Isaya 43
1 Lakini sasa hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
2 Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
3 Kwa kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
9 Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Mwenyezi Mungu, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
11 Mimi, naam mimi, ndimi Mwenyezi Mungu, zaidi yangu hakuna mwokozi.
12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi mwenyewe, bali si mungu mgeni kati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Mwenyezi Mungu, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
14 Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
15 Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
16 Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
19 Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
20 Wanyama pori wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
26 Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, jitetee uweze kupewa haki yako.
27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.
Cross-references
223
- 1Psa 100:3, Isa 43:7, Zec 13:9, Isa 54:4–5, Tit 2:14, Rev 5:9, Isa 45:3–4, Isa 42:6
- 2Isa 41:10, Jos 1:9, Psa 66:12, Psa 23:4, Dan 3:25–27, 2Co 12:9–10, Psa 91:15, 1Pe 4:12–13
- 3Isa 60:16, Isa 45:15, Isa 49:26, 2Ch 14:9–14, Exo 20:2, Pro 21:18, Isa 45:21, Tit 3:4–6
- 4Deu 7:6–8, 1Pe 2:9, Jer 31:3, Rev 3:9, Gen 12:2, Jhn 16:27, Hos 11:1, Jhn 17:23
- 5Deu 30:3, Isa 49:12, Luk 13:29, Ezk 39:25–29, Isa 60:1–11, Isa 44:2, Ezk 36:24–27, Act 18:9–10
- 62Co 6:17–18, Jer 3:14, Jer 3:18–19, Gal 3:26–29, Hos 1:10–11, Rom 9:7–8, Isa 18:7, Psa 107:3
- 7Eph 2:10, Isa 43:21, Eph 1:12, 1Pe 2:9, Rom 9:23, Isa 62:2–5, Isa 43:1, Psa 100:3
- 8Isa 6:9, Ezk 12:2, 2Co 4:4–6, Deu 29:2–4, Isa 42:18–20, Jer 5:21, Isa 44:18–20
- 9Isa 46:10, Isa 44:7–9, Isa 41:21–26, Jol 3:11, Isa 41:1, Isa 43:26, Psa 50:1, Isa 48:14
- 10Isa 41:4, Isa 45:6, Isa 46:8–9, Isa 43:12, Isa 40:21–22, Isa 44:6–8, Act 1:8, Php 2:7
- 11Hos 13:4, Isa 44:6, Isa 45:21–22, Isa 43:3, Act 4:12, Rev 7:10–12, Isa 12:2, Deu 6:4
- 12Isa 44:8, Deu 32:12, Psa 81:9–10, Isa 43:10, Isa 37:20, Isa 46:9–10, Isa 37:7, Isa 48:4–7
- 13Isa 14:27, Isa 46:10, Psa 90:2, Heb 13:8, Jhn 8:58, Job 9:12, 1Ti 1:17, Deu 32:39
- 14Jer 51:24, Isa 44:6, Isa 23:13, Isa 44:24–45:5, Jer 50:27–34, Psa 19:14, Ezk 27:29–36, Jer 51:34–37
- 15Isa 43:1, Isa 33:22, Isa 48:17, Jer 51:5, Isa 43:7, Isa 45:11, Rev 3:7, Isa 41:14
- 16Isa 51:10, Psa 77:19, Isa 43:2, Jer 31:35, Isa 51:15, Isa 63:11–13, Neh 9:11, Psa 106:9
- 17Exo 14:4–9, Isa 1:31, Rev 20:8–9, Psa 118:12, Psa 76:5–6, Ezk 38:8–18, Isa 14:20–22, Rev 19:17–21
- 18Isa 65:17, 2Co 3:10, 1Ch 16:12, Deu 8:2, Jer 16:14–15, Isa 46:9, Deu 7:18, Jer 23:7–8
- 19Isa 48:6, Isa 42:9, 2Co 5:17, Rev 21:5, Isa 41:18, Luk 3:4–5, Isa 35:6–10, Jer 31:22
- 20Isa 41:17, Isa 48:21, Isa 49:10, Isa 13:22, 1Pe 2:9, Rev 17:14, Jhn 4:14, Mrk 13:20
- 211Pe 2:9, Heb 13:15, 1Co 6:19–20, Psa 102:18, Luk 1:74–75, 1Co 10:31, Isa 61:3, Isa 60:21
- 22Mic 6:3, Mal 3:14, Mal 1:13, Jer 10:25, Jas 4:2–3, Psa 14:4, Job 21:14–15, Jhn 6:66–69
- 23Amo 5:25, Zec 7:5–6, Mat 11:30, Pro 15:8, Mal 1:6–8, Jer 7:22, Pro 21:27, Mal 3:8
- 24Isa 7:13, Jer 6:20, Isa 1:14, Ezk 6:9, Isa 63:10, Psa 95:10, Mal 2:13–17, Psa 50:9–13
- 25Heb 8:12, Mic 7:18–19, Heb 10:17, Jer 31:34, Isa 1:18, Isa 44:22, Psa 25:7, Psa 79:8–9
- 26Isa 1:18, Isa 43:9, Rom 8:33, Psa 141:2, Jer 2:21–35, Job 40:7–8, Rom 10:3, Isa 41:1
- 27Isa 28:7, Jer 5:31, Ezk 22:25–28, Lam 4:13–14, Ezk 16:3, Act 5:17–18, Mat 15:14, Mal 2:4–8
- 28Jer 24:9, Zec 8:13, Isa 65:15, Psa 79:4, Isa 47:6, Lam 2:2, 1Th 2:16, Deu 28:15–20
Topics in this chapter
44
Adam, Adoption, Afflictions and Adversities, Anthropomorphisms, Babylon, Backsliders, Blessing, Calamus, Church, Condescension of God, Depravity of Man, Egypt, Ethiopia, Faith, Fall of Man, Fat, Frankincense, God, Gospel, Idolatry, Isaiah, Man, Minister, Christian, Missions, Money, Ostriches, Owl, Power, Praise, Prayerlessness, Prophecy, Reasoning, Red Sea, Regeneration, Righteous, Sabeans, Seba, Sin, Testimony, War, Water, Will, Works, Worship