 13:1, 2Ch 28:27, Isa 6:1
- 292Ch 26:6, Isa 11:8, Isa 30:6, Hos 9:1, Mic 7:8, Ezk 26:2, 2Ch 28:18, Oba 1:12
- 30Isa 7:21–22, Zep 2:4–7, Ezk 25:15–17, Isa 30:23–24, Isa 65:13–14, Isa 8:21, Isa 51:19, Zec 9:5–7
- 31Jer 1:14, Isa 20:1, Jer 25:16–20, Isa 13:6, Isa 14:29, Isa 16:7, Isa 3:26, Isa 24:12
- 32Psa 102:16, Psa 87:5, Jas 2:5, Psa 87:1, Zep 3:12, Isa 25:4, Isa 4:6, Isa 44:28
Topics in this chapter
35
Afflictions and Adversities, Ambition, Assyria, Babylon, Bittern, Burial, Cedar, Children, Church, Cockatrice, Death, Faith, Famine, God, Hell, Heredity, Immortality, Isaiah, Lebanon, Lucifer, Music, Nation, Oath, Parents, Philistines, Poor, Presumption, Pride, Prophecy, Rulers, Scepter (Sceptre), Serpent, Sin, War, Wicked (People)