Yoshua 13
1 Yoshua alipokuwa mzee, umri wake ukiwa umesogea sana, Mwenyezi Mungu akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado imesalia sehemu kubwa sana ya nchi ambayo haijatwaliwa.
2 “Nchi iliyosalia ni hii: “maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
3 kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani, maeneo yale matano ya watawala wa Wafilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni; nchi ya Waavi
4 kuanzia kusini; nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
5 eneo la Wagebali; na Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
6 “Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza, niwaondoe kwa ajili ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
7 sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
8 Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Musa aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Mwenyezi Mungu alivyowagawia.
9 Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba hadi Diboni,
10 nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
11 Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
12 yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Musa alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
13 Lakini Waisraeli hawakuwafukuza Wageshuri na Wamaaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli hadi leo.
14 Lakini kwa kabila la Lawi, Musa hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, ndizo zilikuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
15 Haya ndio maeneo ambayo Musa alikuwa amewapa kabila la Reubeni kufuatana na koo zao:
16 Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
17 hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
18 Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
19 Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
20 Beth-Peori, miteremko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
21 miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Musa alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
22 Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mwaguzi.
23 Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa Wareubeni kufuatana na koo zao.
24 Haya ndio maeneo ambayo Musa alikuwa amewapa kabila la Gadi, kufuatana na koo zao:
25 Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
26 na kuanzia Heshboni hadi Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
27 na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
28 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi kufuatana na koo zao.
29 Haya ndio maeneo ambayo Musa alikuwa amewapa nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, kufuatana na koo zao:
30 Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
31 nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani).
32 Huu ndio urithi Musa alipeana alipokuwa katika tambarare za Moabu, ng’ambo ya Yordani, mashariki mwa Yeriko.
33 Lakini kwa kabila la Walawi, Musa hakuwapa urithi; Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
Cross-references
153
- 1Jos 14:10, Deu 31:3, Jos 24:29, Gen 18:11, Jos 23:1–2, Luk 1:7, 1Ki 1:1
- 2Jos 13:11, 1Sa 27:8, Jdg 3:1, Jol 3:4, 2Sa 13:37–38, 2Sa 15:8, Gen 26:1, Jos 13:13
- 3Jdg 3:3, Jer 2:18, Deu 2:23, 1Sa 6:16–17, Zep 2:4–5, Gen 10:6, Jos 13:13, Num 34:2–14
- 4Jos 19:30, 1Sa 4:1, Jdg 1:34–36, Amo 2:10, Jos 12:7–8, Jos 10:40, Jos 11:3, Jos 12:18
- 5Jos 12:7, 1Ki 5:18, Psa 83:7, Ezk 27:9, Jos 11:17, Num 34:8, Deu 3:25, Isa 10:9
- 6Jos 11:8, Num 33:54, Jos 23:13, Jdg 2:21–23, Jos 14:1–2, Exo 23:30–31, Jos 23:4, Gen 15:18–21
- 7Num 26:53–56, Num 32:2–14, Ezk 47:13–23, Ezk 48:23–29, Num 33:54
- 8Jos 12:6, Jos 4:12, Num 32:33–42, Deu 3:12–17, Jos 22:4
- 9Num 21:30, Jos 13:16, Deu 3:16, Jer 48:18, Jos 12:2, Deu 3:12, Isa 15:2, Jer 48:22
- 10Num 21:24–26
- 111Ch 2:23, Jos 12:2–5, Deu 4:47–48
- 12Jos 12:4, Deu 3:10–11, Num 21:23–35, Jos 14:3–4
- 13Jos 23:12–13, Num 33:55, Jos 13:11, 2Sa 13:37–38, Jdg 2:1–3, 2Sa 3:3
- 14Num 18:20–24, Jos 14:3–4, Deu 18:1–2, Deu 10:9, Deu 12:12, Deu 12:19
- 16Jos 13:9, Jos 12:2, Jer 48:21–24, Isa 16:7–9, Deu 3:12, Isa 15:1–2, Num 32:33–38, Isa 15:4
- 17Num 32:38, Num 22:41, Num 21:19
- 18Num 21:23, Jos 21:36–37, 1Ch 6:78–79
- 19Num 32:37–38
- 20Jos 12:3, Deu 4:46, Deu 3:17, Num 33:49, Ezk 25:9, Num 25:3
- 21Num 31:8, Deu 3:10, Deu 2:30–36, Num 21:24–35
- 22Num 31:8, Rev 2:14, 2Pe 2:15, Jud 1:11, Num 24:1, Num 22:5–7, Rev 19:20
- 24Num 32:34–36
- 25Deu 3:11, 2Sa 11:1, 2Sa 12:26, Num 32:35, Num 21:26–30, Num 21:32, Ezk 21:20, Deu 2:19
- 262Sa 17:27, 2Sa 2:8, 1Ki 22:3, Jdg 10:17, 2Sa 9:4–5, Jos 21:38, Gen 32:1–2, Jos 20:8
- 27Num 34:11, Num 32:36, Gen 33:17, Jos 11:2, Deu 3:17, Jdg 8:5–6, Jos 12:3, Jdg 8:14–16
- 30Jos 13:26, Deu 3:13–15, 1Ch 2:21–23, Num 32:39–41
- 31Jos 12:4, Num 32:39–40
- 33Jos 18:7, Jos 13:14, Deu 18:1–2, Deu 10:9, Num 18:20
Topics in this chapter
72
Ammonites, Amorites, Aroer, Ashdod, Ashdoth-Pisgah, Ashkelon, Ashtaroth, Avites, Baal-Gad, Baal-Meon, Balaam, Bamoth, Bashan, Beth-Aram, Beth-Baal-Meon, Beth-Haran, Beth-Jeshimoth, Beth-Nimrah, Beth-Peor, Betonim, Chinnereth, Dibon, Duke, Edrei, Egypt, Ekron, Evi, Gad, Galilee, Gath, Gaza, Gazathites, Gebal, Geshur, Hamath, Hur, Israel, Jaazer, Jahaz, Jair, Jazer, Joshua, Kedemoth, Kirjathaim, Levites, Lord, Machir, Mahanaim, Medeba, Mephaath, Minister, Christian, Misrephoth-Maim, Moab, Moon, Og, Philistines, Priest, Rabbah, Ramath-Mizpeh, Reba, Rekem, Rephaim, Reubenites, Salcah, Sibmah, Sidon, Sihor, Succoth, Topography, Zaphon, Zareth-Shahar, Zur