Zaburi 50
1 Mwenye Nguvu, Mungu, Mwenyezi Mungu, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9 Sina haja na fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu mdomoni mwako?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupilia mbali maneno yangu.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19 Unakitumia kinywa chako kunena maovu, na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20 Unamsengenya ndugu yako bila kukoma, na kumsingizia mwana wa mama yako.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukadhani Mimi ni kama wewe kabisa. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwa na yeyote wa kuwaokoa:
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwoneshe wokovu wa Mungu.”
Cross-references
171
- 1Psa 113:3, Mat 25:32, Jos 22:22, Amo 3:8, Jer 32:18–19, 1Ch 16:37, Neh 9:6, Isa 1:2
- 2Psa 48:2, Rev 21:23, Psa 80:1, Rev 1:16, Deu 33:2, Hab 3:3–4, Isa 12:6, Psa 94:1
- 3Num 16:35, Dan 7:10, Lev 10:2, Mat 3:12, Mal 4:1, Psa 97:3–5, 1Ki 19:11–12, Rev 22:20
- 4Isa 1:2, Deu 32:1, Deu 31:28, Deu 30:19, Deu 4:26, Mic 6:1–2, Isa 11:3–4, Jhn 5:22–23
- 5Heb 13:20, Exo 24:3–8, Mat 26:28, Heb 12:24, Deu 33:2–3, Heb 9:10–23, Psa 97:10, Mat 24:31
- 6Psa 97:6, Psa 89:5, Psa 75:7, Rev 19:2, Rom 14:9–12, Psa 9:16, 2Co 5:10, Psa 7:3–5
- 7Psa 81:8, Exo 20:2, Jer 2:9, Psa 81:10–12, Exo 19:5–6, Isa 1:18, Zec 13:9, Mal 3:5
- 8Hos 6:6, Heb 10:4–10, Isa 1:11–31, Psa 40:6–8, Psa 51:16, Jer 7:21–23
- 9Mic 6:6–8, Heb 10:4–6, Act 17:25, Isa 43:23–24, Psa 69:31
- 10Jer 27:5–6, Psa 104:14, Psa 8:6–8, Psa 104:24–25, Dan 2:38, 1Ch 29:14–16, Jon 4:11, Gen 1:24–25
- 11Mat 6:26, Gen 1:20–22, Job 39:26–30, Luk 12:24, Psa 104:12, Job 39:13–18, Ezk 14:15–16, Psa 147:9
- 12Exo 19:5, Deu 10:14, Psa 24:1–2, 1Co 10:26–28, Job 41:11, Psa 115:15–16, Gen 1:28–30, Gen 8:17
- 14Heb 13:15, Psa 56:12, Deu 23:21, Psa 107:21–22, Psa 116:12–14, 1Pe 2:5, Psa 76:11, Hos 14:2
- 15Psa 107:28, Psa 91:15, Psa 34:3–4, Psa 107:19, Zec 13:9, Jas 5:13, Psa 81:7, Psa 107:6–13
- 16Isa 29:13, Psa 25:14, Psa 78:36–38, Rom 2:17–24, Isa 55:6–7, Isa 48:1–2, Heb 8:9, Jhn 4:24
- 17Neh 9:26, Pro 12:1, 2Ti 4:3–4, Pro 1:28–29, 1Ki 14:9, 2Th 2:10–12, Pro 1:7, Jer 8:9
- 18Rom 1:32, 1Ti 5:22, Heb 13:4, Pro 1:10–19, Mat 23:30, Pro 2:16–19, Mic 7:3, Job 31:9–11
- 19Psa 10:7, Rev 21:8, Psa 52:2–4, Jer 9:5, Rom 3:13–14, Isa 59:3–4, Psa 55:21, Jas 3:5–9
- 20Mat 10:21, Lev 19:16, Pro 10:18, Mat 5:11, Rev 12:10, Psa 31:18, Luk 22:65, Tit 2:3
- 21Rom 2:4–5, Pro 29:1, Isa 57:11, Psa 94:7–11, Ecc 12:14, Psa 90:8, Ecc 8:11–12, Isa 42:14
- 22Job 8:13, Psa 9:17, Hos 4:6, Psa 7:2, Hos 13:8, Psa 10:4, Jer 2:32, Deu 32:18
- 23Psa 91:16, Jas 3:13, Psa 24:4–5, Rom 12:1, Psa 86:12, Psa 50:14–15, Psa 25:14, Isa 12:2
Topics in this chapter
38
Afflictions and Adversities, Animals, Blasphemy, Church, Company, Complicity, Decision, Dishonesty, Falsehood, Fellowship, Forgetting God, Formalism, Glorifying God, God, Godlessness, Gossip, Heaven, Hypocrisy, Impenitence, Infidelity, Instruction, Judgment, Judgments, Offerings, Praise, Prayer, Psalms, Punishment, Quotations and Allusions, Righteous, Security, Slander, Speaking, Thankfulness, Theft and Thieves, Vows, Wicked (People), Word of God