Waebrania 13
1 Endeleeni kupendana kama ndugu.
2 Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
3 Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
5 Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
6 Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Mwenyezi Mungu ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
7 Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
8 Isa Al-Masihi ni yeye yule jana, leo na hata milele.
9 Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
10 Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
11 Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12 Vivyo hivyo, Isa naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
13 Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
14 Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
15 Basi kupitia kwa Isa, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
16 Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
17 Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa maelezo. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
18 Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
19 Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
20 Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Isa, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo,
21 awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni pake, kupitia kwa Isa Al-Masihi, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen.
22 Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
23 Nataka mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
24 Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
25 Neema iwe nanyi nyote. Amen.
Cross-references
192
- 11Jn 4:20–5:1, 1Pe 3:8, 1Pe 1:22, 1Pe 2:17, 2Pe 1:7, Heb 10:24, Rom 12:9–10, 2Jn 1:5–6
- 2Mat 25:35, Gen 18:1–19:3, 1Pe 4:9, Rom 12:13, Mat 25:43, Mat 25:40, Lev 19:34, 1Ki 17:10–16
- 3Mat 25:36, Heb 10:34, Rom 12:15, 1Co 12:26, Col 4:18, Gal 6:1–2, 1Pe 3:8, Mat 25:43
- 4Gen 2:24, Pro 5:15–23, 1Co 7:2–16, Gal 5:19, Gen 1:27–28, 1Co 6:9, Gal 5:21, Col 3:5–6
- 5Deu 31:8, Jos 1:5, Deu 31:6, 1Sa 12:22, Isa 41:17, Psa 37:25, Isa 41:10, 1Ch 28:20
- 6Psa 118:6–9, Isa 41:10, Rom 8:31, Psa 27:1–3, Psa 124:8, Heb 4:16, Psa 56:4, Psa 56:11–12
- 71Th 5:12–13, Heb 13:17, Php 3:17, Heb 6:12, 1Th 1:6, Mat 24:45, Act 14:23, 1Th 2:13
- 8Mal 3:6, Jas 1:17, Rev 1:8, Heb 1:12, Isa 44:6, Psa 90:2, Psa 102:27–28, Psa 103:17
- 9Eph 4:14, 1Ti 6:3–5, Eph 5:6, Rom 14:6, 1Jn 4:1, Act 20:30, Mat 24:4, Rom 16:17–18
- 101Co 10:20, 1Co 5:7–8, 1Co 9:13, 1Co 10:17–18, Num 7:5
- 11Lev 16:27, Exo 29:14, Num 19:3, Lev 9:11, Lev 6:30, Lev 4:5–7, Lev 4:11–12, Lev 16:14–19
- 12Heb 9:12–14, Jhn 19:17–18, Mrk 15:20–24, 1Co 6:11, Act 7:58, Eph 5:26, Heb 10:29, Jhn 19:34
- 13Heb 11:26, 1Pe 4:14–16, Act 5:41, Luk 6:22, Mat 16:24, 1Co 4:10–13, Mat 27:39–44, 2Co 12:10
- 14Php 3:20, Col 3:1–3, Heb 11:12–16, Heb 12:22, 2Pe 3:13–14, Eph 2:19, 2Co 4:17–5:8, Heb 11:9–10
- 15Psa 107:21–22, Psa 50:14, Rom 12:1, Psa 145:1–21, 1Pe 2:5, Hos 14:2, Eph 5:19–20, Isa 57:19
- 16Gal 6:10, 2Th 3:13, Rom 12:13, Heb 6:10, Heb 13:1–2, 1Ti 6:18, Eph 4:28, 2Co 9:12–13
- 171Th 5:12–13, 1Ti 5:17, Heb 13:7, 1Pe 5:5, Act 20:28, 1Pe 5:2–3, 1Co 16:16, Jer 13:17
- 181Th 5:25, 2Th 3:1, Col 4:3, 1Ti 1:5, Act 24:16, Rom 15:30, Act 23:1, 1Pe 3:16
- 19Phm 1:22, Rom 1:10–12, Rom 15:31–32
- 20Jhn 10:11, Heb 10:22, Rom 15:33, Psa 23:1, Jhn 10:14, 2Th 3:16, Ezk 37:26, Zec 9:11
- 21Php 2:13, 2Th 2:17, Php 4:13, 1Pe 5:10–11, 1Pe 2:5, Php 1:11, 2Ti 4:18, 1Th 5:23
- 222Co 6:1, 1Pe 5:12, Heb 3:1, Gal 6:11, Heb 10:19–39, 2Co 5:20, Heb 12:1–2, Heb 13:1–3
- 23Phm 1:1, 1Th 3:2, 2Ti 1:8, Rom 15:28, Rev 7:14, 1Ti 6:12, Rom 15:25, Phm 1:22
- 24Heb 13:17, Heb 13:7, Act 18:2, Phm 1:5, Rom 16:21–23, Rom 16:1–16, 2Co 1:1, 2Co 13:13
- 25Col 4:18, Rom 16:20, Tit 3:15, Eph 6:24, 2Ti 4:22, Rev 22:21, Rom 1:7, Rom 16:23
Topics in this chapter
62
Adultery, Afflictions and Adversities, Alms, Angel (A Spirit), Atonement, Benedictions, Beneficence, Blood, Boldness, Care, Character, Church, Cities, Commandments, Conscience, Contentment, Covenant, Covetousness, Death, Decision, Doctrines, Example, Faith, Fellowship, Fraternity, Gates, Heaven, Holiness, Honesty, Hospitality, Instability, Integrity, Intercession, Italy, Jesus, the Christ, Liberality, Love, Marriage, Minister, Christian, Neighbor, Obedience, Offerings, Perfection, Persecution, Perseverance, Poor, Praise, Quotations and Allusions, Reverence, Righteous, Sacrifices, Sanctification, Sanitation, Self-Denial, Shepherd, Stability, Thankfulness, Timothy, Types, Vanity, Works, Zeal, Religious