1 Wakorintho 6
1 Kama mtu yeyote wa kwenu ana ugomvi na mwenzake, anathubutuje kuupeleka kwa wasiomcha Mungu ili kuamuliwa badala ya kuupeleka kwa watakatifu?
2 Je, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Nanyi kama mtauhukumu ulimwengu, je, hamwezi kuamua mambo madogo madogo?
3 Hamjui kwamba tutawahukumu malaika? Je, si zaidi mambo ya maisha haya?
4 Kwa hiyo kama kuna ugomvi miongoni mwenu kuhusu mambo kama haya, je, mnachagua watu ambao wanaonekana hata sio wa heshima katika kundi la waumini kuwa waamuzi kati yenu?
5 Nasema hivi ili mwone aibu. Je, inawezekana kuwa miongoni mwenu hakuna mtu mwenye hekima ya kutosha kuamua ugomvi kati ya waumini?
6 Badala yake ndugu mmoja anampeleka mwenzake mahakamani, tena mbele ya watu wasioamini!
7 Huko kuwa na mashtaka miongoni mwenu ina maana kwamba tayari ni kushindwa kabisa. Kwa nini msikubali kutendewa mabaya? Kwa nini msikubali kunyang’anywa?
8 Badala yake, ninyi wenyewe mwadanganya na kutenda mabaya, tena mwawatendea ndugu zenu.
9 Je, hamjui kwamba wasio haki hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike: Waasherati, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wahanithi, wala walawiti,
10 wala wezi, wala wenye tamaa mbaya, wala walevi, wala wanaodhihaki, wala wanyang’anyi hawataurithi ufalme wa Mungu.
11 Baadhi yenu mlikuwa kama hao. Lakini mlioshwa, mlitakaswa, mlihesabiwa haki kwa jina la Bwana Isa Al-Masihi na katika Roho wa Mungu wetu.
12 “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini si vitu vyote vyenye faida. “Vitu vyote ni halali kwangu”: lakini sitatawaliwa na kitu chochote.
13 “Chakula ni cha tumbo, na tumbo ni la chakula”: lakini Mungu ataviangamiza vyote viwili. Mwili sio kwa ajili ya zinaa, bali kwa ajili ya Bwana Isa, na Bwana Isa kwa ajili ya mwili.
14 Naye Mungu aliyemfufua Bwana Isa kutoka kwa wafu atatufufua sisi pia kwa uweza wake.
15 Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya Al-Masihi mwenyewe? Je, nichukue viungo vya mwili wa Al-Masihi na kuviunganisha na mwili wa kahaba? La hasha!
16 Hamjui kwamba aliyeungwa na kahaba anakuwa mwili mmoja naye? Kwa kuwa imenenwa, “Hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
17 Lakini mtu aliyeungwa na Bwana Isa anakuwa roho moja naye.
18 Ikimbieni zinaa. Dhambi zingine zote atendazo mtu ziko nje ya mwili wake, lakini yeye aziniye hutenda dhambi ndani ya mwili wake mwenyewe.
19 Je, hamjui kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu wa Mungu akaaye ndani yenu, ambaye mmepewa na Mungu? Ninyi si mali yenu wenyewe,
20 kwa maana mmenunuliwa kwa gharama. Kwa hiyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
Cross-references
152
- 1Mat 18:15–17, Act 19:38, 1Co 14:33, 1Co 6:6–7, 1Co 16:1, Act 18:14–15, 1Co 16:15, 1Co 1:2
- 2Mat 19:28, Rev 20:4, Dan 7:22, Luk 22:30, Rev 3:21, Rev 2:26–27, Dan 7:18, Psa 149:5–9
- 3Jud 1:6, Mat 25:41, 1Co 6:4, Luk 8:14, 2Ti 2:4, Luk 21:34, 2Ti 4:10, 2Pe 2:4
- 41Co 5:12, Act 6:2–4
- 51Co 4:14, 1Co 15:34, Jas 3:13–18, 1Co 4:10, 1Co 11:14, Pro 14:8, Jas 1:5, 1Co 3:18
- 6Php 2:14–15, 2Co 6:14, 1Jn 3:11–15, 1Jn 2:9–11, Neh 5:8–9, 1Co 6:7, 1Co 6:1, Act 7:26
- 7Rom 12:17–19, Pro 20:22, 1Pe 2:19–23, 1Pe 3:9, Mat 5:39–41, Jas 4:1–3, 1Th 5:15, Luk 6:29
- 81Th 4:6, Col 3:25, Jas 5:4, Mic 2:2, Mrk 10:19, Lev 19:13, Mal 3:5
- 91Ti 1:9–10, Gal 5:19–21, Eph 5:4–5, Lev 20:13, Lev 18:22, Rev 22:15, Rev 21:8, 1Co 6:10
- 101Co 5:11, Gal 5:21, Eph 4:28, Ezk 22:29, Ezk 22:27, 1Pe 4:15, Mat 23:33, Ezk 22:13
- 111Co 1:30, Col 3:5–7, 1Co 1:2, Rom 6:17–19, Act 22:16, Rom 8:30, 1Pe 1:2, Tit 3:3–7
- 121Co 10:23–33, 1Co 9:27, Heb 12:15–16, Rom 14:14–23, 1Co 8:7–13, 2Th 3:9, Jud 1:12, 1Co 9:12
- 131Co 6:19, 1Co 3:16, Rom 6:12, 1Co 6:15, 1Th 4:3–7, Eph 5:23, Mat 15:17, Rom 14:7–9
- 142Co 4:14, Rom 8:11, Eph 1:19–20, Php 3:21, Act 2:24, Rom 6:4–8, Jhn 6:39–40, 1Th 4:14
- 15Eph 5:30, Rom 12:5, Eph 4:15–16, Col 2:19, 1Co 12:27, Eph 4:12, 1Co 11:3, 1Co 6:19
- 16Gen 2:24, Eph 5:31, Mrk 10:8, Mat 19:5–6, Mat 21:31–32, Heb 11:31, Gen 34:31, Jdg 16:1
- 17Jhn 17:21–23, Gal 2:20, 1Co 12:13, Jhn 3:6, Eph 4:3–4, Eph 5:30, Php 2:5
- 181Pe 2:11, 1Th 4:3, Col 3:5, Rom 6:12–13, 2Ti 2:22, Heb 13:4, 1Co 6:9, Eph 5:3
- 191Co 3:16, 2Co 6:16, 1Pe 2:5, Eph 2:21–22, Psa 100:3, 1Co 6:15–16, Tit 2:14, Rom 14:7–9
- 201Co 7:23, Rom 12:1, 1Pe 2:9, 1Pe 1:18, Heb 9:12, Php 1:20, Gal 3:13, Act 20:28
Topics in this chapter
48
Ablution, Adultery, Arbitration, Assurance, Chastity, Corinth, Covetousness, Drunkard, Expediency, Extortion, Fellowship, Fraternity, Glorifying God, God, Holiness, Holy Spirit, Hygiene, Idolatry, Jesus, the Christ, Judgment, Justification, Lasciviousness, Lawsuits, Litigation, Man, Marriage, Meekness, Power, Prudence, Quotations and Allusions, Redemption, Regeneration, Resurrection, Retaliation, Righteous, Salvation, Sanctification, Self-Denial, Sin, Slander, Sodomy, Speaking, Strife, Temptation, Theft and Thieves, Trinity, Washing, Wicked (People)