Yoshua 23
1 Baada ya muda mrefu kupita, naye Mwenyezi Mungu akawa amewapa Israeli pumziko mbele ya adui zao wote waliowazunguka, Yoshua, wakati huo akiwa mzee na umri ukiwa umeendelea sana,
2 akawaita Israeli wote, wazee wao, viongozi, waamuzi na maafisa. Yoshua akawaambia: “Mimi ni mzee na umri wangu umeendelea sana.
3 Ninyi wenyewe mmeona kila kitu Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, alichowatendea mataifa haya yote kwa ajili yenu. Ilikuwa ni Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, aliyewapigania.
4 Kumbukeni jinsi nilivyowagawia kama urithi kwa makabila yenu yote nchi ya mataifa yaliyobaki, yaani mataifa niliyowashinda, kati ya Mto Yordani na Bahari kuu upande wa magharibi.
5 Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, mwenyewe atawaondoa watoke mbele yenu. Atawafukuza mbele yenu, nanyi mtamiliki nchi yao, kama vile Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, alivyowaahidi.
6 “Kuweni hodari sana, kuweni waangalifu kutii yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Torati ya Musa, pasipo kugeuka upande wa kuume au kushoto.
7 Msishirikiane na mataifa yaliyobakia kati yenu, wala msiombe kwa majina ya miungu yao au kuapa kwayo. Msiitumikie wala kuisujudia.
8 Bali mtashikamana kwa uthabiti na Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, kama vile mmefanya hadi sasa.
9 “Mwenyezi Mungu amewafukuza mbele yenu mataifa makubwa na yenye nguvu, hadi leo hakuna yeyote aliyeweza kusimama mbele yenu.
10 Mtu mmoja miongoni mwenu anafukuza watu elfu, kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anawapigania, kama alivyoahidi.
11 Kwa hiyo kuweni waangalifu sana kumpenda Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.
12 “Lakini ikiwa mtageuka na kushikamana na mabaki ya mataifa haya yaliyosalia kati yenu na kama mtaoana na kushirikiana nao,
13 basi mwe na hakika kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, hatawafukuza tena mataifa hayo mbele yenu. Badala yake, watakuwa tanzi na mitego kwenu, mijeledi migongoni mwenu, na miiba machoni mwenu, hata mwangamie kutoka nchi hii nzuri, ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, amewapa.
14 “Sasa mimi ninakaribia kwenda katika njia ya watu wote wa dunia. Mnajua kwa mioyo yenu na roho zenu kwamba hakuna ahadi zozote njema Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, alizowaahidia, ambazo hazikutimia. Kila ahadi imetimizwa, hakuna hata moja ambayo haikutimia.
15 Lakini kama vile kila ahadi njema ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, imekuwa kweli, vivyo hivyo Mwenyezi Mungu ataleta maovu yote kama alivyoonya, hadi awe amewaangamiza kutoka nchi hii nzuri aliyowapa.
16 Mkilivunja agano la Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ambalo aliwaamuru ninyi, mkaenda na kuitumikia miungu mingine na kuisujudia, hasira ya Mwenyezi Mungu itawaka dhidi yenu, basi nanyi mtaangamia kutoka nchi nzuri aliyowapa ninyi.”
Cross-references
108
- 1Jos 13:1, Jos 21:44, Jos 11:23, Jos 22:4, Psa 46:9, Gen 25:8, Deu 31:2
- 2Jos 24:1, 1Ch 28:1, Deu 31:28, Act 20:17–35
- 3Exo 14:14, Jos 10:42, Jos 10:14, Deu 4:9, Mal 1:5, Psa 44:1–3, Deu 20:4
- 4Jos 13:6–7, Jos 13:2, Jos 18:10
- 5Exo 34:11, Deu 11:23, Jos 13:6, Exo 33:2, Exo 23:30–31, Jos 23:12–13, Num 33:52–53
- 6Deu 5:32, Deu 28:14, Heb 12:4, Deu 17:20, Jos 1:7–9, Eph 6:10–19, Deu 12:32, Pro 4:26–27
- 7Exo 23:13, Psa 16:4, Jer 5:7, Deu 7:2–3, Jos 23:12, Exo 23:33, 2Co 6:14–17, 1Co 15:33
- 8Deu 10:20, Jos 22:5, Deu 13:4, Act 11:23, Deu 11:22, Deu 4:4
- 9Jos 1:5, Deu 11:23, Jos 23:5, Exo 23:30, Jos 21:43–44, Jos 15:14, Jos 1:8–9, Deu 7:24
- 10Deu 32:30, Lev 26:8, Deu 3:22, Exo 14:14, Psa 35:1, Deu 20:4, Rom 8:31, Psa 46:7
- 11Jos 22:5, Deu 6:5–12, Jud 1:20–21, Rom 8:28, Pro 4:23, 1Co 16:22, Exo 20:6, 1Co 8:3
- 12Deu 7:3, Ezk 18:24, Zep 1:6, 2Pe 2:18–22, Gen 2:24, Psa 106:34–35, Ezr 9:1–2, 1Ki 11:2
- 13Deu 7:16, Num 33:55, Exo 23:33, Jdg 2:2–3, Luk 21:24, Psa 106:35–39, 2Ki 17:22–23, Psa 69:22
- 14Luk 21:33, 1Ki 2:2, Lev 26:3–13, Ecc 9:10, Jos 21:43–45, Num 23:19, Deu 28:1–14, 1Sa 3:19
- 15Deu 28:15–68, Lev 26:14–46, Jdg 6:1, 1Th 2:16, Jdg 4:1–2, 2Ch 36:16–17, Jdg 10:6–7, Jdg 3:8
- 162Ki 24:20, Deu 4:25–26
Topics in this chapter
20
Anger, Company, Cowardice, Death, Decision, Duty, Fear, Fellowship, God, Government, Israel, Joshua, Love, Mediterranean Sea, Miscegenation, Obedience, Panic, Perfection, Trap, Watchfulness