1 Petro 3
1 Kadhalika enyi wake, watiini waume zenu, ili kama kunao wasioamini lile neno, wapate kuvutwa na mwenendo wa wake zao pasipo neno,
2 kwa kuuona utakatifu na uchaji wa Mungu katika maisha yenu.
3 Kujipamba kwenu kusiwe kwa nje tu, kama vile kusuka nywele, kuvalia vitu vilivyofanyizwa kwa dhahabu na kwa mavazi.
4 Badala yake, kujipamba kwenu kuwe katika utu wenu wa moyoni, yaani uzuri usioharibika wa roho ya upole na utulivu, ambayo ni ya thamani sana machoni pa Mungu.
5 Kwa kuwa hivi ndivyo walivyokuwa wakijipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu. Wao walikuwa ni watiifu kwa waume zao,
6 kama Sara alivyomtii mumewe Ibrahimu, hata akamwita bwana. Ninyi ni watoto wa Sara mkitenda yaliyo mema, bila kuogopa jambo lolote.
7 Vivyo hivyo ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa kuwajali, nanyi wapeni heshima mkitambua ya kuwa wao ni wenzi walio dhaifu, na kama warithi pamoja nanyi wa kipawa cha neema cha uzima, ili kusiwepo na chochote cha kuzuia maombi yenu.
8 Hatimaye, ninyi nyote kuweni na nia moja, wenye kuhurumiana, mkipendana kama ndugu, mkijaliana, na wanyenyekevu.
9 Msilipe ovu kwa ovu, au jeuri kwa jeuri, bali barikini, kwa maana hili ndilo mliloitiwa ili mpate kurithi baraka.
10 Kwa maana, “Yeyote apendaye uzima na kuona siku njema, basi auzuie ulimi wake usinene mabaya, na midomo yake isiseme hila.
11 Mtu huyo lazima aache uovu, akatende mema; lazima aitafute amani na kuifuatilia sana.
12 Kwa maana macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza maombi yao. Bali uso wa Mwenyezi Mungu uko kinyume na watendao maovu.”
13 Basi, ni nani atakayewadhuru mkiwa wenye juhudi katika kutenda mema?
14 Lakini hata ikiwalazimu kuteseka kwa ajili ya haki, mmebarikiwa. “Msiogope vitisho vyao, wala msiwe na wasiwasi.”
15 Bali mtukuzeni Al-Masihi kama Bwana mioyoni mwenu. Siku zote mwe tayari kumjibu mtu yeyote atakayewauliza kuhusu sababu ya tumaini lililo ndani yenu. Lakini fanyeni hivyo kwa upole na kwa heshima,
16 mkizitunza dhamiri zenu ziwe safi, ili wale wasemao mabaya dhidi ya mwenendo wenu mzuri katika Al-Masihi waaibike kwa ajili ya masingizio yao.
17 Kwa maana ni afadhali kupata mateso kwa ajili ya kutenda mema, ikiwa ni mapenzi ya Mungu, kuliko kuteseka kwa kutenda maovu.
18 Kwa kuwa Al-Masihi naye aliteswa mara moja tu kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili ya wasio haki, ili awalete ninyi kwa Mungu. Mwili wake ukauawa, lakini akafanywa hai katika Roho wa Mungu.
19 Baada ya kufanywa hai, alienda na kuzihubiria roho zilizokuwa kifungoni:
20 roho ambazo zamani hazikutii, wakati ule uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja katika siku za Nuhu, wakati wa kujenga safina, ambamo watu wachache tu, yaani watu wanane, waliokolewa ili wasiangamie kwa gharika.
21 Nayo maji hayo ni kielelezo cha ubatizo ambao sasa unawaokoa ninyi pia: si kwa kuondoa uchafu kwenye mwili, bali kama ahadi ya dhamiri safi kwa Mungu. Inatuokoa kupitia kwa ufufuo wa Isa Al-Masihi.
22 Yeye ameingia mbinguni na amekaa mkono wa kuume wa Mungu; nao malaika, mamlaka na nguvu zote zimetiishwa chini yake.
Cross-references
176
- 1Col 3:18, Eph 5:33, Eph 5:22–24, Tit 2:3–6, 1Co 11:3, 1Co 7:16, Gen 3:16, 1Pe 3:7
- 21Pe 2:12, 1Pe 1:15, Php 1:27, 2Pe 3:11, Eph 5:33, Php 3:20, Eph 6:5, Col 3:22
- 31Ti 2:9–10, Rom 12:2, Isa 3:18–24, Tit 2:3–15, Isa 61:10, Jer 4:30, Ezk 16:7–13, Jer 2:32
- 4Col 3:12, 1Sa 16:7, Rom 2:29, Mat 11:29, Tit 3:2, Mat 23:26, Rom 7:22, 2Co 4:16
- 51Ti 5:5, Tit 2:3–4, Act 9:36, Luk 2:37, Pro 31:30, 1Ti 5:10, 1Ti 2:15, Luk 8:2–3
- 6Gen 18:12, Rom 9:7–9, Isa 57:11, Dan 3:16–18, Act 4:19, Mat 26:69–75, 1Pe 3:14–15, Gen 18:15
- 7Col 3:19, Gen 2:23–24, Mat 19:3–9, Eph 5:25–28, Eph 5:33, 1Co 7:3, Mal 2:14–16, Mat 18:19
- 8Rom 12:10, Eph 4:31–5:2, 1Pe 1:22, Php 4:8–9, Jas 3:17, Eph 4:2, Zec 7:9, Col 3:12
- 9Rom 12:17, Pro 20:22, Rom 12:14, Rom 12:19–21, 1Th 5:15, Luk 6:27–29, Mat 5:44, Pro 17:13
- 10Psa 34:12–16, Jas 1:26, 1Pe 2:22, 1Pe 2:1, Rev 14:5, Jhn 1:47, Jas 3:1–10, Jhn 12:25
- 11Mat 5:9, Psa 34:14, Heb 12:14, Col 3:15, Rom 14:19, Rom 14:17, Jas 4:17, 3Jn 1:11
- 12Psa 34:15–16, Jhn 9:31, Pro 15:29, Pro 15:3, 2Ch 7:15, Jas 5:16, Pro 15:8, 2Ch 16:9
- 13Pro 16:7, Rom 8:28, 1Th 5:15, 3Jn 1:11, Psa 38:20, 1Co 14:1, Eph 5:1, Pro 15:9
- 14Mat 10:28, 1Pe 2:19–20, Mat 5:10–12, Isa 41:10–14, Isa 8:12–13, 2Co 12:10, 1Pe 4:13–16, Jas 1:12
- 15Col 4:6, 2Ti 2:25–26, Luk 21:14–15, 1Pe 3:2, Mat 10:18–20, Psa 119:46, Heb 6:1, Tit 1:2
- 161Pe 2:12, 1Pe 2:15, Heb 13:18, Tit 2:8, Mat 5:11, 1Pe 2:19, Act 24:16, 1Ti 1:5
- 171Pe 3:14, 1Pe 4:19, Mat 26:39, 1Pe 2:20, 1Pe 2:15, Act 21:14, Mat 26:42, 1Pe 4:15
- 18Heb 9:28, Heb 9:26, 2Co 5:21, 1Pe 4:6, Tit 2:14, Rom 5:6–8, 1Jn 1:9, Col 1:21–22
- 191Pe 4:6, Isa 61:1, Isa 42:7, Isa 49:9, Neh 9:30, Rev 20:7, 1Pe 1:11–12, Rev 19:10
- 20Heb 11:7, 2Pe 2:5, Gen 6:3, Gen 6:5, Gen 8:18, Gen 6:13–7:7, Rom 2:4–5, Gen 7:13
- 21Mrk 16:16, Ezk 36:25–26, Act 22:16, Gal 3:27, Act 2:38, Eph 5:26, Rom 10:9–10, 1Pe 1:3
- 22Heb 9:24, Heb 12:2, Heb 10:12, Eph 1:20–21, Mrk 16:19, Rom 8:34, Heb 6:20, Rom 8:38
Topics in this chapter
64
Angel (A Spirit), Antediluvians, Anthropomorphisms, Ark, Atonement, Baptism, Charitableness, Commandments, Conscience, Deceit, Dress, Example, Eye, Faith, Falsehood, Family, Fear, Fellowship, Flood, Forgiveness, Fraternity, God, Hair, Happiness, Heart, Holiness, Holy Spirit, Hope, Husband, Influence, Integrity, Jesus, the Christ, Kindness, Longevity, Love, Malice, Manners, Meekness, Noah, Peace, Persecution, Power, Quickening, Quotations and Allusions, Railing, Reasoning, Retaliation, Revenge, Reward, Righteous, Righteousness, Sarah, Sin, Slander, Speaking, Suffering, Sympathy, Testimony, Trinity, Types, Unity, Wicked (People), Wife, Women