Marko 1
1 Mwanzo wa Injili ya Isa Al-Masihi, Mwana wa Mungu,
2 kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
3 “sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Mwenyezi Mungu, yanyoosheni mapito yake.’ ”
4 Yahya alikuja akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
5 Watu kutoka Yudea yote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
6 Yahya alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Alikula nzige na asali ya mwitu.
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
8 Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho wa Mungu.”
9 Wakati huo Isa akaja kutoka Nasiri ya Galilaya, naye akabatizwa na Yahya katika Mto Yordani.
10 Isa alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho wa Mungu akishuka juu yake kama hua.
11 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
12 Wakati huo huo, Roho wa Mungu akamwongoza Isa hadi nyikani,
13 naye Isa akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama pori, nao malaika wakamhudumia.
14 Baada ya Yahya kutiwa gerezani, Isa alienda Galilaya, akaanza kuhubiri Injili ya Mungu,
15 akisema, “Wakati umetimia, ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Injili.”
16 Isa alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa walikuwa wavuvi.
17 Isa akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
19 Alipoenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Isa.
21 Wakaenda hadi Kapernaumu. Mara ilipofika siku ya Sabato, Isa akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
22 Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye mamlaka, wala si kama walimu wa Torati.
23 Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, naye akapaza sauti akisema,
24 “Tuna nini nawe, Isa Al-Nasiri? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
25 Lakini Isa akamkemea, akamwamuru, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu!”
26 Yule pepo mchafu akamgaragaza huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
27 Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
29 Mara walipotoka katika sinagogi, walienda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani mwa Simoni na Andrea.
30 Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Isa habari zake.
31 Hivyo Isa akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
32 Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Isa wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
33 Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
34 Isa akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
35 Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Isa akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
37 nao walipomwona, wakapaza sauti, wakasema, “Kila mtu anakutafuta!”
38 Isa akawajibu, “Twendeni mahali pengine, kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia. Maana nilikuja kwa kusudi hili.”
39 Kwa hiyo akazunguka Galilaya yote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Isa, akapiga magoti, akimwomba, “Ukitaka, unaweza kunitakasa.”
41 Isa, akiwa amejawa na huruma, akaunyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
42 Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
43 Baada ya Isa kumwonya vikali, akamruhusu aende zake mara moja;
44 akamwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajioneshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Musa kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
45 Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Isa hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi bali alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.
Cross-references
284
- 11Jn 5:11–12, Mat 3:17, Mat 4:3, Jhn 20:31, Jhn 1:14, Luk 1:2–3, Mat 14:33, Mat 17:5
- 2Mal 3:1, Luk 1:76, Mat 11:10, Mat 3:1–11, Luk 1:15–17, Luk 7:27–28, Luk 1:70, Psa 40:7
- 3Isa 40:3–5, Mat 3:3, Luk 3:4–6, Jhn 3:28–36, Jhn 1:19–34, Jhn 1:15
- 4Act 19:3–4, Act 13:24–25, Jhn 3:23, Mat 3:6, Luk 1:77, Luk 3:2–3, Mat 3:1–2, Act 10:37
- 5Act 19:18, Lev 26:40–42, Act 2:38, Mat 3:5–6, Jhn 1:28, Jhn 3:23, Pro 28:13, Mat 4:25
- 62Ki 1:8, Lev 11:22, Mat 3:4, Zec 13:4
- 7Act 13:25, Luk 3:16, Jhn 1:27, Mat 3:11, Luk 7:6–7, Jhn 3:28–31, Mat 3:14
- 8Act 1:5, 1Co 12:13, Act 19:4–6, Act 11:15–16, Act 10:45, Act 2:4, Jol 2:28, Ezk 36:25–27
- 9Mat 3:13–17, Mat 2:23, Luk 3:21–22
- 10Jhn 1:31–34, Luk 3:22, Isa 42:1, Mat 3:16, Isa 64:1
- 11Isa 42:1, Mrk 9:7, Mat 3:17, Psa 2:7, Col 1:13, 2Pe 1:17–18, Rom 1:4, Jhn 3:16
- 12Mat 4:1–11, Luk 4:1–13
- 13Heb 4:15, Heb 2:17–18, Exo 34:28, Mat 26:53, Deu 9:11, 1Ki 19:5–8, Deu 9:25, Mat 4:10–11
- 14Mat 4:23, Mat 4:12, Luk 8:1, Mat 9:35, Eph 2:17, Isa 61:1–3, Luk 4:17–19, Luk 4:43–44
- 15Mat 3:2, Mat 4:17, Act 2:36–38, Act 20:21, Eph 1:10, Mat 10:7, Gal 4:4, Luk 10:9
- 16Mat 4:18–22, Jhn 1:40–42, Jhn 6:8, Luk 6:14, Mrk 3:16, Mrk 1:16–20, Mrk 3:18, Mat 10:2
- 17Luk 5:10, Mat 4:19–20, Act 2:38–41, Ezk 47:10
- 18Luk 18:28–30, Mrk 10:28–31, Luk 5:11, Mat 19:27–30, Luk 14:33, Php 3:8
- 19Act 12:2, Act 1:13, Mrk 9:2, Mat 4:21, Mrk 5:37, Mrk 14:33, Mrk 3:17, Mrk 10:35
- 20Luk 14:26, Mrk 10:29, Mat 10:37, 2Co 5:16, Mat 4:21–22, Mat 8:21–22, 1Ki 19:20, Deu 33:9
- 21Mrk 6:2, Mrk 1:39, Mat 4:23, Act 17:2, Act 13:14–52, Act 18:4, Mat 4:13, Luk 4:31–37
- 22Mat 7:28–29, Mat 13:54, Luk 4:32, Luk 21:15, Jer 23:29, Jhn 7:46, Act 6:10, Act 9:21–22
- 23Mrk 9:25, Luk 4:33–37, Mrk 5:2, Mrk 1:34, Mrk 7:25, Mat 12:43
- 24Jas 2:19, Mat 8:29, Luk 4:34, Act 3:14, Rev 3:7, Act 2:27, Luk 8:28, Mrk 5:7
- 25Mrk 1:34, Act 16:17, Luk 4:41, Mrk 3:11–12, Mrk 9:25, Luk 4:35, Psa 50:16
- 26Mrk 9:26, Mrk 9:20, Luk 11:22, Luk 9:39, Luk 9:42
- 27Mat 15:31, Luk 9:1, Mrk 7:37, Luk 4:36, Mat 9:33, Mrk 10:24, Mrk 10:32, Mat 12:22–23
- 28Mat 9:31, Luk 4:37, Mic 5:4, Luk 4:17, Mrk 1:45, Mat 4:24
- 29Mat 8:14–15, Luk 4:38–39, Mrk 1:21, Luk 9:58, Mrk 1:23
- 301Co 9:5, Jas 5:14–15, Mrk 5:23, Jhn 11:3
- 31Act 9:41, Psa 116:12, Mrk 5:41, Psa 103:1–3, Luk 8:2–3, Mrk 15:41
- 32Mat 8:16, Luk 4:40, Mrk 3:2, Mat 4:24, Mrk 1:21
- 33Act 13:44, Mrk 1:5
- 34Luk 4:41, Mrk 3:12, Act 16:16–18, Mat 4:23, Mrk 1:25
- 35Luk 6:12, Luk 5:16, Luk 22:39–46, Eph 6:18, Psa 5:3, Jhn 6:15, Heb 5:7, Mat 14:23
- 37Jhn 12:19, Mrk 1:5, Zec 11:11, Jhn 3:26, Jhn 11:48
- 38Luk 4:43, Isa 61:1–3, Jhn 17:8, Luk 4:18–21, Jhn 16:28, Luk 2:49, Jhn 17:4, Jhn 9:4
- 39Mat 4:23, Mrk 1:21, Mrk 7:30, Luk 4:41, Luk 4:43–44
- 40Luk 5:12–14, Mat 8:2–4, Lev 13:1–14, Mat 17:14, 2Sa 3:29, Mrk 9:22–23, Deu 24:8–9, Mrk 10:17
- 41Mat 9:36, Heb 2:17, Heb 4:15, Mrk 6:34, Mrk 5:41, Luk 7:12–13, Gen 1:3, Mrk 4:39
- 42Jhn 15:3, Mat 15:28, Mrk 5:29, Mrk 1:31, Jhn 4:50–53, Psa 33:9
- 43Mat 9:30, Mrk 7:36, Luk 8:56, Mrk 3:12, Mrk 5:43
- 44Lev 14:1–32, Mat 8:4, Luk 17:14, 1Co 10:11, Rom 15:4, Luk 5:14, Mat 23:2–3
- 45Mrk 2:13, Mat 9:31, Luk 5:15–17, Jhn 6:2, Psa 77:11, Mat 28:15, Mrk 2:1–2, Mrk 3:7
Parallel passages
4
- The Baptism of JesusMat 3:13–17, Mrk 1:9–11, Luk 3:21–22
- The Temptation in the WildernessMat 4:1–11, Mrk 1:12–13, Luk 4:1–13
- Calling the First DisciplesMat 4:18–22, Mrk 1:16–20
- Cleansing a LeperMat 8:1–4, Mrk 1:40–45, Luk 5:12–16
Topics in this chapter
51
Andrew, Angel (A Spirit), Animals, Baptism, Call, Camel, Capernaum, Demons, Diligence, Disobedience to God, Faith, Fasting, Fishermen, Galilee, Gospel, Holy Spirit, Humility, Intercession, James, Jesus, the Christ, John, Jordan, Leather, Leprosy, Locust, Messenger, Minister, Christian, Miracles, Mother-in-Law, Nazareth, Obedience, Peter, Prayer, Preaching, Prophecy, Quotations and Allusions, Repentance, Salvation, Satan, Self-Denial, Shoe, Son-in-Law, Symbols and Similitudes, Synagogue, Trinity, Unbelief, Vision, Wilderness, Worship, Zeal, Religious, Zebedee