Isaya 57
1 Mwenye haki hupotea, wala hakuna hata mmoja awazaye hilo moyoni mwake; watu wanaomcha Mungu huondolewa, wala hakuna hata mmoja anayeelewa kuwa wenye haki wameondolewa ili wasipatikane na maovu.
2 Wale wanaoenda kwa unyofu huwa na amani; hupata pumziko wanapolala mautini.
3 “Lakini ninyi: Njooni hapa, ninyi wana wa wachawi, ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!
4 Mnamdhihaki nani? Ni nani mnayemcheka kwa dharau, na kumtolea ndimi zenu? Je, ninyi si watoto wa waasi, uzao wa waongo?
5 Mnawaka tamaa katikati ya mialoni na chini ya kila mti uliotanda matawi; mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde na chini ya majabali yenye mianya.
6 “Sanamu zilizo kati ya mawe laini ya mabondeni ndizo fungu lenu; hizo ndizo sehemu yenu. Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji, na kutoa sadaka za nafaka. Katika haya yote, niendelee kuona huruma?
7 Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka, huko ulienda kutoa dhabihu zako.
8 Nyuma ya milango yako na miimo yako umeweka alama zako za kipagani. Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako, umepanda juu yake na kukipanua sana; ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao, nawe uliangalia uchi wao.
9 Ulienda kwa Moleki ukiwa na mafuta ya zeituni, na ukaongeza manukato yako. Ukawatuma wajumbe wako mbali sana, ukashuka kwenye kaburi lenyewe!
10 Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote, lakini hukusema, ‘Hakuna tumaini.’ Ulipata uhuisho wa nguvu zako, kwa sababu hiyo hukuzimia.
11 “Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa hata ukawa mwongo kwangu, wala hukunikumbuka au kutafakari hili moyoni mwako? Si ni kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu hata huniogopi?
12 Nitaifunua haki yako na matendo yako, nayo hayatakufaidi.
13 Utakapolia kwa kuhitaji msaada, sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe! Upepo utazipeperusha zote, pumzi peke yake itazipeperusha, Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake, atairithi nchi na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”
14 Tena itasemwa: “Jengeni, jengeni, itengenezeni njia! Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”
15 Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu, yeye aliyeinuliwa sana, yeye aishiye milele, ambaye jina lake ni Mtakatifu: “Ninaishi mahali palipoinuka na patakatifu, lakini pia pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu, na mwenye roho ya unyenyekevu, ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu na kuihuisha mioyo yao waliotubu.
16 Sitaendelea kulaumu milele, wala sitakasirika siku zote, kwa kuwa roho ya mwanadamu ingezimia mbele zangu: yaani pumzi ya mwanadamu niliyemuumba.
17 Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi; nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira, na bado aliendelea katika njia zake za tamaa.
18 Nimeziona njia zake, lakini nitamponya, nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,
19 nikiumba sifa midomoni ya waombolezaji katika Israeli. Amani, amani, kwa wale walio mbali na kwa wale walio karibu,” asema Mwenyezi Mungu. “Nami nitawaponya.”
20 Bali waovu ni kama bahari ichafukayo, ambayo haiwezi kutulia, mawimbi yake hutupa takataka na matope.
21 Mungu wangu asema, “Hakuna amani kwa waovu.”
Cross-references
161
- 12Ki 22:20, 2Ch 34:28, Psa 12:1, Mic 7:2, Isa 42:25, Isa 47:7, 2Ch 35:24, Mal 2:2
- 2Rev 14:13, 2Co 5:1, Job 3:17, Luk 2:29, Ecc 12:7, 2Co 5:8, Mat 25:21, 2Ch 16:14
- 3Mat 16:4, 1Jn 3:10, Jas 4:4, Hos 1:2, Mat 12:34, Isa 1:21, Jhn 8:40–44, Luk 3:7
- 42Pe 2:13, Exo 9:17, Isa 1:4, Psa 35:21, Lam 2:15–16, Job 16:9–10, Jdg 16:25–27, Psa 22:17
- 5Isa 1:29, 2Ki 16:3–4, Ezk 16:20, Lev 18:21, 2Ki 23:10, Jer 3:13, Jer 2:20, Jer 7:31
- 6Jer 3:9, Jer 7:18, Hab 2:19, Jer 44:17–25, Jer 5:9, Jer 5:29, Isa 66:3, Ezk 20:39
- 7Ezk 23:41, Ezk 16:16, Jer 2:20, Ezk 20:28–29, Ezk 16:25, Jer 3:6, Jer 3:2, Ezk 23:17
- 8Ezk 16:32, Ezk 16:25–28, Ezk 23:41, Ezk 8:8–12, Ezk 23:2–20
- 9Ezk 23:16, Ezk 23:40, Isa 30:1–6, Col 2:18, Isa 31:1–3, 2Ki 16:7–11, Hos 12:1, Ezk 16:33
- 10Jer 2:25, Jer 18:12, Jer 5:3, Jer 2:36, 2Ch 28:22–23, Ezk 24:12, Jer 9:5, Jer 44:17–18
- 11Isa 51:12–13, Pro 29:25, Psa 50:21, Jer 3:21, Jer 2:32, Isa 59:3–4, Ecc 8:11, Isa 26:10
- 12Jer 7:4–11, Mat 23:13, Rom 3:10–20, Mic 3:2–4, Isa 1:11–15, Rom 10:2–3, Isa 64:5, Isa 29:15
- 13Psa 37:9, Psa 37:3, Isa 65:25, Isa 56:7, Isa 66:20, Jdg 10:14, Isa 11:9, Isa 65:9
- 14Isa 62:10, Luk 3:5–6, Isa 35:8, Isa 40:3, Jer 18:15, Rom 14:13, 1Co 8:13, Heb 12:13
- 15Psa 34:18, Isa 66:1–2, Psa 138:6, Psa 147:3, Exo 15:11, Dan 4:34, Psa 51:17, Psa 90:2
- 16Mic 7:18, Jer 10:24, Psa 85:5, Psa 103:9–16, Heb 12:9, Psa 78:38–39, Job 34:14–15, Num 16:22
- 17Isa 56:11, Jer 6:13, Col 3:5, 2Pe 2:14, Eph 5:3–5, Jer 22:17, Jer 5:3, Isa 9:13
- 18Jer 33:6, Rev 7:17, Jer 3:22, Hos 14:4–8, Jer 31:3, Jer 13:17, Jer 31:18–20, Ezk 16:60–63
- 19Act 2:39, Heb 13:15, Eph 6:19, Luk 2:14, Luk 10:5–6, Act 10:36, Luk 21:15, Isa 6:7
- 20Pro 4:16–17, Isa 3:11, Job 18:5–14, Jud 1:12, Job 20:11–29, Psa 73:18–20, Job 15:20–24
- 21Isa 48:22, Isa 3:11, 2Ki 9:22, Rom 3:16–17, Isa 59:8
Topics in this chapter
42
Adultery, Afflictions and Adversities, Anger, Anointing, Backsliders, Blessing, Character, Chastisement, Church, Commandments, Confidence, Covetousness, Death, Eternity, Faith, Falsehood, Fellowship, God, Heaven, Hell, Holiness, Humility, Idolatry, Impenitence, Infidelity, Isaiah, Legends (Inscriptions), Minister, Christian, Molech, Offerings, Peace, Perfume, Remorse, Repentance, Righteous, Salvation, Scoffing, Sin, Stumbling, Vanity, Wicked (People), Works