1 Wakorintho 10
1 Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari.
2 Wote wakabatizwa kuwa wa Musa ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari.
3 Wote walikula chakula kile kile cha roho,
4 na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Al-Masihi.
5 Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.
6 Basi mambo haya yalifanyika kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.
7 Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”
8 Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu elfu ishirini na tatu kwa siku moja.
9 Wala tusimjaribu Al-Masihi, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.
10 Msinung’unike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na malaika mharibifu.
11 Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia.
12 Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
13 Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kushinda ili mweze kustahimili.
14 Kwa hiyo wapendwa wangu, zikimbieni ibada za sanamu.
15 Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo.
16 Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Al-Masihi? Mkate tunaoumega, si ushirika wa mwili wa Al-Masihi?
17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja.
18 Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni?
19 Je, nina maana kwamba sadaka iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote?
20 La hasha! Lakini sadaka za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani.
21 Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana Isa na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika Chakula cha Bwana Isa na katika chakula cha mashetani pia.
22 Je, tunataka kuamsha wivu wa Mwenyezi Mungu? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye?
23 “Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga.
24 Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine.
25 Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri.
26 Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Mwenyezi Mungu.”
27 Ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri.
28 Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa sadaka kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri.
29 Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
30 Nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa ajili ya kile ambacho ninamshukuria Mungu?
31 Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
32 Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kundi la waumini la Mungu,
33 kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.
Cross-references
243
- 1Exo 14:29, Neh 9:11–12, Psa 78:13–14, Psa 105:39, Psa 106:7–11, Exo 13:21–22, Exo 14:19–22, Psa 77:16–20
- 2Heb 3:2–3, 1Co 1:13–16, Exo 14:31, Rom 6:3, Gal 3:27, Jhn 9:28–29
- 3Deu 8:3, Neh 9:15, Neh 9:20, Exo 16:35, Exo 16:4, Exo 16:15, Psa 105:40, Psa 78:23–25
- 4Exo 17:6, Jhn 7:37, Isa 48:21, Jhn 4:14, Psa 105:41, Num 20:11, Psa 78:15, Psa 78:20
- 5Heb 3:17, Jud 1:5, Num 26:64–65, Num 14:37, Num 14:28–35, Psa 106:26, Psa 78:32–34, Num 14:11–12
- 6Jud 1:7, 1Co 10:11, 2Pe 2:6, Heb 4:11, Num 11:4, Zep 3:6–7, Num 11:31–34, Psa 106:14–15
- 7Exo 32:6–8, Psa 106:19–20, 1Co 6:9, Deu 9:12, 1Co 10:14, Deu 9:16–21, 1Co 5:11, Exo 32:19
- 8Num 25:1–9, 1Co 6:18, Psa 106:29, 1Co 6:9, Rev 2:14
- 9Num 21:5–6, Psa 78:18, Heb 3:8–11, Exo 17:2, Deu 6:16, Psa 78:56, Exo 17:7, Exo 23:20–21
- 10Num 14:2, Num 16:41, Num 14:37, Php 2:14, 1Ch 21:15, 2Sa 24:16, Psa 106:25, Exo 12:23
- 11Rom 15:4, Rom 13:11, 1Jn 2:18, 1Co 9:10, Php 4:5, Rom 4:23, Heb 10:37, Heb 10:25
- 12Rom 11:20, 2Pe 3:17, Pro 16:18, 1Co 8:2, Mat 26:40–41, Mat 26:33–34, Pro 28:14, Rev 3:17–18
- 132Pe 2:9, 2Ti 4:18, 2Th 3:3, 1Pe 5:8–9, Heb 12:4, 1Th 5:24, Rom 8:28–39, 2Co 12:8–10
- 14Rev 21:8, 1Jn 5:21, 1Pe 2:11, 2Co 7:1, Rev 22:15, 2Co 6:17, Rev 2:14, 1Co 10:7
- 151Th 5:21, 1Co 8:1, 1Co 4:10, Job 34:2–3, 1Co 14:20, 1Co 6:5, 1Co 11:13
- 16Mat 26:26–28, 1Co 11:23–29, Act 2:42, Heb 3:14, 1Jn 1:7, Jhn 6:53–58, Luk 22:19–20, Act 2:46
- 17Rom 12:5, Col 3:15, 1Co 12:12, 1Co 12:27, Eph 4:12–13, Eph 4:4, Eph 4:25, Eph 4:16
- 18Lev 7:6, Lev 3:11, Gal 6:16, Php 3:3–5, Eph 2:11–12, 2Co 11:18–22, Rom 1:3, Lev 3:3–5
- 191Co 8:4, 1Co 3:7, Isa 40:17, Isa 41:29, 1Co 13:2, 1Co 1:28, Deu 32:21, 2Co 12:11
- 20Rev 9:20, Psa 106:37–39, Deu 32:16–17, 2Co 4:4, Lev 17:7, 2Ch 11:15
- 21Mat 6:24, 1Ki 18:21, 2Co 6:15–17, Isa 65:11, 1Co 10:16, Deu 32:37–38, 1Co 8:10
- 22Deu 32:21, Deu 32:16, Heb 10:31, Exo 34:14, Psa 78:58, Ezk 22:14, Jos 24:19, Deu 6:15
- 231Co 6:12, 1Co 8:9, Eph 4:29, Rom 14:19–20, 1Th 5:11, Rom 15:1–2, Rom 14:15, 1Co 14:17
- 24Rom 15:1–2, Php 2:4–5, 1Co 10:33, Php 2:21, 1Co 9:19–23, 1Co 13:5, 2Co 12:14
- 251Ti 4:4, 1Co 8:7, Tit 1:15, Rom 14:14, Rom 13:5, Act 10:15, 1Co 10:27–29
- 26Psa 24:1, Psa 50:12, Exo 19:5, Deu 10:14, Job 41:11, 1Ti 6:17, 1Co 10:28
- 271Co 10:25, Luk 10:7–8, 1Co 5:9–11, Luk 5:29–30, 2Co 1:13, Luk 19:7, Luk 15:23, 2Co 4:2
- 281Co 8:10–13, 1Co 8:7, Rom 14:15, 1Co 10:26, Jer 27:5–6, Mat 6:31–32, Psa 115:16, Exo 9:29
- 291Co 9:19, Rom 14:15–21, 1Co 8:9–13, 1Co 10:32, 2Co 8:21, 1Th 5:22
- 30Rom 14:6, 1Ti 4:3–4
- 31Col 3:17, Col 3:23, 1Pe 4:11, Deu 12:7, Deu 12:18, Zec 7:5–6, Deu 12:12, Luk 11:41
- 32Act 20:28, 1Co 10:33, Rom 14:13, 2Co 6:3, Act 24:16, 1Co 8:13, 1Co 11:22, 1Ti 3:15
- 33Gal 1:10, 1Co 10:24, 1Co 9:19–23, Rom 15:2–3, 2Co 12:19, Rom 11:14, 2Co 11:28–29
Topics in this chapter
64
Adultery, Afflictions and Adversities, Amusements and Worldly Pleasures, Backsliders, Baptism, Blood, Bread, Charitableness, Church, Commandments, Communion, Conscience, Consistency, Cup, Demons, Eucharist (the Lord's Supper), Evil, Example, Expediency, Fellowship, Gentiles, Glorifying God, God, Grace of God, Greece, Guest, Holiness, Humility, Idolatry, Jealousy, Jesus, the Christ, Judgments, Love, Lust, Manna, Manners, Meekness, Minister, Christian, Murmuring, Prayer, Presumption, Pride, Prudence, Quotations and Allusions, Reasoning, Red Sea, Righteous, Rock, Self-Denial, Selfishness, Serpent, Sincerity, Stones, Symbols and Similitudes, Table, Temptation, Toleration, Types, Unselfishness, Watchfulness, Wicked (People), Word of God, Worldliness, Zeal, Religious