Isaya 55
1 “Haya! Njooni, ninyi nyote wenye kiu, njooni kwenye maji; nanyi ambao hamna fedha, njooni, nunueni na mle! Njooni, nunueni divai na maziwa bila fedha na bila gharama.
2 Kwa nini kutumia fedha kwa kitu ambacho si chakula, na kutaabikia kitu kisichoshibisha? Sikilizeni, nisikilizeni mimi na mle kilicho kizuri, nazo nafsi zenu zitafurahia utajiri wa unono.
3 Tegeni sikio mje kwangu, nisikieni mimi, ili nafsi zenu zipate kuishi. Nitafanya agano la milele nanyi, pendo la uaminifu nililomwahidi Daudi.
4 Tazama, nimemfanya kuwa shahidi wa mataifa, kiongozi na jemadari wa mataifa.
5 Hakika utaita mataifa usiyoyajua, nayo mataifa yale yasiyokujua yataharakisha kukujia, kwa sababu ya Mwenyezi Mungu, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, kwa maana amekutukuza.”
6 Mtafuteni Mwenyezi Mungu maadamu anapatikana; mwiteni maadamu yu karibu.
7 Mtu mwovu na aiache njia yake, na mtu mbaya na ayaache mawazo yake. Yeye na amrudie Mwenyezi Mungu, naye atamrehemu, arudi kwa Mungu wetu, kwa kuwa atamsamehe bure kabisa.
8 “Kwa kuwa mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu,” asema Mwenyezi Mungu.
9 “Kama vile mbingu zilivyo juu kuliko dunia, ndivyo njia zangu zilivyo juu kuliko njia zenu na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.
10 Kama vile mvua na theluji ishukavyo kutoka mbinguni, nayo hairudi tena huko bila kunywesha dunia na kuichipusha na kuistawisha, ili itoe mbegu kwa mpanzi na mkate kwa mlaji,
11 ndivyo lilivyo neno langu litokalo kinywani mwangu: Halitanirudia tupu, bali litatimiliza lile nililokusudia, na litafanikiwa katika kusudi lile nililolituma.
12 Mtatoka nje kwa furaha na kuongozwa kwa amani; milima na vilima vitapaza sauti kwa nyimbo mbele yenu, nayo miti yote ya shambani itapiga makofi.
13 Badala ya kichaka cha miiba itaota miti ya misunobari, na badala ya michongoma utaota mhadasi. Hili litakuwa jambo la kumpatia Mwenyezi Mungu jina, kwa ajili ya ishara ya milele, ambayo haitaharibiwa.”
Cross-references
102
- 1Jhn 7:37–38, Rev 21:6, Rev 22:17, Isa 44:3, Jhn 4:10–14, Isa 41:17–18, Psa 143:6, Rev 22:1
- 2Jhn 6:48–58, Jer 2:13, Psa 36:8, Psa 22:26, Rom 10:2–3, Heb 13:9, Jer 31:14, Isa 51:7
- 3Jer 32:40, Mat 11:28, Pro 4:20, Jhn 10:27, Act 13:34, Gen 17:7, Isa 61:8, Psa 78:1
- 4Isa 9:6–7, Rev 1:5, Dan 9:25, 1Ti 6:13, Rev 3:14, Ezk 34:23–24, Psa 18:43, Heb 2:10
- 5Isa 60:5, Isa 60:9, Zec 2:11, Rom 15:20, Gen 49:10, Isa 56:8, Isa 55:4, Jhn 17:1
- 6Jer 29:12–14, Psa 145:18, Isa 45:19, Psa 32:6, Psa 14:2, Isa 65:24, Mat 7:7–8, 2Co 6:1–2
- 7Pro 28:13, Jas 4:8–10, Ezk 18:21–23, Luk 15:10, Isa 44:22, Jon 3:10, Isa 43:25, Ezk 33:14–16
- 8Psa 92:5, Psa 40:5, Hos 14:9, Ezk 18:29, Psa 25:10, Dan 4:37, Isa 53:6, Pro 21:8
- 9Rom 11:31–36, Psa 103:11, Mat 11:25, Psa 77:19, Psa 36:5, Psa 89:2
- 102Co 9:9–11, Deu 32:2, Isa 30:23, Ezk 34:26, Hos 10:12, Isa 61:11, Psa 65:9–13, 1Sa 23:4
- 11Mat 24:35, Isa 46:10, Rom 10:17, Jhn 6:63, Isa 45:23, Luk 8:11–16, 1Co 1:18, 1Th 2:13
- 12Gal 5:22, Rom 15:13, Isa 44:23, Psa 105:43, Psa 96:11–13, Psa 98:7–9, Rev 19:1–6, Isa 49:13
- 13Eph 3:20–21, 1Pe 2:9–10, Isa 41:19, 2Co 5:17, Jer 33:9, Isa 61:3, Isa 60:13, Jer 50:5
Topics in this chapter
33
Blessing, Bread, Brier, Call, Church, Covenant, Desire, Diligence, Gentiles, Gifts From God, God, Gospel, Hunger, Jesus, the Christ, Joy, Milk, Money, Myrtle, Peace, Prayer, Prophecy, Quotations and Allusions, Regeneration, Repentance, Righteousness, Salvation, Seekers, Sin, Thirst, Water, Wicked (People), Wine, Word of God