Waebrania 10
1 Torati ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kupitia kwa dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu.
2 Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi.
3 Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka,
4 kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
5 Kwa hiyo, Al-Masihi alipokuja duniani, alisema: “Dhabihu na sadaka hukuzitaka, bali mwili uliniandalia;
6 sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukupendezwa nazo.
7 Ndipo niliposema, ‘Mimi hapa, nimekuja, imeandikwa kunihusu katika kitabu: Nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu.’ ”
8 Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo” (ingawa sheria iliagiza zitolewe).
9 Kisha akasema, “Mimi hapa, nimekuja kuyafanya mapenzi yako.” Aondoa lile agano la kwanza ili kuimarisha la pili.
10 Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu kupitia kwa sadaka ya mwili wa Isa Al-Masihi alioutoa mara moja tu.
11 Kila kuhani husimama siku kwa siku akifanya huduma yake ya ibada, na kutoa tena na tena dhabihu zile zile, ambazo haziwezi kamwe kuondoa dhambi.
12 Lakini huyu kuhani baada ya kutoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi kwa wakati wote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu.
13 Tangu wakati huo anangoja hadi adui zake wawekwe chini ya miguu yake,
14 kwa sababu kwa dhabihu moja amewafanya wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.
15 Pia Roho wa Mungu anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema:
16 “Hili ndilo agano nitakalofanya nao baada ya siku hizo, asema Mwenyezi Mungu. Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika katika nia zao.”
17 Kisha aongeza kusema: “Dhambi zao na kutokutii kwao sitakumbuka tena.”
18 Basi haya yaliposamehewa, hakuna tena dhabihu yoyote inayohitajika kwa ajili ya dhambi.
19 Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Isa,
20 kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani mwili wake,
21 basi kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
22 sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Al-Masihi na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.
23 Tushike kwa uthabiti lile tumaini la ukiri wetu bila kuyumbayumba, kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.
24 Tuangaliane na kuhimizana sisi kwa sisi katika upendo na katika kutenda mema.
25 Wala tusiache kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tuhimizane sisi kwa sisi kadiri tuonavyo Siku ile inakaribia.
26 Tukiendelea kutenda dhambi kwa makusudi baada ya kupokea ufahamu wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.
27 Lakini kinachobaki ni kungoja kwa hofu hukumu ya moto uwakao, utakaowaangamiza adui za Mungu.
28 Yeyote aliyeikataa Torati ya Musa alikufa pasipo huruma kwa ushahidi wa watu wawili au watatu.
29 Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani anayostahili kupewa mtu aliyemkanyaga Mwana wa Mungu chini ya nyayo zake, yeye aliyeifanya damu ya agano iliyomtakasa kuwa kitu najisi na kumtendea maovu Roho wa neema?
30 Kwa kuwa tunamjua yeye aliyesema, “Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.” Tena asema, “Mwenyezi Mungu atawahukumu watu wake.”
31 Ni jambo la kutisha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.
32 Kumbukeni siku zile za kwanza, ambazo baada ya kutiwa nuru mlistahimili mashindano makali ya maumivu.
33 Wakati mwingine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale waliotendwa hivyo.
34 Mliwahurumia wale waliokuwa kifungoni, mkikubali kwa furaha kunyang’anywa mali yenu kwa maana mlijua kwamba mnayo mali iliyo bora zaidi idumuyo.
35 Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno.
36 Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi.
37 Kwa kuwa, “Bado kitambo kidogo tu, yeye ajaye atakuja wala hatakawia.”
38 Na, “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Naye akisitasita, sina furaha naye.”
39 Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.
Cross-references
280
- 1Heb 9:11, Heb 8:5, Col 2:17, Heb 9:23, Heb 7:18–19, Heb 9:25, Heb 10:11–18, Heb 9:8–9
- 2Isa 43:25, Mic 7:19, Psa 103:12, Isa 44:22, Heb 10:17, Heb 9:13–14
- 3Heb 9:7, Exo 30:10, Lev 23:27–28, Lev 16:34, Lev 16:6–11, Lev 16:29–30, Num 29:7–11, Lev 16:21–22
- 4Heb 10:11, Isa 1:11–15, Mic 6:6–8, Rom 11:27, 1Jn 3:5, Heb 10:8, Mrk 12:33, Jhn 1:29
- 5Psa 40:6–8, Isa 1:11, Isa 7:14, 1Pe 2:24, Mat 1:20–23, Heb 10:7, Heb 1:6, Heb 2:14
- 6Heb 10:4, Mal 1:10, Mat 3:17, Psa 147:11, Eph 5:2, Lev 1:1–6, Php 4:18
- 7Psa 40:7–8, Jhn 4:34, Jhn 6:38, Jhn 5:30, Heb 10:9–10, Jer 36:2, Gen 3:15, Pro 8:31
- 8Heb 10:5, Mrk 12:33
- 9Heb 7:18–19, Heb 12:27–28, Heb 9:11–14, Heb 10:7, Heb 8:7–13
- 10Heb 10:14, Heb 10:12, 1Co 6:11, Heb 7:27, Jhn 17:19, Heb 13:12, Heb 9:12, 1Co 1:30
- 11Heb 10:4, Heb 5:1, Num 28:3, Psa 50:8–13, Isa 1:11, Heb 10:1, Heb 7:27, Dan 11:31
- 12Heb 1:3, Col 3:1, Rom 8:34, Heb 8:1, Heb 9:12, Act 2:33–34
- 13Heb 1:13, Psa 110:1, Luk 20:43, 1Co 15:25, Mrk 12:36, Mat 22:44, Act 2:35, Dan 2:44
- 14Heb 9:14, Heb 7:25, Heb 10:1, Heb 2:11, Heb 13:12, Rom 15:16, Act 20:32, Eph 5:26
- 15Heb 3:7, Rev 3:6, 2Pe 1:21, Rev 2:11, Act 28:25, Jhn 15:26, Rev 3:13, Heb 9:8
- 16Jer 31:33–34, Heb 8:8–12, Rom 11:27
- 17Heb 8:12, Jer 31:34
- 18Heb 10:2, Heb 10:14
- 19Eph 2:18, Heb 9:12, Heb 4:16, Eph 3:12, Rom 5:2, Heb 12:28, 1Jn 4:17, Rom 8:15
- 20Jhn 14:6, Jhn 10:9, Heb 9:3, Lev 16:2, Heb 6:19, Mat 27:51, Jhn 10:7, Mrk 15:38
- 21Heb 2:17, Heb 4:14–16, Heb 8:1, Heb 6:20, Heb 3:1, Eph 2:19–22, Heb 7:26, Heb 3:3–6
- 22Ezk 36:25, Jhn 3:5, Eph 5:26, 1Pe 3:21, 1Co 6:11, Heb 7:19, Heb 4:16, 2Co 7:1
- 231Th 5:24, 1Co 1:9, 2Th 3:3, Heb 6:18, Tit 1:2, Heb 3:6, 1Co 10:13, Rev 3:11
- 241Th 5:11, 1Jn 3:18, Heb 13:1, Gal 5:13, Col 3:16, Tit 3:8, 1Th 3:12–13, 1Ti 6:18
- 25Act 2:42, 1Th 5:11, Mat 18:20, Heb 3:13, Heb 10:24, 1Co 5:4, 1Th 4:18, Act 20:7
- 262Pe 2:20–22, Heb 6:4–6, Jhn 9:41, Luk 12:47, Mat 12:43–45, Num 15:28–31, Mat 12:31–32, Jas 4:17
- 27Isa 26:11, Zep 1:18, Heb 2:3, Heb 9:27, Heb 12:25, Mat 13:50, Nam 1:2, Mal 4:1
- 28Heb 2:2, Deu 19:15, Deu 17:2–13, Mat 18:16, Deu 19:13, 2Co 13:1, Num 15:30–31, Jhn 8:17
- 29Eph 4:30, Heb 6:6, Isa 63:10, 1Co 11:27, Luk 12:10, Act 7:51, Heb 2:3, Mat 12:31–32
- 30Deu 32:35–36, Rom 12:19, Nam 1:2, Psa 50:4, 2Co 5:10, Psa 135:14, Psa 96:13, Psa 98:9
- 31Mat 10:28, Luk 12:5, Heb 12:29, Isa 33:14, Psa 76:7, Psa 90:11, Mat 16:16, Heb 10:27
- 32Heb 6:4, 2Ti 4:7–8, Gal 3:3–4, 2Ti 2:3–13, Heb 12:4, Act 8:1–3, Php 3:16, 2Jn 1:8
- 331Co 4:9, Php 4:14, Heb 11:36, Php 1:7, Isa 51:7, 2Co 12:10, Psa 74:22, 2Ti 1:16–18
- 341Pe 1:4, 2Ti 1:16, Mat 6:19–20, Mat 5:11–12, Eph 6:20, Heb 11:16, Jas 1:2, 1Ti 6:19
- 351Co 15:58, Gal 6:8–10, Heb 3:6, Luk 14:14, Heb 11:26, Heb 4:14, Mat 5:12, Heb 3:14
- 36Heb 12:1, Psa 37:7, Jas 5:7–11, 1Co 13:7, Luk 21:19, Heb 6:15, Rom 2:7, Rom 8:25
- 37Jas 5:7–9, Hab 2:3–4, Luk 18:8, Isa 26:20, Rev 22:20, Isa 60:22, 2Pe 3:8
- 38Gal 3:11, Hab 2:4, Rom 1:17, Psa 85:8, Heb 6:4–6, Ezk 3:20, Mat 13:21, Psa 147:11
- 391Jn 5:5, 1Pe 1:5, 2Th 2:12–14, Mrk 16:16, 1Jn 5:16, 2Pe 3:7, 1Sa 15:11, Jhn 6:40
Topics in this chapter
74
Ablution, Afflictions and Adversities, Apostasy, Assurance, Atonement, Backsliders, Blasphemy, Blessing, Blood, Boldness, Bull, Character, Church, Commandments, Communion, Conscience, Constancy, Decision, Emulation, Evidence, Faith, Fellowship, Fight of Faith, God, Godlessness, Gospel, Heart, Heaven, Holiness, Holy Spirit, Immortality, Infidelity, Jesus, the Christ, Joy, Judgment, Judgments, Law, Love, Meekness, Obedience, Offerings, Patience, Paul, Perfection, Persecution, Perseverance, Prayer, Priest, Prophecy, Punishment, Purification, Purity, Quotations and Allusions, Regeneration, Reprobacy, Resignation, Reward, Righteous, Sanctification, Scoffing, Sin, Sprinkling, Stability, Suffering, Symbols and Similitudes, Types, Vail, War, Wicked (People), Witness, Word of God, Works, Worship, Zeal, Religious