Sefania 1
1 Neno la Mwenyezi Mungu lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:
2 Mwenyezi Mungu asema, “Nitafagia kila kitu kutoka uso wa dunia.
3 Nitafagilia mbali watu na wanyama; nitafagilia mbali ndege wa angani na samaki wa baharini. Wafanyao maovu watapata tu kokoto, nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,” asema Mwenyezi Mungu.
4 “Nitaiadhibu Yuda na wote wanaoishi Yerusalemu. Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali kila mabaki ya Baali, majina ya wapagani na makuhani waabuduo sanamu:
5 wale ambao husujudu juu ya mapaa kuabudu jeshi la vitu vya angani, wale ambao husujudu na kuapa kwa Mwenyezi Mungu na ambao pia huapa kwa Malkamu,
6 wale wanaoacha kumfuata Mwenyezi Mungu, wala hawamtafuti Mwenyezi Mungu wala kutaka shauri lake.
7 Nyamazeni mbele za Bwana Mungu Mwenyezi, kwa maana siku ya Mwenyezi Mungu iko karibu. Mwenyezi Mungu ameandaa dhabihu, amewaweka wakfu wale aliowaalika.
8 Katika siku ya dhabihu ya Mwenyezi Mungu nitawaadhibu wakuu na wana wa mfalme na wale wote wanaovaa nguo za kigeni.
9 Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao hukwepa kukanyaga kizingiti, ambao hujaza hekalu la miungu yao kwa dhuluma na udanganyifu.”
10 Mwenyezi Mungu asema, “Katika siku hiyo kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki, maombolezo kutoka mtaa wa pili, na mshindo mkubwa kutoka vilimani.
11 Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni; wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa, wote ambao wanafanya biashara ya fedha wataangamizwa.
12 Wakati huo nitaupekua mji wa Yerusalemu kwa taa, na kuwaadhibu wale ambao wanakaa katika hali ya kuridhika, ambao ni kama divai iliyobaki kwenye machicha, ambao hudhani, ‘Mwenyezi Mungu hatafanya lolote, jema au baya.’
13 Utajiri wao utatekwa nyara, nyumba zao zitabomolewa. Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani yake; watapanda mizabibu lakini hawatakunywa divai yake.
14 “Siku kubwa ya Mwenyezi Mungu iko karibu: iko karibu na inakuja haraka. Sikilizeni! Kilio katika siku ya Mwenyezi Mungu kitakuwa chungu. Shujaa atapiga ukelele wa vita huko.
15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, siku ya fadhaa na dhiki, siku ya uharibifu na ukiwa, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene,
16 siku ya tarumbeta na kelele za vita dhidi ya miji yenye ngome, na dhidi ya minara mirefu.
17 Nitawaletea watu dhiki, nao watatembea kama vipofu, kwa sababu wametenda dhambi dhidi ya Mwenyezi Mungu. Damu yao itamwagwa kama vumbi na matumbo yao kama kinyesi.
18 Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Katika moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, kwa maana ghafula ataleta mwisho wa wote wanaoishi duniani.”
Cross-references
143
- 1Jer 1:2, 2Ch 34:1–33, 2Pe 1:19, Hos 1:1, 2Ki 22:1–20, Ezk 1:3, Jer 25:3, 2Ti 3:16
- 2Mic 7:13, 2Ki 22:16–17, Jer 36:29, Ezk 33:27–29, Jer 34:22, Gen 6:7, Jer 6:8–9, 2Ch 36:21
- 3Hos 4:3, Ezk 7:19, Isa 27:9, Jer 12:4, Ezk 14:13–21, Mat 23:39, Rev 2:14, Ezk 15:6–8
- 4Hos 10:5, Mic 5:13, 2Ki 23:4–5, 2Ch 34:4, 2Ki 21:13, Isa 14:26–27, Jer 6:12, Exo 15:12
- 52Ki 17:33, Jer 19:13, 1Ki 11:33, 2Ki 17:41, 2Ki 23:12, 1Ki 18:21, Hos 4:15, Mat 6:24
- 6Isa 1:4, Jer 2:13, Jer 15:6, Jer 2:17, Hos 11:7, Jer 3:10, Ezk 3:20, Isa 9:13
- 7Hab 2:20, Zec 2:13, Zep 1:14, Isa 34:6, Jer 46:10, Isa 13:6, Mat 22:4, Jol 2:31
- 8Isa 24:21, Jer 22:11–19, Isa 39:7, Isa 3:18–24, Jer 39:6–7, Jer 22:24–30, 2Ki 25:19–21, 2Ki 23:30–34
- 91Sa 5:5, Amo 3:10, 2Ki 5:20–27, 1Sa 2:15–16, Neh 5:15, Pro 29:12, Act 16:19
- 102Ch 33:14, Amo 8:3, 2Ki 22:14, Neh 3:3, Jer 4:19–21, Jer 4:31, 2Ch 3:1, Zep 1:15
- 11Jas 5:1, Ezk 21:12, Jer 25:34, Hos 12:7–8, Zec 11:2–3, Jol 1:13, Hos 9:6, Jhn 2:16
- 12Amo 6:1, Jer 48:11, Ezk 8:12, Ezk 9:9, Psa 94:7, Jer 16:16–17, Mal 3:14–15, Amo 9:1–3
- 13Amo 5:11, Mic 6:15, Deu 28:30, Jer 9:19, Jer 15:13, Ezk 7:21, Deu 28:39, Jer 4:20
- 14Ezk 30:3, Mal 4:5, Zep 1:7, 1Th 4:16, Jol 2:11, Ezk 7:12, Isa 15:4, Isa 33:7
- 15Jol 2:2, Isa 22:5, Rev 6:17, Amo 5:18–20, Jer 30:7, Jol 2:11, Zep 2:2, Job 3:4–8
- 16Isa 2:12–15, Amo 3:6, Isa 32:14, Hos 8:1, Jer 4:19–20, Isa 59:10, Hos 5:8, Psa 48:12–13
- 17Psa 83:10, Rev 3:17, Jer 2:17, Mic 7:13, 2Pe 1:9, Mat 15:14, Jer 10:18, 1Jn 2:11
- 18Zep 3:8, Ezk 7:19, Pro 11:4, Zep 1:2–3, Zep 1:11, Jer 9:11, Mat 16:26, Zep 1:15
Topics in this chapter
39
Amariah, Amon, Apostasy, Backsliders, Blasphemy, Chemarim, Colors, Confidence, Cushi, Day, Dishonesty, Dress, Fear, Fish Gate, Gedaliah, Hizkiah, House, Idolatry, Infidelity, Israel, Prophecies Concerning, Jealousy, Lamp, Lees, Maktesh, Malcham, Prayerlessness, Punishment, Rich, the, Rulers, Sacrifices, Servant, Skepticism, Stars, Stumbling, Symbols and Similitudes, Trumpet, War, Wicked (People), Zephaniah