Isaya 11
1 Chipukizi litatokea kutoka shina la Yese, kutoka mizizi yake Tawi litazaa tunda.
2 Roho wa Mwenyezi Mungu atakaa juu yake, Roho wa hekima na wa ufahamu, Roho wa shauri na wa uweza, Roho wa maarifa na wa kumcha Mwenyezi Mungu
3 naye atafurahia kumcha Mwenyezi Mungu. Hatahukumu kwa yale ayaonayo kwa macho yake, wala kuamua kwa yale ayasikiayo kwa masikio yake,
4 bali kwa uadilifu atahukumu wahitaji, kwa haki ataamua wanyenyekevu wa dunia. Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, kwa pumzi ya midomo yake atawaua waovu.
5 Haki itakuwa mkanda wake na uaminifu utakuwa mshipi kiunoni mwake.
6 Mbwa-mwitu ataishi pamoja na mwana-kondoo, naye chui atalala pamoja na mbuzi, ndama, mwana simba na ng’ombe wa mwaka mmoja watakaa pamoja, naye mtoto mdogo atawaongoza.
7 Ng’ombe na dubu watalisha pamoja, watoto wao watalala pamoja, na simba atakula majani makavu kama maksai.
8 Mtoto mchanga atacheza karibu na shimo la nyoka, naye mtoto mdogo ataweka mkono wake kwenye kiota cha fira.
9 Hawatadhuru wala kuharibu juu ya mlima wangu mtakatifu wote, kwa kuwa dunia itajawa na kumjua Mwenyezi Mungu kama maji yajazavyo bahari.
10 Katika siku hiyo, Shina la Yese atasimama kama bendera kwa ajili ya mataifa. Mataifa yatakusanyika kwake, na mahali pake pa kupumzikia patakuwa utukufu.
11 Katika siku hiyo Bwana atanyoosha mkono wake mara ya pili kurudisha mabaki ya watu wake waliosalia kutoka Ashuru, Misri, Pathrosi, Kushi, Elamu, Babeli, Hamathi, na kutoka visiwa vya baharini.
12 Atainua bendera kwa mataifa na kuwakusanya Waisraeli walio uhamishoni; atawakusanya watu wa Yuda waliotawanyika kutoka pembe nne za dunia.
13 Wivu wa Efraimu utatoweka, na adui wa Yuda watakatiliwa mbali; Efraimu hatamwonea Yuda wivu, wala Yuda hatakuwa na uadui na Efraimu.
14 Watawashukia katika miteremko ya Wafilisti hadi upande wa magharibi, kwa pamoja watawateka watu nyara hadi upande wa mashariki. Watawapiga Edomu na Moabu, na Waamoni watatawaliwa nao.
15 Mwenyezi Mungu atakausha ghuba ya bahari ya Misri; kwa upepo mkavu ataupeleka mkono wake juu ya Mto Frati. Ataugawanya katika vijito saba ili watu waweze kuuvuka wakiwa wamevaa viatu.
16 Kutakuwa na njia kuu kwa mabaki ya watu wake wale waliosalia kutoka Ashuru, kama ilivyokuwa kwa Israeli walipopanda kutoka Misri.
Cross-references
111
- 1Jer 23:5, Rev 22:16, Zec 6:12, Rev 5:5, Act 13:22–23, Jer 33:15, Isa 53:2, Zec 3:8
- 2Isa 61:1, Jhn 16:13, Eph 1:17–18, 2Ti 1:7, Isa 42:1, Mat 3:16, Col 1:8–9, Jhn 3:34
- 3Jhn 7:24, Luk 2:52, Jhn 8:15–16, 1Sa 16:7, Pro 2:5, 1Co 2:13–15, 1Ki 3:28, Heb 5:14
- 4Rev 19:15, 2Th 2:8, Mal 4:6, Job 4:9, Pro 31:8–9, Psa 72:12–14, Isa 61:1, Mat 5:5
- 5Eph 6:14, 1Jn 1:9, Isa 59:17, Isa 25:1, 2Co 6:7, Rev 3:14, Rev 1:13, 1Pe 4:1
- 6Isa 65:25, Hos 2:18, Ezk 34:25, Rev 5:9–10, Gal 3:26–27, Col 3:3–8, Tit 3:3–5, 1Co 6:9–11
- 8Psa 140:3, Isa 59:5
- 9Hab 2:14, Isa 52:10, Psa 98:2–3, Mic 4:2–4, Job 5:23, Isa 60:1–22, Isa 59:19, Psa 72:19
- 10Rom 15:9–12, Luk 2:32, Isa 11:1, Mat 2:1–2, Jhn 12:32, Mat 12:21, Mat 8:11, Mat 11:28–30
- 11Zec 10:8–12, Mic 7:12, Hos 3:4–5, Isa 10:20, Rom 11:26, Lev 26:40–42, Jer 30:8–11, Deu 4:27–31
- 12Isa 43:6, Isa 56:8, Psa 147:2, Zep 3:10, Zec 10:6, Isa 11:10, Isa 27:13, Psa 68:22
- 13Jer 3:18, Ezk 37:16–24, Hos 1:11, Isa 9:21, Isa 7:1–6
- 14Jol 3:19, Dan 11:41, Isa 25:10, Jer 49:28, Mat 8:11, Amo 9:12, Isa 60:14, Oba 1:18–19
- 15Rev 16:12, Zec 10:11, Isa 50:2, Isa 7:20, Isa 19:16, Isa 51:9–10, Ezk 29:10, Ezk 30:12
- 16Isa 19:23, Isa 35:8–10, Isa 11:11, Isa 62:10, Exo 14:26–29, Isa 57:14, Isa 51:10, Isa 40:3–4
Topics in this chapter
40
Allegory, Ammonites, Animals, Asp, Babylon, Bear, Branch, Church, Cockatrice, Edomites, Elam, Ensign, Ephraim, Ethiopia, Gentiles, Girdle, God, Hamath, Highways, Holy Spirit, Isaiah, Island, Israel, Prophecies Concerning, Jesus, the Christ, Kindness, Knowledge, Leopard, Meekness, Nile, Pathros, Peace, Poor, Power, Prophecy, Quotations and Allusions, Righteous, Trinity, Wicked (People), Wisdom, Wolf