Yoshua 19
1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, kufuatana na koo zao. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
2 Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
4 Eltoladi, Bethuli, Horma,
5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na tatu pamoja na vijiji vyake.
7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii hadi Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu).
9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, kufuatana na koo zao: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea hadi kwenye bonde karibu na Yokneamu.
12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na mbili pamoja na vijiji vyake.
16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa Zabuloni, kufuatana na koo zao.
17 Kura ya nne ikaangukia kabila la Isakari, kufuatana na koo zao.
18 Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, kufuatana na koo zao.
24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, kufuatana na koo zao.
25 Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akshafu,
26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwa miji ishirini na mbili, pamoja na vijiji vyake.
31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Asheri, kufuatana na koo zao.
32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, kufuatana na koo zao:
33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mwaloni ulio Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
36 Adama, Rama, Hazori,
37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Naftali, kufuatana na koo zao.
40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, kufuatana na koo zao.
41 Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
43 Eloni, Timna, Ekroni,
44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,
45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
48 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Dani, kufuatana na koo zao.
49 Walipomaliza kuigawa nchi kulingana na sehemu zilizowaangukia, Waisraeli walimpa Yoshua mwana wa Nuni urithi kati yao,
50 kama vile Mwenyezi Mungu alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
51 Haya ndio maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za makabila ya Israeli waliyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Mwenyezi Mungu, penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.
Cross-references
154
- 1Jos 19:9, Gen 49:5–7, Jos 18:6–11
- 21Ch 4:28–30, Neh 11:26–30, Jos 15:28, Gen 21:31
- 3Jos 15:28–29
- 4Jos 15:30, Jdg 1:17
- 5Jos 15:31, 1Sa 27:6, 1Sa 30:1, 1Ch 4:31
- 6Jos 15:32
- 7Jos 15:42, Jos 15:32, 1Ch 4:32, Num 33:19–20
- 81Ch 4:33, 1Sa 30:27
- 92Co 8:14–15, Exo 16:18
- 10Jos 18:6, Jos 18:11, Deu 33:18–19, Gen 49:13
- 11Jos 12:22, 1Ki 4:12, 1Ch 6:68
- 12Jos 19:22, Psa 89:12, Jos 21:28, 1Ch 6:72, Jdg 4:6, Jdg 4:12
- 132Ki 14:25
- 15Jos 11:1, Jos 12:20, 2Ch 11:6, Rut 1:19, Jos 21:34–35, 2Sa 23:15, Jdg 1:30
- 181Sa 28:4, 2Ki 4:8, 2Ki 9:15, 1Ki 2:21, 1Ki 21:15–16, 2Ki 9:30, 1Ki 2:17, 1Ki 21:1
- 21Jos 21:29
- 22Jdg 4:6, 1Ki 4:9, 2Ki 14:11–13, Jos 19:12, Psa 89:12, 1Ch 6:77, Jos 19:38, Jos 21:16
- 24Luk 2:26–38
- 25Jos 12:20, Jos 11:1, 2Sa 2:16
- 261Ki 18:20, Isa 33:9, 1Ki 18:42, Sng 7:5, 1Ch 6:74, Isa 35:2, Jer 46:18, Jos 21:30
- 271Ki 9:13, 1Sa 5:2
- 28Jdg 1:31, Jos 11:8, Isa 23:12, Isa 23:4, Jhn 2:11, Jhn 4:46, Isa 23:2, Gen 10:19
- 29Jdg 1:31, 2Sa 5:11, Gen 38:5, Mic 1:14, Ezk 26:1–21, Isa 23:1–18
- 30Num 13:11, Jos 21:31, Jos 19:28, 1Ki 20:30, Jos 13:4, 1Sa 4:1, Jos 12:18
- 31Deu 33:24–25, Gen 49:20
- 33Jdg 4:11
- 34Deu 33:23, Jos 19:22, Jos 19:12
- 35Jos 11:2, 1Ki 8:65, Gen 10:18, Mrk 6:53, Num 34:8, Num 13:21, Jos 13:27
- 36Jos 11:1, Jos 12:19, Jos 11:20
- 37Jos 20:7, Jos 12:22
- 412Ch 11:10, Jos 15:33, Jdg 13:2, Jdg 18:2, Jdg 16:31, Jdg 13:25, 1Ch 2:53
- 42Jdg 1:35, Jos 21:24, 1Sa 14:31, Jos 10:12
- 43Gen 38:12, Jos 15:45, 1Sa 5:10, Jdg 14:1–2, Amo 1:8
- 441Ki 9:18, 1Ki 16:15, 1Ki 15:27, Jos 21:23
- 45Jos 21:24
- 46Act 9:36, 2Ch 2:16, Act 9:43, Jon 1:3, Act 10:8
- 47Jdg 1:34–35, Jdg 18:1–29
- 49Ezk 45:7–8
- 50Jos 24:30, Jdg 2:9, 1Ch 7:24
- 51Jos 14:1, Jos 18:10, Jos 18:1, Heb 4:8–9, Mat 20:23, Jhn 17:2, Gen 49:10, Mat 25:34
Topics in this chapter
139
Abez, Achshaph, Achzib, Adamah, Ain, Ajalon, Alammelech, Allon, Amad, Amam, Anaharath, Aphek, Ashan, Asher, Azem, Aznoth-Tabor, Baal, Baalah, Baalath, Baal-Hamon, Balah, Beer-Sheba, Bene-Berak, Beten, Beth-Anath, Beth-Dagon, Beth-Emek, Beth-Haggan, Beth-Lebaoth, Bethlehem, Beth-Marcaboth, Beth-Pazzez, Beth-Shemesh, Bethul, Bilhah, Bizjothjah, Cabul, Canaan, Chesil, Chesulloth, Chinnereth, Chisloth-Tabor, Dabbasheth, Daberath, Dan, Ekron, Elon, Elon-Beth-Hanan, Eltekeh, Eltolad, En-Gannim, En-Haddah, En-Hazor, Eshtaol, Ether, Ezem, Gath-Rimmon, Gibbethon, Gittah-Hepher, Hali, Hammath, Hammon, Hammoth-Dor, Hannathon, Haphraim, Hazar-Shual, Hazar-Susah, Hazor, Hebron, Heleph, Helkath, Horem, Hormah, Hosah, Hukkok, Idalah, Iron, Ir-Shemesh, Israel, Issachar, Ittah-Kazin, Jabneel, Japhia, Japho, Jehud, Jethlah, Jezreel, Jiphthah-El, Jokneam, Joppa, Joshua, Judah, Kanah, Kattath, Kedesh, Lakum, Lot, the, Maralah, Mashal, Me-Jarkon, Migdal-El, Misheal, Nahallal, Naphtali, Neah, Neiel, Nekeb, Rabbith, Rakkath, Rakkon, Ramah, Ramath, Ramoth, Rehob, Rimmon, Sarid, Shaalbim, Shahazimah, Sharuhen, Sheba, Shihon, Shihor-Libnath, Shimron, Shunem, Sidon, Simeon, Tabernacle, Tabor, Thankfulness, Thimnathah, Timnath-Serah, Tyre, Ummah, Zaanaim, Zebulun, Zer, Ziddim, Ziklag, Zorah