Hosea 4
1 Sikieni neno la Mwenyezi Mungu, enyi Waisraeli, kwa sababu Mwenyezi Mungu analo shtaka dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi: “Hakuna uaminifu, hakuna upendo, hakuna kumjua Mungu katika nchi.
2 Kuna kulaani tu, uongo na uuaji, wizi na uzinzi, bila kuwa na mipaka, nao umwagaji damu mmoja baada ya mwingine.
3 Kwa sababu hii nchi huomboleza, wote wanaoishi ndani yake wanadhoofika; wanyama wa kondeni, ndege wa angani na samaki wa baharini wanakufa.
4 “Lakini mtu yeyote na asilete shtaka, mtu yeyote na asimlaumu mwenzake, kwa maana watu wako ni kama wale waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
5 Unajikwaa usiku na mchana, nao manabii hujikwaa pamoja nawe. Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
6 watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa. “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali Torati ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.
7 Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
8 Wanajilisha dhambi za watu wangu na kupendezwa na uovu wao.
9 Hata itakuwa: Kama walivyo watu, ndivyo walivyo makuhani. Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao na kuwalipa kwa matendo yao.
10 “Watakula lakini hawatashiba; watajiingiza katika ukahaba lakini hawataongezeka, kwa sababu wamemwacha Mwenyezi Mungu na kujiingiza wenyewe
11 katika ukahaba; kunywa divai ya zamani na divai mpya huondoa ufahamu
12 wa watu wangu. Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti nao hujibiwa na fimbo ya mti. Roho ya ukahaba imewapotosha, hawana uaminifu kwa Mungu wao.
13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima, chini ya mialoni, milibua na miela, ambako kuna vivuli vizuri. Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba na wake za wana wenu uzinzi.
14 “Sitawaadhibu binti zenu wakati wanapogeukia ukahaba, wala wake za wana wenu wanapofanya uzinzi, kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya na kutambikia pamoja na makahaba wa mahali pa ibada za sanamu: watu wasiokuwa na ufahamu wataangamia!
15 “Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli, Yuda naye asije akawa na hatia. “Usiende Gilgali, usipande kwenda Beth-Aveni. Wala usiape, ‘Hakika kama Mwenyezi Mungu aishivyo!’
16 Waisraeli ni wakaidi, kama ndama jike mkaidi. Ni jinsi gani basi Mwenyezi Mungu anaweza kuwachunga kama wana-kondoo katika shamba la majani?
17 Efraimu amejiunga na sanamu, achana naye!
18 Hata wakati wamemaliza vileo vyao wanaendelea na ukahaba wao, watawala wao hupenda sana njia za aibu.
19 Kisulisuli kitawafagilia mbali na dhabihu zao zitawaletea aibu.
Cross-references
150
- 1Jer 4:22, Mic 6:2, 1Co 15:34, Isa 3:13–14, Isa 34:1, Jer 25:31, Hos 12:2, Rom 1:28
- 2Hos 6:9, Jer 6:7, Mic 7:2, 1Th 2:15, Jer 5:26–27, Hos 7:1, Jer 7:6–10, Jer 5:7–9
- 3Zep 1:3, Nam 1:4, Isa 24:4–12, Jer 12:4, Ezk 38:20, Amo 5:16, Jer 4:27–28, Isa 33:9
- 4Deu 17:12, Ezk 3:26, Hos 4:17, Jer 18:18, Mat 7:3–6, Amo 5:13, Amo 6:10
- 5Jer 15:8, Hos 2:2, Gal 4:26, Zec 13:2, Ezk 16:44–45, Isa 9:13–17, Ezk 14:7–10, Jer 6:4–5
- 6Isa 5:13, Pro 19:2, Hos 6:6, 2Co 4:3–6, Hos 4:1, Mat 15:8, Pro 1:30–32, Isa 17:10
- 7Hos 13:6, Php 3:19, 1Sa 2:30, Mal 2:9, Hos 4:10, Hos 10:1, Hab 2:16, Hos 6:9
- 8Tit 1:11, Isa 56:11, Mic 3:11, 1Sa 2:29, Lev 6:26, Mal 1:10, Lev 7:6–7, Psa 24:4
- 9Jer 5:31, Mat 15:14, Isa 24:2, Jer 23:11–12, Hos 1:4, Pro 5:22, Isa 9:14–16, Psa 109:17–18
- 10Mic 6:14, Hag 1:6, Lev 26:26, Zep 1:6, Psa 125:5, Psa 36:3, Pro 13:25, Mal 2:1–3
- 11Pro 20:1, Luk 21:34, Isa 28:7, Ecc 7:7, Pro 6:32, Rom 13:11–14, Hos 4:12, Isa 5:12
- 12Jer 2:27, Hos 5:4, Hab 2:19, Num 15:39, Isa 44:18–20, Deu 31:16, Psa 73:27, Mic 2:11
- 13Jer 3:6, Ezk 6:13, Isa 1:29, Amo 7:17, Ezk 16:16, Job 31:9–10, 2Sa 12:10–12, Ezk 20:28–29
- 14Hos 4:1, Eph 4:18, 1Co 6:16, Hos 4:17, Hos 14:9, Isa 56:11, Heb 12:8, Dan 12:10
- 15Hos 9:15, Hos 12:11, Amo 4:4, Amo 5:5, Eph 5:11, Jer 5:2, Hos 10:5, Hos 10:8
- 161Sa 15:11, Jer 7:24, Jer 3:6, Jer 3:8, Hos 11:7, Isa 7:21–25, Isa 5:17, Jer 14:7
- 17Psa 81:12, Rev 22:11, Hos 11:2, Mat 15:14, Hos 4:4, Hos 13:2, Hos 12:1
- 18Pro 30:15–16, Mic 3:11, Deu 32:32–33, Hos 4:2, Deu 16:19, Psa 47:9, Hos 4:10, Amo 5:12
- 19Jer 51:1, Isa 1:29, Jer 4:11–12, Hos 13:15, Jer 2:26–27, Jer 17:13, Hos 12:1, Zec 5:9–11
Topics in this chapter
50
Adultery, Alliances, Backsliders, Beth-Aven, Blindness, Character, Church, Company, Covetousness, Crime, Dishonesty, Drunkenness, Elm, Ephraim, Example, Falsehood, Forgetting God, Gilgal, Glory, Heifer, Holy Spirit, Homicide, Idolatry, Ignorance, Impenitence, Influence, Ingratitude, Israel, Prophecies Concerning, Jotham, Judgment, Knowledge, Mercy, Minister, Christian, Mountain, Oath, Poplar, Priest, Prosperity, Proverbs, Reasoning, Self-Delusion, Sin, Sodomites, Sorcery, Theft and Thieves, Truth, Wicked (People), Wind, Wine, Women