Isaya 26
1 Katika siku ile, wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda: Tuna mji ulio na nguvu, Mungu huufanya wokovu kuwa kuta zake na maboma yake.
2 Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia, taifa lidumishalo imani.
3 Utamlinda katika amani kamilifu yeye ambaye moyo wake ni thabiti kwa sababu anakutumaini wewe.
4 Mtumaini Mwenyezi Mungu milele, kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, ni Mwamba wa milele.
5 Huwashusha wale wajikwezao, huushusha chini mji wenye kiburi, huushusha hadi ardhini na kuutupa chini mavumbini.
6 Miguu huukanyagia chini: miguu ya hao waliodhulumiwa, hatua za hao maskini.
7 Mapito ya wenye haki ni nyoofu. Ewe uliye Mwenye Haki, waisawazisha njia ya mtu mnyofu.
8 Naam, Mwenyezi Mungu, tukienenda katika sheria zako, twakungojea wewe, jina lako na sifa zako ndizo shauku za mioyo yetu.
9 Nafsi yangu yakutamani wakati wa usiku, wakati wa asubuhi roho yangu yakuonea shauku. Hukumu zako zinapokuja juu ya dunia, watu wa ulimwengu hujifunza haki.
10 Ingawa neema yaoneshwa kwa waovu, hawajifunzi haki; hata katika nchi ya unyofu huendelea kutenda mabaya wala hawazingatii utukufu wa Mwenyezi Mungu.
11 Ee Mwenyezi Mungu, mkono wako umeinuliwa juu, lakini hawauoni. Wao na waone wivu wako kwa ajili ya watu wako tena waaibishwe, moto uliowekwa akiba kwa ajili ya adui zako na uwateketeze.
12 Mwenyezi Mungu, unaamuru amani kwa ajili yetu, yale yote tuliyoweza kuyakamilisha ni wewe uliyetenda kwa ajili yetu.
13 Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametutawala, lakini jina lako pekee ndilo tunaloliheshimu.
14 Wao sasa wamekufa, wala hawako tena hai, roho za waliokufa hazitarudi tena. Uliwaadhibu na kuwaangamiza, umefuta kumbukumbu lao lote.
15 Umeliongeza hilo taifa, Ee Mwenyezi Mungu, umeliongeza hilo taifa. Umejipatia utukufu kwa ajili yako mwenyewe, umepanua mipaka yote ya nchi.
16 Mwenyezi Mungu, walikujia katika taabu yao, wewe ulipowarudi, waliweza kuomba kwa kunong’ona tu.
17 Kama mwanamke mwenye mimba aliyekaribia kuzaa anavyogaagaa na kulia kwa ajili ya maumivu yake, ndivyo tulivyokuwa mbele zako, Ee Mwenyezi Mungu.
18 Tulikuwa na mimba, tuligaagaa kwa maumivu, lakini tulizaa upepo. Hatukuleta wokovu duniani, hatujazaa watu katika ulimwengu huu.
19 Lakini wafu wenu wataishi, nayo miili yao itafufuka. Ninyi mnaokaa katika mavumbi, amkeni mkashangilie kwa furaha. Umande wenu ni kama umande wa asubuhi, dunia itawazaa wafu wake.
20 Nendeni, watu wangu, ingieni vyumbani mwenu na mfunge milango nyuma yenu, jificheni kwa kitambo kidogo hadi ghadhabu yake ipite.
21 Tazama, Mwenyezi Mungu anakuja kutoka makao yake ili kuwaadhibu watu wa dunia kwa ajili ya dhambi zao. Dunia itadhihirisha umwagaji damu juu yake, wala haitaendelea kuwaficha watu wake waliouawa.
Cross-references
168
- 1Isa 62:11, Isa 60:18, Zec 2:5, Eph 5:19–20, Psa 48:12, Isa 27:1–2, Jer 33:11, Isa 25:9
- 2Rev 5:9, Isa 60:11, 1Pe 2:9, Psa 118:20, Isa 62:10, Isa 62:2, Isa 54:14, Exo 19:6
- 3Php 4:7, Jhn 16:33, Jhn 14:27, Jer 17:7–8, Psa 9:10, Rom 5:1, Psa 85:7–8, Rom 4:18–21
- 4Isa 12:2, Psa 62:8, Psa 55:22, Php 4:13, Psa 18:2, Psa 62:11, Pro 3:5–6, Psa 46:1
- 5Rev 18:2, Job 40:11–13, Jer 51:37, Isa 13:11, Jer 51:25–26, Jer 51:64, Isa 32:19, Jer 50:31–32
- 6Luk 10:19, Rom 16:20, Rev 2:26, Jas 2:5, Jos 10:24, Isa 25:10, Jer 50:45, Dan 7:27
- 7Eph 2:10, Isa 42:16, 1Jn 3:10, 1Jn 3:7, 2Co 1:12, Pro 20:7, Psa 11:7, Job 27:5–6
- 8Jas 5:7–11, Psa 37:3–7, Isa 33:2, Psa 65:6, Exo 3:15, 2Th 3:5, Act 1:4, Rom 8:25
- 9Mat 6:33, Psa 63:1, Psa 119:62, Sng 3:1–4, Psa 63:6–7, Rev 11:13, Luk 6:12, Psa 58:11
- 10Hos 11:7, Jhn 5:37–38, Rom 2:4–5, Ecc 3:16, Deu 32:15, Mic 3:10–12, Exo 8:31–32, Exo 8:15
- 11Heb 10:27, Mic 5:9, Isa 5:24, Act 28:27, 1Sa 6:9, Jer 5:3, Jer 44:28, Job 34:27
- 12Eph 2:10, Psa 57:2, Psa 29:11, Ezk 20:14, Heb 13:20, Jer 33:6, Deu 30:6, Jhn 14:27
- 13Isa 63:7, Isa 2:8, Isa 10:11, Rom 6:22, Heb 13:15, 2Ch 12:8, Jos 23:7, Isa 51:22
- 14Pro 10:7, Rev 18:2–3, Hab 2:18–20, Isa 8:19, Isa 51:12–13, Psa 106:28, Isa 14:19–22, Isa 10:3
- 15Isa 9:3, Jhn 13:31–32, Jhn 17:1, Neh 9:23, Isa 33:17, Jhn 12:23–28, Isa 44:23, Jhn 15:8
- 16Hos 5:15, Psa 50:15, Psa 77:1–2, Psa 142:2, 2Ch 33:12–13, Jdg 10:9–10, Isa 37:3, 1Sa 1:15
- 17Isa 13:8, Isa 21:3, Jhn 16:21, Jer 4:31, 1Th 5:3, Jer 30:6, Psa 48:6, Jer 6:24
- 18Psa 17:14, Hos 13:13, 2Ki 19:3, Isa 59:4, Isa 37:3, Isa 33:11, 1Sa 11:13, 1Jn 5:19
- 19Dan 12:2, Ezk 37:1–14, Mat 27:52, Eph 5:14, Hos 13:14, Rev 20:12–13, Psa 71:20, Hos 6:2
- 20Psa 30:5, Psa 27:5, Isa 54:7–8, Mat 6:6, Psa 91:4, Pro 18:10, Psa 17:8, 2Co 4:17
- 21Rev 6:9–11, Isa 13:11, Jud 1:14–15, Isa 18:4, Job 16:18, Mic 1:3–8, Rev 16:6, Num 35:32–33
Topics in this chapter
39
Afflictions and Adversities, Blessing, Blindness, Bulwark, Character, Chastisement, Death, Desire, Dew, Envy, Faith, Gates, God, Holiness, Homicide, Immortality, Impenitence, Injustice, Integrity, Isaiah, Israel, Prophecies Concerning, Judgments, Man, Peace, Persecution, Power, Pride, Psalms, Regeneration, Resurrection, Righteous, Rising, Salvation, Seekers, Sin, Spirituality, Waiting, War, Wicked (People)