Kutoka 21
1 “Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli.
2 “Ukimnunua mtumwa Mwebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye ataenda zake pasipo kulipa chochote.
3 Akija peke yake, ataenda huru peke yake, lakini akija na mke, ataondoka pamoja naye.
4 Ikiwa bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake, na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
5 “Lakini mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
6 basi bwana wake atalazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango, au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
7 “Mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume wanavyoachiwa.
8 Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
9 Akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
10 Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
11 Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
12 “Yeyote anayempiga mtu na kumuua ni lazima auawe.
13 Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
15 “Yeyote anayemshambulia baba yake au mama yake ni lazima auawe.
16 “Yeyote anayemteka nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
17 “Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
18 “Watu wakigombana, naye mmoja akampiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa, bali akaugua na kulala kitandani,
19 yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia ikiwa mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda aliopoteza na awajibike hadi apone kabisa.
20 “Mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
21 lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
22 “Watu wawili wakipigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
23 Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
25 kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
26 “Mtu akimpiga mtumwa wa kiume au wa kike kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
27 Akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
28 “Fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
29 Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
30 Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
31 Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
32 Fahali akimpiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
33 “Mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ng’ombe au punda akatumbukia ndani yake,
34 mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
35 “Fahali wa mtu fulani akimuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
36 Hata hivyo, ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
Cross-references
142
- 1Deu 4:14, Deu 6:20, Exo 24:3–4, Psa 147:19, Ezk 20:11, Lev 18:5, Mal 4:4, Num 36:13
- 2Deu 15:12–15, Exo 12:44, Deu 15:18, Jer 34:8–17, Neh 5:1–5, Neh 5:8, Deu 31:10, Lev 25:39–45
- 3Deu 15:12–14
- 52Co 5:14–15, Deu 15:16–17, Isa 26:13
- 6Deu 15:17, Lev 25:40, Deu 19:17–18, 1Sa 28:2, Num 25:5–8, Exo 12:12, Lev 25:23, 1Ki 12:7
- 7Neh 5:5, Exo 21:2–3
- 8Jdg 14:3, Jdg 9:19, Gen 28:8, Deu 21:11–14, Deu 20:7, Mal 2:11–15, Exo 8:29, 1Sa 18:8
- 101Co 7:1–6
- 12Gen 9:6, Mat 26:52, Lev 24:17, Num 35:30–31, Num 35:16–24, Exo 20:13, Deu 19:11–13, 2Sa 12:13
- 13Jos 20:2–9, 1Sa 24:18, Deu 4:41–43, 1Sa 24:10, 1Sa 24:4, Deu 19:1–13, Num 35:10–34, 2Sa 16:10
- 141Ki 2:28–34, Heb 10:26, Num 35:20–21, 2Ki 11:15, 2Sa 3:27, 2Pe 2:10, Deu 17:12–13, 2Sa 20:9–10
- 15Deu 27:24, 1Ti 1:9, Deu 21:18–21, Pro 30:17, Pro 30:11
- 16Deu 24:7, 1Ti 1:10, Exo 22:4, Gen 37:28, Gen 40:15
- 17Pro 20:20, Mrk 7:10–11, Deu 27:16, Mat 15:3–6, Pro 30:11, Lev 20:9–10, Pro 30:17
- 18Exo 21:20, 2Sa 14:6, Exo 2:13, Num 35:16–24, Exo 21:22, Deu 25:11
- 192Sa 3:29, Zec 8:4
- 20Pro 29:19, Deu 19:21, Rom 13:4, Num 35:30–33, Gen 9:6, Num 35:19, Isa 58:3–4, Gen 4:15
- 21Lev 25:44–46
- 22Deu 22:18–19, Exo 21:30, Deu 16:18
- 23Deu 19:21, Num 35:31, Lev 24:19
- 24Deu 19:21, Mat 7:2, Mat 5:38–40, Lev 24:19–20, Luk 6:38, Jdg 1:6–7, Rev 16:6, Exo 21:26–27
- 26Eph 6:9, Deu 16:19, Job 31:13–15, Psa 10:18, Exo 21:20, Pro 22:22–23, Col 4:1, Psa 10:14
- 28Exo 21:32, Gen 9:5–6, Lev 20:15–16
- 29Deu 21:1–9
- 30Exo 21:22, Num 35:31–33, Exo 30:12, Pro 13:8
- 32Zec 11:12–13, Mat 26:15, Mat 27:3–9, Php 2:7, Gen 37:28, Exo 21:28–29
- 33Jer 18:22, Pro 28:10, Psa 119:85, Jer 18:20, Psa 9:15, Ecc 10:8
- 34Exo 22:6, Exo 21:29–30, Exo 22:14
Topics in this chapter
40
Abortion, Altar, Animals, Assault and Battery, Awl, Boring the Ear, Bullock, Children, Concubinage, Contracts, Creditor, Damages and Compensation, Daughter, Debtor, Divorce, Ear, Homicide, Israel, Kidnapping, Master, Money, Mother, Music, Parents, Polygamy, Property, Punishment, Quotations and Allusions, Ransom, Refuge, Restitution, Retaliation, Revelation, Sabbatic Year, Scourging, Servant, Theft and Thieves, Trespass, Wife, Women