Yoshua 12
1 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kumiliki maeneo yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni hadi Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki mwa Araba:
2 Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya miteremko ya Pisga.
4 Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa Wageshuri, na Wamaaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Musa, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Musa mtumishi wa Mwenyezi Mungu akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 Hawa ndio wafalme ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao.
8 Nchi hizi ni: nchi ya vilima, Shefela, Araba, miteremko ya milima, jangwa, na Negebu; yaani nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
9 mfalme wa Yeriko; mfalme wa Ai (karibu na Betheli);
10 mfalme wa Yerusalemu; mfalme wa Hebroni;
11 mfalme wa Yarmuthi; mfalme wa Lakishi;
12 mfalme wa Egloni; mfalme wa Gezeri;
13 mfalme wa Debiri; mfalme wa Gederi;
14 mfalme wa Horma; mfalme wa Aradi;
15 mfalme wa Libna; mfalme wa Adulamu;
16 mfalme wa Makeda; mfalme wa Betheli;
17 mfalme wa Tapua; mfalme wa Heferi;
18 mfalme wa Afeki; mfalme wa Lasharoni;
19 mfalme wa Madoni; mfalme wa Hazori;
20 mfalme wa Shimron-Meroni; mfalme wa Akshafu;
21 mfalme wa Taanaki; mfalme wa Megido;
22 mfalme wa Kedeshi; mfalme wa Yokneamu katika Karmeli;
23 mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori); mfalme wa Goimu katika Gilgali;
24 mfalme wa Tirsa;
Cross-references
119
- 1Deu 3:8–9, Jdg 11:18, Num 21:13, Jos 1:15, Num 21:24, Psa 133:3, Deu 2:24, Deu 4:48
- 2Gen 32:22, Deu 3:6–17, Neh 9:22, Deu 2:24–37, Psa 136:19–20, Jdg 11:13, Psa 135:11, Jdg 11:22
- 3Deu 3:17, Jos 11:2, Jos 13:20, Deu 4:49, Num 21:20, Jos 3:16, Jhn 6:1, Jos 15:2
- 4Deu 1:4, Deu 3:10–11, Jos 13:12, Num 21:33–35, Deu 3:1–7
- 5Deu 3:14, Jos 13:11, 1Sa 27:8, Deu 3:8–10, Deu 4:47–48, 2Sa 3:3, Jos 11:3, 2Sa 13:37
- 6Num 32:33, Num 32:29, Deu 3:11–17, Luk 22:29–42, Num 21:24–35, Jos 13:8–32
- 7Jos 11:17, Jos 11:23–12:1, Gen 36:30, Jos 9:1, Jos 13:1–19, Deu 11:23–24, Deu 2:1, Gen 36:20
- 8Jos 11:16, Jos 10:40, Jos 9:1, Deu 7:1, Exo 23:23, Exo 3:8, Gen 15:18–21, Deu 9:1
- 9Jos 8:29–35, Jos 6:2–21, Jos 8:1, Jos 8:17
- 10Jos 10:23, Jos 10:3, Jos 10:36–37
- 11Jos 10:31–32, Jos 10:3–23
- 12Jos 10:33, Jos 10:3, Jos 10:23, Jos 15:39
- 13Jos 10:38, Jos 15:36, Jos 10:3
- 14Num 21:1, Num 14:45, Num 21:3
- 15Jos 10:29–30, 1Sa 22:1
- 16Jos 10:28, Jdg 1:22, Jos 8:17, Gen 12:8, Gen 28:19
- 171Ki 4:10, Jos 15:34, Jos 19:13
- 181Sa 4:1, Isa 33:9, Jos 19:30, Jos 13:4
- 19Jos 11:1, Jos 11:10–11, Jdg 4:2
- 20Jos 11:1, Jos 19:15, Jos 19:25
- 21Jos 17:11, 2Ki 23:29–30, Jdg 5:19, 1Ki 4:12
- 22Jos 19:37, Jos 21:32, Jos 15:55, Jos 15:23, Jos 19:11, Isa 35:2, 1Sa 25:2, Jos 20:7
- 23Jos 11:2, Jos 4:19, Jos 17:11, Isa 9:1, Gen 14:1–2, Jos 5:9–10
- 24Deu 7:24, 1Ki 16:23, 2Ki 15:14
Topics in this chapter
49
Achshaph, Adullam, Ammonites, Amorites, Aphek, Arad, Arnon, Ashdoth-Pisgah, Ashtaroth, Baal-Gad, Bashan, Beth-El, Beth-Gader, Beth-Jeshimoth, Canaan, Chinnereth, Dor, Galilee, Geder, Gezer, Gilgal, Halak, Hazor, Hepher, Hittites, Hivites, Hormah, Jabbok, Jarmuth, Jebusites, Jokneam, Joshua, Kedesh, Lasharon, Lebanon, Libnah, Maachah, Madon, Makkedah, Megiddo, Og, Pisgah, Rephaim, Salcah, Salt, Shimron-Meron, Taanach, Tappuah, Tirzah