Zekaria 12
1 Neno la unabii: Hili ni neno la Mwenyezi Mungu kuhusu Israeli. Mwenyezi Mungu, yeye azitandaye mbingu, awekaye misingi ya dunia na aiumbaye roho ya mwanadamu ndani yake, asema:
2 “Nitaenda kufanya Yerusalemu kuwa kikombe cha kuyumbisha mataifa yote yanayoizunguka. Yuda utazingirwa kwa vita na Yerusalemu pia.
3 Katika siku hiyo, wakati mataifa yote ya dunia yatakapokusanyika dhidi yake, nitaufanya Yerusalemu kuwa jabali lisilosogezwa kwa mataifa yote. Wote watakaojaribu kulisogeza watajiumiza wenyewe.
4 Katika siku hiyo nitampiga kila farasi kwa hofu ya ghafula, naye ampandaye nitampiga kwa wazimu,” asema Mwenyezi Mungu. “Nitalielekeza jicho langu la ulinzi juu ya nyumba ya Yuda, nami nitawapofusha farasi wote wa mataifa.
5 Kisha viongozi wa Yuda watasema mioyoni mwao, ‘Watu wa Yerusalemu wana nguvu kwa sababu Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni ni Mungu wao.’
6 “Katika siku hiyo nitawafanya viongozi wa Yuda kuwa kama kigae cha moto ndani ya lundo la kuni, kama mwenge uwakao kati ya miganda. Watateketeza kulia na kushoto mataifa yote yanayowazunguka, lakini Yerusalemu utabaki salama mahali pake.
7 “Mwenyezi Mungu atayaokoa makao ya Yuda kwanza, ili heshima ya nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu isiwe kubwa kuliko ile ya Yuda.
8 Katika siku hiyo, Mwenyezi Mungu atawakinga wale wanaoishi Yerusalemu, ili aliye dhaifu kupita wote miongoni mwao awe kama Daudi, nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama Malaika wa Mwenyezi Mungu akiwatangulia.
9 Katika siku hiyo nitatoka kuangamiza mataifa yote yatakayoshambulia Yerusalemu.
10 “Nami nitamiminia nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu roho ya neema na maombi. Watanitazama mimi, yule waliyemchoma. Nao watamwombolezea kama mtu anayemwombolezea mwanawe wa pekee na kusikitika kwa uchungu kama anayemsikitikia mzaliwa wake wa kwanza wa kiume.
11 Katika siku hiyo kilio kitakuwa kikubwa Yerusalemu, kama kilio cha Hadad-Rimoni katika tambarare ya Megido.
12 Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yake, nao wake zao peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi na wake zao, ukoo wa nyumba ya Nathani na wake zao,
13 ukoo wa nyumba ya Lawi na wake zao, ukoo wa Shimei na wake zao,
14 na koo zote zilizobaki na wake zao.
Cross-references
95
- 1Isa 42:5, Jer 51:15, Isa 57:16, Psa 102:25–26, Heb 12:9, Isa 44:24, Heb 1:10–12, Isa 48:13
- 2Psa 75:8, Zec 14:14, Isa 51:22–23, Isa 51:17, Jer 49:12, Rev 18:6, Hab 2:16, Jer 8:14
- 3Mat 21:44, Zec 14:2–4, Dan 2:34–35, Luk 20:18, Zec 13:1, Zec 14:6, Ezk 38:1–23, Isa 66:14–16
- 4Deu 28:28, Zec 12:3, Act 17:30, Zec 12:6, Neh 1:6, 2Ch 6:40, 2Ki 6:18, Zec 10:5
- 5Jol 3:16, Psa 18:32, Zec 10:12, Psa 18:39, Psa 144:1, Isa 28:6, 2Co 12:9–10, Isa 41:10–16
- 6Oba 1:18, Psa 149:6–9, Zec 2:4, Dan 2:44–45, Mic 5:5–8, Isa 41:15–16, Zec 8:3–5, Isa 54:3
- 7Jer 30:18, Rom 3:27, Psa 55:12, Amo 9:11, Psa 35:26, Mat 11:25–26, Psa 38:16, Zec 11:11
- 8Mic 5:2–4, Mic 7:16, Mic 7:8, Zec 9:8, Jol 3:16–17, Zec 2:5, Jol 3:10, Exo 23:20–21
- 9Isa 54:17, Zec 14:2–3, Hag 2:22, Zec 12:2
- 10Rev 1:7, Ezk 39:29, Jol 2:28–29, Jhn 19:34–37, Jer 6:26, Rom 8:26, Act 2:33, Mat 24:30
- 112Ch 35:24, 2Ki 23:29
- 12Rev 1:7, Luk 3:31, Zec 7:3, 1Co 7:5, Jer 31:18, Mat 24:30, Exo 12:30, 2Sa 5:14
- 131Ch 3:19, 1Ch 23:10, 2Ch 29:14, 1Ch 4:27, 1Ch 23:7, Exo 6:16–26, 1Ki 1:8, Num 3:1–4
- 14Pro 9:12