Marko 9
1 Isa akaendelea kuwaambia, “Amin, nawaambia, kuna watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
2 Baada ya siku sita, Isa akawachukua Petro, Yakobo na Yohana, akawapeleka juu ya mlima mrefu, mahali walipokuwa faraghani. Huko, Isa akageuka sura mbele yao.
3 Mavazi yake yakawa na weupe wa kuzima macho, meupe kuliko vile mtu yeyote duniani angeweza kuyang’arisha.
4 Musa na Ilya wakawatokea, wakawa wanazungumza na Isa.
5 Petro akamwambia Isa, “Mwalimu, ni vyema sisi tukae hapa. Turuhusu tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Musa na kingine cha Ilya.”
6 Petro hakujua aseme nini kwa maana yeye na wenzake walikuwa wameogopa sana.
7 Ndipo pakatokea wingu, likawafunika, nayo sauti kutoka lile wingu ikasema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Msikieni yeye.”
8 Mara walipotazama huku na huku, hawakuona tena mtu mwingine yeyote pamoja nao isipokuwa Isa.
9 Walipokuwa wakishuka kutoka mlimani, Isa akawakataza wasimwambie mtu yeyote mambo waliyoyaona, hadi Mwana wa Adamu atakapokuwa amefufuka kutoka kwa wafu.
10 Wakalihifadhi jambo hilo wao wenyewe, lakini wakawa wanajiuliza, “Huku kufufuka kwa wafu maana yake nini?”
11 Wakamuuliza, “Kwa nini walimu wa Torati husema kwamba ni lazima Ilya aje kwanza?”
12 Isa akawajibu, “Ni kweli, Ilya yuaja kwanza ili kutengeneza mambo yote. Mbona basi imeandikwa kwamba Mwana wa Adamu ni lazima ateseke sana na kudharauliwa?
13 Lakini nawaambia, Ilya amekwisha kuja, nao wakamtendea walivyopenda, kama ilivyoandikwa kumhusu.”
14 Walipowafikia wale wanafunzi wengine, wakawakuta wamezungukwa na umati mkubwa wa watu na baadhi ya walimu wa Torati wakibishana nao.
15 Mara wale watu walipomwona Isa, wakastaajabu sana, wakamkimbilia ili kumsalimu.
16 Akawauliza wanafunzi wake, “Mnabishana nao kuhusu nini?”
17 Mtu mmoja miongoni mwa umati ule wa watu akajibu, “Mwalimu, nilimleta kwako mwanangu ambaye ana pepo mchafu anayemfanya asiweze kuongea.
18 Kila mara huyo pepo mchafu ampagaapo mwanangu, humwangusha chini na kumfanya atokwe povu mdomoni na kusaga meno, kisha mwili wake hukauka. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.”
19 Isa akawaambia, “Enyi kizazi kisichoamini! Nitakuwa pamoja nanyi hadi lini? Nitawavumilia hadi lini? Mleteni mvulana kwangu.”
20 Nao wakamleta yule mvulana. Yule pepo mchafu alipomwona Isa, mara akamtia yule mvulana kifafa, akaanguka, akagaagaa chini huku akitokwa na povu kinywani.
21 Isa akamuuliza baba yake, “Mwanao amekuwa katika hali hii tangu lini?” Akamjibu, “Tangu utoto wake.
22 Mara kwa mara huyo pepo mchafu amekuwa akimwangusha kwenye moto au kwenye maji ili kumwangamiza. Lakini kama unaweza kufanya jambo lolote, tafadhali tuhurumie utusaidie.”
23 Isa akamwambia, “Ati, ‘Kama unaweza kufanya jambo lolote’? Yote yawezekana kwake yeye aaminiye.”
24 Mara baba yake yule mvulana akapaza sauti akisema, “Ninaamini. Nisaidie kutokuamini kwangu!”
25 Isa alipoona kwamba umati wa watu wanakusanyika pamoja mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akimwambia, “Wewe pepo bubu na kiziwi, nakuamuru umtoke, wala usimwingie tena!”
26 Baada ya yule pepo mchafu kupiga kelele, akamtia kifafa kwa nguvu, akamtoka. Yule mvulana alikuwa kama maiti, hivyo watu wengi wakasema, “Amekufa.”
27 Lakini Isa akamshika mkono, akamwinua, naye akasimama.
28 Baada ya Isa kuingia ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza wakiwa peke yao, “Mbona sisi hatukuweza kumtoa huyo pepo mchafu?”
29 Isa akawajibu, “Pepo aina hii haiwezi kutoka isipokuwa kwa kuomba [na kufunga].”
30 Wakaondoka huko, wakapitia Galilaya. Isa hakutaka mtu yeyote afahamu mahali walipo,
31 kwa maana alikuwa anawafundisha wanafunzi wake. Akawaambia, “Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu. Nao watamuua, lakini siku tatu baada ya kuuawa atafufuka.”
32 Lakini wao hawakuelewa kile alimaanisha, nao waliogopa kumuuliza maana yake.
33 Basi wakafika Kapernaumu na baada ya kuingia nyumbani akawauliza, “Mlikuwa mnabishana nini kule njiani?”
34 Lakini hawakumjibu, kwa sababu njiani walikuwa wakibishana kuhusu nani miongoni mwao alikuwa mkuu zaidi ya wote.
35 Akaketi chini, akawaita wote kumi na wawili, akawaambia: “Kama mtu yeyote akitaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa wa mwisho na mtumishi wa wote.”
36 Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha katikati yao. Akamkumbatia, akawaambia,
37 “Mtu yeyote amkaribishaye mmoja wa hawa watoto wadogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi. Naye anikaribishaye mimi, amkaribisha Baba yangu aliyenituma.”
38 Yohana akamwambia, “Mwalimu, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamkataza, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”
39 Isa akasema, “Msimkataze, kwa kuwa hakuna yeyote atendaye miujiza kwa Jina langu ambaye baada ya kitambo kidogo aweza kunena lolote baya dhidi yangu.
40 Kwa maana yeyote asiye kinyume chetu, yuko upande wetu.
41 Amin, nawaambia, yeyote awapaye ninyi kikombe cha maji kwa Jina langu kwa sababu ninyi ni mali ya Al-Masihi, hakika hataikosa thawabu yake.
42 “Mtu yeyote akimsababisha mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa baharini.
43 Mkono wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili lakini ukaingia Jehanamu, mahali ambako moto hauzimiki. [
44 Ni mahali ambako funza wao hawafi wala moto wao hauzimiki.]
45 Mguu wako ukikusababisha kutenda dhambi, ukate. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili lakini ukaingia Jehanamu. [
46 Ni mahali ambako funza wao hawafi wala moto wao hauzimiki.]
47 Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, ling’oe. Ni afadhali kwako kuingia katika ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa Jehanamu.
48 Ni mahali ambako funza wao hawafi, wala moto wao hauzimiki.
49 Kila mmoja atatiwa chumvi kwa moto.
50 “Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake utaifanyaje ili iweze kukolea tena? Mwe na chumvi ndani yenu, mkaishi kwa amani, kila mmoja na mwenzake.”
Cross-references
311
- 1Luk 9:27, Heb 2:9, Mrk 13:30, Mat 16:28, Jhn 8:51–52, Luk 22:18, Luk 2:26, Mat 24:30
- 2Luk 9:28–36, Mat 17:1–8, Isa 33:17, Mrk 5:37, Mrk 14:33, 2Co 13:1, Exo 24:13, Exo 34:29–35
- 3Mat 28:3, Dan 7:9, Mal 3:2–3, Psa 104:1–2, Rev 7:9, Isa 1:18, Rev 7:14, Psa 51:7
- 4Luk 9:30–31, Mat 17:3–4, Luk 24:44, Jhn 5:39, Act 3:21–24, Mat 11:13, Luk 24:27, Luk 9:19
- 5Jhn 14:21–23, Jhn 14:8–9, Mat 23:7, Php 1:23, Rev 22:3–4, Psa 84:10, Psa 62:2–3, 1Jn 3:2
- 6Mrk 16:5–8, Rev 1:17, Dan 10:15–19
- 72Pe 1:17, Mat 3:17, Luk 9:34–36, Mrk 1:11, Heb 2:1, Jhn 5:22–25, Mat 17:5–7, Exo 23:21–22
- 8Luk 24:31, Act 8:39–40, Act 10:16, Luk 9:36
- 9Mrk 5:43, Mat 17:9–13, Mat 12:40, Luk 24:46, Mat 27:63, Mrk 9:30–31, Mrk 8:29–31, Mat 16:21
- 10Act 17:18, Jhn 16:17–19, Jhn 2:19–22, Luk 24:7–8, Luk 18:33–34, Luk 24:25–27, Jhn 16:29–30, Jhn 12:33–34
- 11Mal 4:5, Mal 3:1, Mat 11:14, Mrk 9:4, Mat 17:10–11
- 12Isa 53:1–12, Isa 50:6, Isa 52:14, Luk 1:16–17, Isa 40:3–5, Isa 49:7, Luk 23:11, Zec 13:7
- 13Mat 14:3–11, Mat 17:12–13, Mat 11:14, Mrk 6:14–28, Luk 1:17, Luk 3:19–20, Act 7:52
- 14Luk 9:37–42, Mat 17:14–20, Mrk 2:6, Mrk 11:28, Luk 11:53–54, Mrk 12:14, Heb 12:3
- 15Mrk 9:2–3, Exo 34:30
- 16Luk 5:30–32, Mrk 8:11
- 17Luk 11:14, Mrk 9:25, Mrk 10:13, Luk 9:38, Mrk 7:26, Mat 12:22, Jhn 4:47, Mat 17:15
- 18Mrk 11:23, Mrk 9:28–29, Mat 17:19–20, Luk 9:39–40, Mat 17:16, Mrk 9:26, Mrk 9:20, Act 7:54
- 19Num 14:11, Psa 106:21–25, Num 14:27, Mat 17:17, Mrk 16:14, Luk 9:41, Heb 3:10–12, Luk 24:25
- 20Mrk 1:26, Luk 4:35, Luk 9:42, 1Pe 5:8, Mrk 9:18, Luk 8:29, Job 2:6–8, Jhn 8:44
- 21Act 9:33, Jhn 9:20–21, Mrk 5:25, Act 3:2, Job 14:1, Luk 8:43, Act 14:8, Jhn 9:1
- 22Mat 20:34, Mat 8:2, Mat 14:31, Mrk 1:40–42, Mat 15:22–28, Mrk 5:19, Mat 8:8–9, Mat 9:28
- 23Jhn 11:40, Heb 11:6, Mrk 11:23, Mat 17:20, Mat 21:21–22, Luk 17:6, 2Ch 20:20, Jhn 4:48–50
- 24Luk 17:5, Heb 12:2, Eph 2:8, 2Th 1:11, 2Th 1:3, Psa 126:5, Php 1:29, 2Co 2:4
- 25Act 16:18, Mrk 9:15, Mat 17:18, Luk 9:42, Isa 35:5–6, Mrk 5:7–8, Luk 8:29, Luk 11:14
- 26Mrk 9:20, Mrk 1:26, Exo 5:23, Mrk 9:18, Rev 12:12
- 27Act 3:7, Mrk 1:31, Isa 41:13, Mrk 5:41, Act 9:41, Mrk 1:41, Mrk 8:23
- 28Mat 17:19–20, Mrk 4:10, Mat 13:10, Mat 15:15, Mrk 7:17, Mat 13:36, Mrk 4:34
- 29Jas 5:15, Dan 9:3, Mat 17:20, Eph 6:18, 2Co 12:8, 2Co 11:27, Luk 11:26, 1Ki 17:20–22
- 30Luk 9:43–45, Mat 17:22–23, Mrk 6:31–32, Mat 27:22–23
- 31Mat 16:21, Mrk 9:12, Mrk 8:31, Mat 20:18–19, Luk 24:44–46, Mat 26:2, Mat 20:28, Luk 24:26
- 32Luk 18:34, Jhn 16:19, Luk 2:50, Luk 9:45, Jhn 12:16, Mrk 9:10, Mrk 16:14, Mrk 8:33
- 33Mat 18:1–5, Heb 4:13, Luk 9:46–48, Jhn 21:17, Jhn 2:25, Rev 2:23, Mrk 2:8, Mat 17:24
- 34Mrk 9:50, Php 2:3–7, Rom 12:10, Luk 9:46–48, 3Jn 1:9, 1Pe 5:3, Luk 22:24–30, Mat 20:21–24
- 35Mat 20:25–28, Luk 22:26, Mrk 10:42–45, Luk 14:10–11, Mat 23:11, Jas 4:6, Luk 18:14, Jer 45:5
- 36Mrk 10:16, Mat 18:2, Mat 19:14–15
- 37Mat 18:3–5, Luk 10:16, Mat 10:40–42, Jhn 14:21–23, Jhn 10:30, Jhn 12:44–45, Luk 9:48, Jhn 5:23
- 38Luk 9:49–50, Num 11:26–29, Luk 11:19
- 391Co 12:3, 1Co 13:1–2, Php 1:18, Mat 7:22–23, Mat 13:28–29, 1Co 9:27, Mrk 10:13–14, Act 19:13–16
- 40Mat 12:30, Luk 11:23
- 41Mat 10:42, Mat 25:40
- 42Mat 18:6, Luk 17:1–2, Mat 18:10, Act 26:11–14, 2Co 6:3, 2Th 1:6–9, Rom 14:13, Rom 16:17
- 43Mat 5:29–30, Mat 18:8–9, Mat 25:41, Mat 5:22, Heb 12:1, Mat 3:12, Gal 5:24, Col 3:5
- 45Mat 5:22, Mat 18:8, Mrk 9:43
- 47Mat 18:9, Mat 5:22, Mat 5:28–29, Php 3:7–8, Mrk 9:43, Mat 10:37–39, Job 31:1, Luk 14:26
- 48Isa 66:24, Mat 25:41, Mrk 9:43–45
- 49Lev 2:13, Ezk 43:24
- 50Col 4:6, Mat 5:13, Rom 12:18, Heb 12:14, 2Co 13:11, Php 1:27, Job 6:6, Luk 14:34–35
Parallel passages
3
- The TransfigurationMat 17:1–8, Mrk 9:2–8, Luk 9:28–36
- Healing the Epileptic BoyMat 17:14–21, Mrk 9:14–29, Luk 9:37–43
- Who Is the GreatestMat 18:1–5, Mrk 9:33–37, Luk 9:46–48
Topics in this chapter
61
Afflictions and Adversities, Ambition, Angel (A Spirit), Apostles, Backsliders, Beneficence, Bigotry, Catholicity, Children, Colors, Commandments, Deafness, Death, Demons, Doubting, Dumb (Deafness, Mute), Ecclesiasticism, Elijah, Epilepsy, Faith, Fellowship, Fire, Fuller, Hand, Hell, Holiness, Humility, Hypocrisy, Intercession, Intolerance, Religious, James, Jesus, the Christ, John, Love, Meekness, Millstone, Minister, Christian, Miracles, Moses, Mountain, Offerings, Parents, Peace, Persecution, Peter, Power, Prayer, Prophecy, Prudence, Quotations and Allusions, Rabbi, Righteous, Salt, Self-Denial, Strife, Teeth, Toleration, Unbelief, Wicked (People), Worldliness, Worm