Hosea 7
1 kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wezi huvunja nyumba, maharamia hunyang’anya barabarani,
2 lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.
3 “Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.
4 Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambalo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.
5 Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.
6 Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.
7 Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.
8 “Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.
9 Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.
10 Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wake, wala kumtafuta.
11 “Efraimu ni kama hua, hudanganywa kwa urahisi na hana akili: mara anaita Misri, mara anageukia Ashuru.
12 Watakapoenda, nitatupa wavu wangu juu yao; nitawavuta chini waanguke kama ndege wa angani. Nitakaposikia wakikusanyika pamoja, nitawanasa.
13 Ole wao, kwa sababu wamepotoka kutoka kwangu! Maangamizi ni yao kwa sababu wameniasi! Ninatamani kuwakomboa, lakini wanasema uongo dhidi yangu.
14 Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao, bali wanaomboleza vitandani mwao. Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya, lakini hugeukia mbali nami.
15 Niliwafundisha na kuwatia nguvu, lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana, wako kama upinde wenye kasoro. Viongozi wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya maneno yao ya jeuri. Kwa ajili ya hili watadhihakiwa katika nchi ya Misri.
Cross-references
126
- 1Hos 7:13, Hos 6:4, Mic 7:3–7, Hos 4:2, Mat 23:37, Luk 19:42, Jer 9:2–6, Luk 13:34
- 2Luk 12:2, Amo 8:7, Psa 90:8, Jer 14:10, Jer 2:19, Psa 9:16, Jer 32:19, 1Co 4:5
- 3Rom 1:32, Mic 7:3, Jer 28:1–4, Jer 5:31, 1Jn 4:5, Hos 4:2, 1Ki 22:6, Amo 7:10–13
- 4Jer 9:2, Jas 4:4, Jer 5:7–8, Hos 7:6–7, Hos 4:2, Hos 4:12
- 51Pe 4:3–4, Gen 40:20, Eph 5:18, Psa 1:1, Psa 69:12, Isa 28:1, Dan 5:23, Isa 28:7–8
- 6Psa 10:8–9, Mic 2:1, Hos 7:7, Hos 7:4, 1Sa 19:11–15, Pro 4:16, 2Sa 13:28–29, Psa 21:9
- 72Ki 15:30, 2Ki 15:14, 2Ki 15:25, 2Ki 15:10, Isa 64:7, Hos 7:10, Job 36:13, Hos 8:4
- 8Psa 106:35, Neh 13:23–25, Ezr 9:12, Ezr 9:1, Mal 2:11, 1Ki 18:21, Hos 5:7, Hos 5:13
- 9Hos 8:7, Isa 42:22–25, Isa 1:7, 2Ki 13:22, Pro 23:35, 2Ki 13:3–7, Isa 57:1, 2Ki 15:19
- 10Hos 5:5, Isa 9:13, Psa 53:2, Amo 4:6–13, Jer 35:15–17, Jer 8:5–6, Hos 6:1, Psa 10:4
- 11Hos 12:1, Hos 5:13, Hos 11:11, Jer 2:18, Hos 4:11, Pro 6:32, Hos 9:3, Ezk 23:4–8
- 12Ezk 12:13, Deu 28:15–68, Deu 29:22–28, Ezk 32:3, Ezk 17:20, Ecc 9:12, Jer 44:4, Job 19:6
- 13Hos 9:12, Lam 5:16, Mat 23:13–29, Hos 11:12, Hos 7:1, Jon 1:3, Mic 6:4, Mat 23:37
- 14Jas 4:3, Job 35:9–10, Jer 3:10, Psa 78:34–37, Amo 2:8, Zec 7:5, Isa 29:13, Php 3:19
- 15Nam 1:9, Psa 94:12, Job 5:17, 2Ki 14:25–27, Psa 106:43–45, Act 4:25, 2Co 10:5, Heb 12:5
- 16Psa 78:57, Hos 9:3, Psa 73:9, Ezk 23:32, Mat 12:36, Psa 12:4, Hos 9:6, Jer 18:18
Topics in this chapter
35
Adultery, Afflictions and Adversities, Anger, Baker, Blasphemy, Blindness, Bread, Character, Chastisement, Company, Confidence, Cooking, Dough, Drunkenness, False Confidence, Furnace, Godlessness, Hypocrisy, Impenitence, Infidelity, Ingratitude, King, Leaven (Yeast), Nation, Net, Oven, Prayerlessness, Pride, Robbers, Rulers, Scoffing, Sin, Temptation, Wicked (People), Wine