1 Wakorintho 9
1 Je, mimi si huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Isa, Bwana wetu? Je, ninyi si matunda ya kazi yangu katika Bwana?
2 Hata kama mimi si mtume kwa wengine, hakika mimi ni mtume kwenu, kwa maana ninyi ni muhuri wa utume wangu katika Bwana Isa.
3 Huu ndio utetezi wangu kwa hao wanaokaa kunihukumu.
4 Je, hatuna haki ya kula na kunywa?
5 Je, hatuna haki ya kusafiri na mke anayeamini, kama wanavyofanya mitume wengine na ndugu zake Bwana Isa na Kefa?
6 Au ni mimi na Barnaba tu inatubidi kufanya kazi ili tuweze kupata mahitaji yetu?
7 Ni askari yupi aendaye vitani kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye shamba la mizabibu na asile matunda yake? Ni nani achungaye kundi na asipate maziwa yake.
8 Je, nasema mambo haya katika mtazamo wa kibinadamu tu? Je, Torati haisemi vivyo hivyo?
9 Kwa maana imeandikwa katika Torati ya Musa: “Usimfunge maksai kinywa apurapo nafaka.” Je, Mungu hapa anahusika na ng’ombe?
10 Je, Mungu hasemi haya hasa kwa ajili yetu? Hakika yameandikwa kwa ajili yetu, kwa sababu mtu anapolima na mpuraji akapura nafaka, wote wanapaswa kufanya hivyo wakiwa na tumaini la kushiriki mavuno.
11 Je, ikiwa sisi tulipanda mbegu ya kiroho miongoni mwenu, itakuwa ni jambo kubwa iwapo tutavuna vitu vya mwili kutoka kwenu?
12 Kama wengine wana haki ya kupata msaada kutoka kwenu, isingepasa tuwe na haki hiyo hata zaidi? Lakini sisi hatukutumia haki hii. Kinyume chake, tunavumilia kila kitu ili tusije tukazuia Injili ya Al-Masihi.
13 Je, hamjui kwamba, watu wafanyao kazi hekaluni hupata chakula chao kutoka hekaluni, nao wale wahudumiao madhabahuni hushiriki kile kitolewacho madhabahuni?
14 Vivyo hivyo, Bwana Isa ameamuru kwamba wale wanaohubiri Injili wapate riziki yao kutokana na Injili.
15 Lakini sijatumia hata mojawapo ya haki hizi. Nami siandiki haya nikitumaini kwamba mtanifanyia mambo hayo. Heri nife kuliko mtu yeyote kuninyima huku kujisifu kwangu.
16 Lakini ninapohubiri Injili siwezi kujisifu maana ninalazimika kuhubiri. Ole wangu nisipoihubiri Injili!
17 Nikihubiri kwa hiari, ninayo thawabu. Lakini kama si kwa hiari, basi ninachofanya ni kutekeleza tu uwakili niliowekewa.
18 Basi je, thawabu yangu ni nini? Thawabu yangu ni hii: Ya kwamba katika kuhubiri Injili niitoe bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili.
19 Ingawa mimi ni huru, wala si mtumwa wa mtu yeyote, nimejifanya mtumwa wa kila mtu, ili niweze kuwavuta wengi kadiri iwezekanavyo.
20 Kwa Wayahudi, nilikuwa kama Myahudi, ili niwapate Wayahudi. Kwa watu wale walio chini ya Torati, nilikuwa kama aliye chini ya Torati (ingawa mimi siko chini ya Torati), ili niweze kuwapata wale walio chini ya Torati.
21 Kwa watu wasio na Torati nilikuwa kama asiye na Torati (ingawa siko huru mbali na Torati ya Mungu, bali niko chini ya sheria ya Al-Masihi), ili niweze kuwapata wale wasio na sheria.
22 Kwa walio dhaifu nilikuwa dhaifu, ili niweze kuwapata walio dhaifu. Nimekuwa mtu wa hali zote kwa watu wote ili kwa njia yoyote niweze kuwaokoa baadhi yao.
23 Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, ili nipate kushiriki baraka zake.
24 Je, hamjui kwamba katika mashindano ya mbio wote wanaoshindana hukimbia, lakini ni mmoja wao tu apewaye tuzo? Kwa hiyo kimbieni katika mashindano ili mkapata tuzo.
25 Kila mmoja anayeshiriki katika mashindano hufanya mazoezi makali. Wao hufanya hivyo ili wapokee taji lisilodumu, lakini sisi tunafanya hivyo ili kupata taji linalodumu milele.
26 Kwa hiyo mimi sikimbii kama mtu akimbiaye bila lengo, sipigani kama mtu anayepiga hewa.
27 La, bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha, ili nikiisha kuwahubiria wengine, nisije nikakataliwa.
Cross-references
204
- 1Act 9:17, Act 9:3, 1Co 9:19, 1Co 3:6, 1Ti 2:7, Act 23:11, Gal 1:15–17, Tit 1:1–3
- 22Co 12:12, Jhn 6:27, 2Co 3:1–3
- 3Php 1:17, Act 22:1, 2Co 13:10, 2Ti 4:16, 2Co 13:3, 2Co 12:16–19, 1Co 14:37, Act 25:16
- 41Th 2:6, 2Th 3:8–9, Luk 10:7, 1Co 9:7–14, Mat 10:10, 1Th 2:9, Gal 6:6, 1Ti 5:17–18
- 5Jhn 1:42, Act 1:14, Mat 8:14, 1Co 7:39, 1Co 7:7, Heb 13:4, Gal 1:19, Mrk 6:3
- 62Th 3:7–9, Act 13:1–2, Act 4:36, Act 18:3, 1Th 2:9, Act 15:36–37, Act 11:22, Act 14:12
- 7Pro 27:18, Deu 20:6, 2Ti 2:3–4, 1Co 3:6–8, 1Ti 1:18, Jer 23:2–3, Act 20:28, Sng 8:12
- 8Rom 3:31, Rom 6:19, 1Co 14:34, 1Th 2:13, 1Th 4:8, Isa 8:20, 1Co 7:40
- 9Deu 25:4, 1Ti 5:18, Psa 104:27, Psa 145:15–16, Jon 4:11, Deu 5:14, Luk 12:24–28, Num 22:28–35
- 102Ti 2:6, Rom 15:4, Rom 4:23–24, 2Co 4:15, Jhn 4:35–38, 1Co 3:9, Luk 17:7–8, Mat 24:22
- 11Rom 15:27, Gal 6:6, 2Co 11:15, Mat 10:10, 2Ki 5:13, Mal 3:8–9
- 122Co 11:12, 1Co 9:15, 1Co 9:18, 1Th 2:6–9, 2Co 11:7–10, 1Co 9:2, Act 18:3, Rom 15:22
- 13Lev 6:26, Num 18:8–20, Num 5:9–10, Deu 18:1–5, 1Sa 2:28, 1Co 10:18, Deu 10:9, Lev 6:16–18
- 14Mat 10:10, 1Ti 5:17–18, Gal 6:6, 1Co 9:4, Luk 10:7
- 151Th 2:9, 2Th 3:8, 1Co 9:12, Act 18:3, Act 20:24, Act 20:34, 2Co 11:9–12, Mat 18:6
- 16Rom 1:14, Jer 20:9, Col 4:17, Luk 9:62, Act 26:16–20, Act 4:20, Amo 3:8, Act 9:15
- 17Gal 2:7, 1Co 3:8, Mat 10:41, Col 1:25, 1Ch 28:9, Isa 6:8, Ezk 3:14, 1Pe 5:2–4
- 182Co 11:7–9, 1Th 2:6, 1Co 8:9, 2Th 3:8–9, 2Co 12:13–18, 1Co 10:33, 2Co 4:5, 1Co 9:6–7
- 19Gal 5:13, Mat 18:15, Jas 5:19–20, 1Co 10:33, Mat 20:26–28, 1Ti 4:16, 2Ti 2:10, 1Co 9:20–22
- 20Act 16:3, Gal 5:18, Act 21:20–26, Act 17:2–3, Rom 3:19, Act 18:18, Rom 11:14, Gal 4:5
- 21Rom 2:12, Rom 2:14, Gal 3:2, 1Co 7:19–22, Mat 5:17–20, Gal 5:13–14, Tit 2:2–12, Eph 6:1–3
- 221Co 10:33, Rom 15:1, 1Co 9:19, Rom 11:14, Gal 6:1, 1Co 8:13, 1Co 7:16
- 232Ti 2:10, Mrk 8:35, 1Co 9:25–27, Gal 2:5, 1Jn 1:3, Heb 3:14, 2Co 2:4, 2Ti 2:6
- 24Php 3:14, Heb 12:1, 2Ti 4:7–8, Rev 3:11, Php 2:16, 1Co 9:26, Gal 5:7, Jer 12:5
- 252Ti 2:5, Rev 2:10, 1Ti 6:12, 2Ti 4:7–8, Jas 1:12, Rev 3:11, 2Pe 1:6, 1Pe 5:4
- 262Ti 2:5, 2Pe 1:10, Php 1:21, Col 1:29, Luk 13:24, 2Ti 1:12, 1Pe 5:1, Eph 6:12
- 27Rom 8:13, 1Co 9:25, Col 3:5, 2Co 13:5–6, 1Pe 2:11, 1Co 6:12–13, 2Co 6:4–5, 1Co 8:13
Topics in this chapter
44
Affections, Animals, Apostasy, Appetite, Barnabas, Boxing, Bullock, Captivity, Celibacy, Continence, Crown, Diplomacy, Evil, Expediency, Faith, Games, Gospel, Hygiene, Jesus, the Christ, Labor, Lasciviousness, Lust, Marriage, Milk, Minister, Christian, Paul, Priest, Prize, Quotations and Allusions, Race, Reciprocity, Righteous, Self-Denial, Stoicism, Tact, Temperance, Threshing, Unselfishness, Vision, War, Watchfulness, Wicked (People), Word of God, Zeal, Religious