Luka 15
1 Basi watoza ushuru na wenye dhambi wote walikuwa wanakusanyika ili wapate kumsikiliza Isa.
2 Lakini Mafarisayo na walimu wa Torati wakanung’unika wakisema, “Huyu mtu anawakaribisha wenye dhambi na kula nao.”
3 Ndipo Isa akawaambia mfano huu:
4 “Ikiwa mmoja wenu ana kondoo mia moja, naye akapoteza mmoja wao, je, hawaachi wale tisini na tisa nyikani na kwenda kumtafuta huyo aliyepotea hadi ampate?
5 Naye akishampata, humbeba mabegani mwake kwa furaha
6 na kwenda nyumbani. Kisha huwaita rafiki zake na majirani, na kuwaambia, ‘Furahini pamoja nami; nimempata kondoo wangu aliyepotea.’
7 Nawaambieni, vivyo hivyo kutakuwa na furaha zaidi mbinguni kwa sababu ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa wenye haki tisini na tisa ambao hawana haja ya kutubu.
8 “Au ikiwa mwanamke ana sarafu za fedha kumi, naye akapoteza moja, je, hawashi taa na kufagia nyumba na kuitafuta kwa bidii hadi aipate?
9 Baada ya kuipata, yeye huwaita rafiki zake na majirani na kuwaambia, ‘Furahini pamoja nami; nimeipata ile sarafu yangu ya fedha iliyopotea.’
10 Vivyo hivyo, nawaambia, kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu juu ya mwenye dhambi mmoja atubuye.”
11 Isa akaendelea kusema: “Kulikuwa na mtu mmoja aliyekuwa na wana wawili.
12 Yule mdogo akamwambia baba yake, ‘Baba, nipe urithi wangu.’ Hivyo akawagawia wanawe mali yake.
13 “Baada ya muda mfupi, yule mdogo akakusanya vitu vyote alivyokuwa navyo, akaenda nchi ya mbali, na huko akaitapanya mali yake kwa maisha ya anasa.
14 Baada ya kutumia kila kitu alichokuwa nacho, kukawa na njaa kali katika nchi ile yote, naye akawa hana chochote.
15 Kwa hiyo akaenda akaajiriwa na raia mmoja wa nchi ile ambaye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.
16 Akatamani kujishibisha kwa maganda waliyokula wale nguruwe, wala hakuna mtu aliyempa chochote.
17 “Lakini alipozingatia moyoni mwake, akasema, ‘Ni watumishi wangapi walioajiriwa na baba yangu ambao wana chakula cha kuwatosha na kusaza, bali mimi hapa nakufa kwa njaa!
18 Nitaondoka na kurudi kwa baba yangu na kumwambia: Baba, nimetenda dhambi mbele za Mungu na mbele yako.
19 Sistahili tena kuitwa mwanao; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.’
20 Basi akaondoka, akaenda kwa baba yake. “Lakini alipokuwa bado yuko mbali, baba yake akamwona, moyo wake ukajawa na huruma. Akamkimbilia mwanawe, akamkumbatia na kumbusu.
21 “Yule mwana akamwambia baba yake, ‘Baba, nimekosa mbele za Mungu na mbele yako. Sistahili kuitwa mwanao tena.’
22 “Lakini baba yake akawaambia watumishi, ‘Leteni upesi joho lililo bora sana, tieni pete kidoleni mwake na viatu miguuni mwake.
23 Leteni ndama aliyenona, mkamchinje ili tuwe na karamu, tule na kufurahi.
24 Kwa maana huyu mwanangu alikuwa amekufa na sasa yu hai tena; alikuwa amepotea na sasa amepatikana!’ Nao wakaanza kusherehekea.
25 “Wakati huo, yule mwana mkubwa alikuwa shambani. Alipokaribia nyumbani, akasikia sauti ya nyimbo na watu wakicheza.
26 Akamwita mmoja wa watumishi na kumuuliza maana ya mambo yale.
27 Akamwambia, ‘Ndugu yako amekuja, naye baba yako amemchinjia ndama aliyenona kwa sababu mwanawe amerudi nyumbani akiwa salama na mzima.’
28 “Yule mwana mkubwa akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi baba yake akatoka nje na kumsihi.
29 Lakini yeye akamjibu baba yake, ‘Tazama! Miaka yote hii nimekutumikia na hata siku moja sijaacha kutii amri zako, lakini hujanipa hata mwana-mbuzi ili nifurahi na rafiki zangu.
30 Lakini huyu mwanao ambaye ametapanya mali yako kwa makahaba aliporudi nyumbani, wewe umemchinjia ndama aliyenona!’
31 “Baba yake akamjibu, ‘Mwanangu, umekuwa nami siku zote na vyote nilivyo navyo ni vyako.
32 Lakini ilitubidi tufurahi na kushangilia kwa sababu huyu ndugu yako alikuwa amekufa na sasa yu hai; alikuwa amepotea naye amepatikana.’ ”
Cross-references
204
- 11Ti 1:15, Mat 9:10–13, Luk 5:29–32, Mat 21:28–31, Ezk 18:27, Rom 5:20, Luk 7:29, Luk 13:30
- 2Mat 9:11, Luk 7:39, Luk 19:7, Luk 5:30, Act 11:3, Gal 2:12, Luk 7:34, Luk 15:29–30
- 4Ezk 34:16, Ezk 34:11–12, Mat 18:12–14, Luk 19:10, 1Pe 2:25, Psa 119:176, Ezk 34:31, Jer 50:6
- 5Heb 12:2, Mic 7:18, Isa 46:3–4, Isa 40:10–11, Luk 19:9, Isa 63:9, Isa 53:10–11, Mic 5:4
- 6Luk 15:10, Luk 15:24, Psa 119:176, 1Pe 2:25, Jhn 3:29, Act 11:23, Jhn 15:14, Luk 15:7
- 7Luk 15:10, Luk 5:32, Luk 15:32, Mat 18:13, Pro 30:12, Luk 18:9–11, Php 3:6–7, Luk 16:15
- 8Luk 19:10, Ezk 34:12, Jhn 10:16, Jhn 11:52, Eph 2:17
- 9Luk 15:6–7
- 10Luk 15:7, Ezk 33:11, 2Co 7:10, Ezk 18:23, Luk 13:5, Mat 18:14, Ezk 18:32, Act 11:18
- 12Deu 21:16–17, Mrk 12:44, Psa 17:14, Luk 15:30
- 13Pro 21:17, Pro 29:3, Jer 2:5, Pro 23:19–22, Luk 15:30, Luk 16:19, Luk 16:1, Ecc 11:9–10
- 142Ch 33:11, Ezk 16:27, Amo 8:9–12, Hos 2:9–14
- 15Tit 3:3, 2Ti 2:25–26, Isa 1:5, Isa 57:17, Jer 31:18–19, Eph 2:2–3, Nam 3:6, Jer 5:3
- 16Rom 6:19–21, Hos 12:1, Isa 55:2, Jon 2:2–8, Psa 142:4, Lam 4:5, Psa 73:22, Isa 57:3
- 17Ezk 18:28, Eph 2:4–5, Luk 15:18–19, Eph 5:14, Act 16:29–30, Act 26:11–19, Tit 3:4–6, Jer 31:19
- 18Lam 3:40, 1Jn 1:8–10, Luk 15:21, Jer 50:4–5, Psa 51:3–5, Luk 18:13, Mat 6:14, Psa 32:3–5
- 19Job 42:6, Psa 84:10, 1Pe 5:6, Jas 4:8–10, Luk 5:8, Jos 9:24–25, Gen 32:10, 1Co 15:9
- 20Psa 103:10–13, Psa 86:5, Psa 86:15, Eph 2:13, Isa 49:15, Gen 46:29, Deu 30:2–4, Job 33:27–28
- 21Psa 51:4, Luk 15:18–19, Jer 3:13, 1Co 8:12, Rom 2:4, Psa 143:2, Ezk 16:63
- 22Est 8:2, Gen 41:42, Rev 6:11, Isa 61:10, Est 3:10, Rev 19:8, Zec 3:3–5, Rev 7:9
- 23Mat 22:2–14, Isa 25:6, Psa 63:5, Isa 65:13–14, Gen 18:7, Pro 9:2
- 24Eph 2:5, Ezk 34:16, Luk 19:10, Col 2:13, Luk 15:4, Eph 2:1, Luk 15:32, Rom 6:11
- 25Psa 150:4, Jer 31:4, 2Sa 6:14, Psa 149:3, Luk 15:11–12, Psa 126:1, Ecc 3:4, Exo 15:20
- 27Phm 1:16, Act 9:17, Luk 15:30, Act 22:13
- 281Sa 18:8, Luk 15:2, Jon 4:9, Gen 4:5–7, Isa 65:5, Jon 4:1–4, Luk 13:34, Luk 7:39
- 29Luk 18:11–12, Luk 15:7, Zec 7:3, Mal 3:14, Rev 2:17, Php 3:4–6, Luk 18:9, Isa 65:5
- 30Pro 29:3, Luk 15:12–13, Luk 15:32, Luk 18:11, Exo 32:11, Exo 32:7, Luk 15:22–23
- 31Mrk 7:27–28, Rom 9:4, Rom 11:1, Mat 20:13–16, Luk 19:22–23, Rom 11:35
- 32Eph 2:1–10, Luk 15:24, Isa 35:10, Rom 3:4, Psa 51:8, Jon 4:10–11, Rom 15:9–13, Hos 14:9
Topics in this chapter
29
Afflictions and Adversities, Angel (A Spirit), Bigotry, Dancing, Employee, Fatted Calf, Feasts, God, Heaven, Husk, Inheritance, Jealousy, Jesus, the Christ, Joy, Kiss, Lost Sheep, Penitent, Pharisees, Praise, Prodigal Son, Readings, Select, Repentance, Salvation, Self-Righteousness, Servant, Sheep, Sin, Swine, Young Men