Kutoka 34
1 Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitaandika juu yake maneno yale yaliyokuwa kwenye vile vibao vya kwanza, ulivyovivunja.
2 Uwe tayari asubuhi, kisha upande juu ya Mlima Sinai. Uje mbele zangu kukutana nami huko juu ya mlima.
3 Mtu yeyote asije nawe, wala asionekane mtu popote mlimani; wala kondoo na mbuzi au ng’ombe wasilishe mbele ya huo mlima.”
4 Kwa hiyo Musa akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, naye akapanda juu ya Mlima Sinai asubuhi na mapema, kama Mwenyezi Mungu alivyokuwa amemwagiza, akachukua vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake.
5 Kisha Mwenyezi Mungu akashuka katika wingu akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina lake, Mwenyezi Mungu.
6 Mwenyezi Mungu akapita mbele ya Musa, akitangaza, “Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Mungu mwenye huruma na neema, asiye mwepesi wa hasira, mwingi wa upendo na uaminifu,
7 akidumisha upendo kwa maelfu, pia akisamehe uovu, uasi na dhambi. Lakini haachi kuadhibu mwenye hatia; huwaadhibu watoto na watoto wao kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata katika kizazi cha tatu na cha nne.”
8 Mara Musa akasujudu na kuabudu.
9 Musa akasema, “Ee Bwana, kama nimepata kibali mbele zako, basi Bwana uende pamoja nasi. Ingawa watu hawa ni wenye shingo ngumu, samehe uovu wetu na dhambi yetu, tuchukue kuwa urithi wako.”
10 Kisha Mwenyezi Mungu akasema: “Tazama, ninafanya agano nanyi. Mbele ya watu wako wote nitafanya maajabu ambayo hayajafanyika katika taifa lolote katika ulimwengu wote. Watu wale mnaoishi miongoni mwao wataona jinsi ilivyo ya kushangaza kazi nitakayowafanyia Mimi, Mwenyezi Mungu wenu.
11 Tii yale ninayokuamuru leo. Tazama nawafukuza mbele yako Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
12 Uwe mwangalifu, usifanye agano na wale wanaokaa katika nchi ile unayoiendea, la sivyo watakuwa mtego katikati yako.
13 Bomoa madhabahu yao, vunja mawe yao ya kuabudia, na ukatekate nguzo zao za Ashera.
14 Usiabudu mungu mwingine, kwa kuwa Mwenyezi Mungu, ambaye jina lake ni Wivu, ni Mungu mwenye wivu.
15 “Uwe mwangalifu usifanye agano na wale watu wanaoishi katika nchi, kwa maana wakati wanapojifanyia ukahaba kwa miungu yao na kuwatolea kafara, watakualika wewe, nawe utakula sadaka za matambiko yao.
16 Unapowachagua baadhi ya binti zao kuwa wake wa wana wenu na binti hao wakajifanyia ukahaba kwa miungu yao, watawaongoza wana wenu kufanya vivyo hivyo.
17 “Usijifanyie sanamu za kusubu.
18 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, kama nilivyokuamuru. Fanya hivi kwa wakati ulioamriwa, katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa kuwa katika mwezi huo ndipo wewe ulipotoka Misri.
19 “Mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo ni mali yangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wote wa kiume wa mifugo yako, ikiwa ni wa ng’ombe au wa kondoo au mbuzi.
20 Utakomboa mzaliwa wa kwanza wa punda kwa mwana-kondoo, lakini kama humkomboi, utavunja shingo yake. Utakomboa wazaliwa wako wa kwanza wote wa kiume. “Mtu yeyote asije mbele zangu mikono mitupu.
21 “Kwa siku sita utafanya kazi, lakini siku ya saba utapumzika, hata ikiwa ni majira ya kulima au ya kuvuna lazima upumzike.
22 “Utaadhimisha Sikukuu ya Majuma kwa malimbuko ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Mavuno mwishoni mwa mwaka.
23 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote watakuja mbele za Bwana Mungu Mwenyezi, Mungu wa Israeli.
24 Nitawafukuza mataifa mbele yako na kupanua mipaka ya nchi yako, wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati unapoenda mara tatu kila mwaka kuonana na Mwenyezi Mungu, Mungu wako.
25 “Usinitolee damu ya dhabihu pamoja na kitu chochote chenye chachu, wala usibakize dhabihu yoyote ya Sikukuu ya Pasaka hadi asubuhi.
26 “Leta matunda ya kwanza yaliyo bora zaidi ya ardhi yako katika nyumba ya Mwenyezi Mungu, Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”
27 Kisha Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya agano na wewe pamoja na Israeli.”
28 Musa alikuwa huko pamoja na Mwenyezi Mungu kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya agano, yaani zile Amri Kumi.
29 Musa alipoteremka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa uking’aa, kwa sababu alikuwa amezungumza na Mwenyezi Mungu.
30 Haruni na Waisraeli wote walipomwona Musa, kuwa uso wake unang’aa, waliogopa kumkaribia.
31 Lakini Musa akawaita, kwa hiyo Haruni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao.
32 Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zote Mwenyezi Mungu alizompa katika Mlima Sinai.
33 Musa alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake.
34 Lakini kila wakati Musa alipoingia mbele za Mwenyezi Mungu kuzungumza naye, aliondoa ule utaji hadi alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa,
35 waliona kuwa uso wake unang’aa. Kisha Musa angerudisha utaji juu ya uso wake hadi alipoingia ili kuzungumza na Mwenyezi Mungu.
Cross-references
228
- 1Exo 32:19, Psa 119:89, Deu 10:1–4, Exo 31:18, Exo 34:28, Exo 32:16, Deu 9:15–17
- 2Exo 19:20, Deu 9:25, Exo 19:11, Exo 24:12, Exo 19:24
- 3Exo 19:12–13, Exo 19:21, 1Ti 2:5, Heb 12:20, Lev 16:17
- 5Exo 33:19, Num 11:25, Luk 9:34–35, Exo 33:9, Num 11:17, Psa 102:21, Pro 18:10, Deu 32:3
- 6Psa 86:15, Jol 2:13, Psa 103:8–13, Psa 145:8, Neh 9:17, Jon 4:2, Num 14:17–19, Psa 86:5
- 7Exo 20:5–6, Psa 103:3, Deu 5:9–10, Eph 1:7, 1Jn 1:9, Nam 1:2–3, Num 14:18–23, Jer 32:18
- 8Exo 4:31, Gen 17:3, 2Ch 20:18
- 9Psa 33:12, Psa 94:14, Deu 32:9, Exo 33:13–17, Psa 135:4, Jer 10:16, Psa 28:9, Exo 32:9
- 10Deu 10:21, Psa 77:14, Isa 64:3, Psa 66:5, Jer 32:21, 2Sa 7:23, Psa 66:3, Psa 78:12
- 11Exo 33:2, Deu 6:25–7:1, Exo 3:17, Exo 3:8, Gen 15:18–21, Deu 6:3, Deu 28:1, Jhn 14:21
- 12Exo 23:32–33, Jos 23:12–13, Deu 7:2, Jdg 2:2–3, Deu 7:16, Psa 106:36, Jdg 8:27
- 132Ki 18:4, Deu 7:5, Exo 23:24, Deu 7:25–26, Deu 16:21, Deu 12:2–3, Jdg 6:25, 2Ch 31:1
- 14Deu 4:24, Deu 32:21, 1Co 10:22, Mat 4:10, Exo 20:3–5, Nam 1:2, Deu 29:20, Deu 6:15
- 15Jdg 2:17, Deu 31:16, 1Co 8:4, Num 25:2, Psa 106:28, 1Co 8:10, 1Co 10:27, Lev 17:7
- 16Deu 7:3–4, 1Ki 11:2–4, Ezr 9:2, Num 25:1–2, Neh 13:25, Neh 13:23, 2Co 6:14–17
- 17Lev 19:4, Exo 32:8, Isa 46:6–7, Act 19:26, Jer 10:14, Act 17:29
- 18Exo 13:4, Lev 23:6, Deu 16:1–4, Exo 13:6–7, Mrk 14:1, Exo 12:2, Exo 23:15, Exo 12:15–20
- 19Exo 13:2, Exo 22:29, Exo 13:12, Num 18:15–17, Ezk 44:30, Luk 2:23
- 20Exo 13:13, Exo 23:15, Deu 16:16, Num 18:15, Exo 13:15, 1Sa 9:7–8, 2Sa 24:24, Num 3:45–51
- 21Exo 23:12, 1Sa 8:12, Deu 21:4, Luk 13:14, Exo 35:2, Luk 23:56, Isa 30:24, Deu 5:12–15
- 22Exo 23:16, Deu 16:10–15, Num 28:16–31, Jhn 7:2, Act 2:1, Num 29:12–39
- 23Exo 23:14, Exo 23:17, Deu 16:16, Gen 32:28, Gen 33:20, Psa 84:7
- 24Psa 78:55, Exo 33:2, Act 18:10, 1Ch 4:10, Deu 12:20, Pro 16:7, Psa 80:8, Deu 7:1
- 25Exo 23:18, Exo 12:10, Exo 12:8, Exo 12:20, Deu 16:3, Num 9:12, 1Co 5:7–8, Exo 29:34
- 26Exo 23:19, Deu 14:21, Deu 26:2, Mat 6:33, 1Co 15:20, Pro 3:9–10, Deu 26:10, Jas 1:18
- 27Exo 24:4, Deu 31:9, Deu 4:13, Exo 17:14, Exo 34:10, Exo 24:7
- 28Exo 34:1, Deu 9:25, Deu 4:13, Deu 9:18, Exo 24:18, Exo 31:18, Exo 32:16, 2Co 3:7
- 29Mat 17:2, Luk 9:29, Exo 32:15, Rev 1:16, 2Co 3:7–9, 2Co 3:13, Rev 10:1, Act 6:15
- 30Mrk 9:3, Luk 5:8, Num 12:8, Mrk 9:15
- 31Exo 3:15, Exo 24:1–3, Gen 45:3, Gen 45:15
- 32Exo 21:1, 1Co 11:23, 1Co 15:3, Num 15:40, 1Ki 22:14, Mat 28:20, Exo 24:3
- 332Co 4:4–6, 2Co 3:13–18, Rom 10:4
- 342Co 3:16, Heb 10:19–22, Heb 4:16
- 35Exo 34:29–30, Php 2:15, Mat 13:43, Jhn 5:35, Dan 12:3, Ecc 8:1, Mat 5:16
Topics in this chapter
69
Agriculture, Alliances, Amorites, Ass (Donkey), Blessing, Canaanites, Children, Church, Cloud, Communion, Company, Countenance, Covenant, Decalogue, Face, Fasting, Feasts, Fellowship, Firstborn, First Fruits, Forty, Glory, God, Harvest, Heredity, Iconoclasm, Idol, Idolatry, Intercession, Israel, Jealousy, Jebusites, Judgments, Labor, Law, Leaven (Yeast), Liberality, Marriage, Miracles, Miscegenation, Molding, Moses, Offerings, Passover, Pentecost, Prayer, Punishment, Quotations and Allusions, Rest, Revelation, Reverence, Sabbath, Sanitation, Self-Will, Sin, Sinai, Stones, Tabernacles, Feast of, Table, Temptation, Thankfulness, Transfiguration, Treaty, Truth, Veil, Watchfulness, Wicked (People), Word of God, Worship