Isaya 21
1 Neno la unabii kuhusu Jangwa kando ya Bahari: Kama upepo wa kisulisuli unaopita katika nchi hadi kusini, mshambuliaji anakuja kutoka jangwani, kutoka nchi inayotisha.
2 Nimeoneshwa maono ya kutisha: Msaliti anasaliti, mteka nyara anateka nyara. Elamu, shambulia! Umedi, zingira kwa jeshi! Nitakomesha huzuni zote alizosababisha.
3 Kwa sababu hii, mwili wangu umeteswa na maumivu, maumivu makali ya ghafula yamenishika, kama yale ya mwanamke mwenye uchungu wa kuzaa. Nimeduwazwa na lile ninalolisikia, nimeshangazwa na lile ninaloliona.
4 Moyo wangu unababaika, woga unanifanya nitetemeke, gizagiza la jioni nililolitamani sana, limekuwa hofu kuu kwangu.
5 Wanaandaa meza, wanatandaza mazulia, wanakula, wanakunywa! Amkeni, enyi maafisa, zitieni ngao mafuta!
6 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Nenda, weka mlinzi, na atoe taarifa ya kile anachokiona.
7 Anapoona magari ya vita pamoja na kundi la farasi, wapanda punda au wapanda ngamia, na awe macho, awe macho kikamilifu.”
8 Naye mlinzi alipaza sauti, “Mchana baada ya mchana, bwana wangu, ninasimama katika mnara wa ulinzi, kila usiku ninakaa mahali pangu nilipoamriwa.
9 Tazama, yuaja mtu anayepanda gari la vita pamoja na kundi la farasi. Naye anajibu: ‘Babeli umeanguka, umeanguka! Vinyago vyote vya miungu yake vimelala chini vikiwa vimevunjwa!’ ”
10 Ee watu wangu, mliopondwa kwenye sakafu ya kupuria, ninawaambia kile nilichokisikia kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, kutoka kwa Mungu wa Israeli.
11 Neno la unabii kuhusu Duma: Mtu fulani ananiita kutoka Seiri, “Mlinzi, usiku utaisha lini? Mlinzi, usiku utaisha lini?”
12 Mlinzi anajibu, “Asubuhi inakuja, lakini pia usiku. Ukitaka kuuliza, basi uliza; na urudi mara tena.”
13 Neno la unabii kuhusu Arabia: Enyi misafara ya Wadedani, mnaopiga kambi katika vichaka vya Arabia,
14 leteni maji kwa wenye kiu, ninyi mnaoishi Tema, leteni chakula kwa ajili ya wakimbizi.
15 Wanaukimbia upanga, upanga uliochomolewa alani, kutoka upinde uliopindwa, na kutoka kwa joto la vita.
16 Hili ndilo Bwana analoniambia: “Katika muda wa mwaka mmoja, kama vile mtumishi aliyefungwa na mkataba angeihesabu, majivuno yote ya Kedari yatafikia mwisho.
17 Wanaume wavutao pinde walionusurika, mashujaa wa Kedari, watakuwa wachache.” Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, amesema.
Cross-references
123
- 1Isa 14:23, Jer 51:42, Isa 13:1, Zec 9:14, Isa 17:1, Isa 13:20–22, Dan 11:40, Isa 13:4–5
- 2Jer 49:34, Isa 33:1, Isa 24:16, Psa 60:3, Dan 5:28, Rev 13:10, Jer 51:48–49, Jer 51:53
- 3Isa 13:8, Isa 26:17, Psa 48:6, Mic 4:9–10, 1Th 5:3, Jer 48:41, Isa 16:11, Hab 3:16
- 4Luk 21:34–36, Jer 51:57, 2Sa 13:28–29, 1Sa 25:36–38, Jer 51:39, Isa 5:11–14, Nam 1:10, Est 7:6–10
- 5Jer 51:39, Jer 51:57, Jer 51:11, Dan 5:1–5, Isa 45:1–3, 1Co 15:32, Isa 13:17–18, Isa 13:2
- 6Ezk 33:2–7, Hab 2:1–2, Ezk 3:17, 2Ki 9:17–20, Isa 62:6, Jer 51:12–13
- 7Isa 21:9, Isa 37:24, Heb 2:1
- 8Hab 2:1–2, Isa 5:29, Jer 25:38, Isa 56:10, 1Pe 5:8, Psa 127:1, Jer 49:19, Psa 63:6
- 9Rev 18:2, Rev 14:8, Jer 51:8, Jer 51:44, Isa 13:19, Isa 46:1–2, Jer 51:27, Jer 50:42
- 10Jer 51:33, Mic 4:13, Mat 3:12, Ezk 3:17–19, Isa 41:15–16, 2Ki 13:7, Act 20:26–27, 1Ki 22:14
- 11Gen 25:14, Oba 1:1–16, Amo 1:6, Jol 3:19, Gen 32:3, Jer 49:7–22, Deu 2:5, Isa 34:1–17
- 12Act 17:30–32, Act 2:37–38, Ezk 14:1–6, Ezk 7:12, Ezk 7:10, Isa 55:7, Ezk 7:5–7, Ezk 18:30–32
- 13Jer 25:23–24, Ezk 27:15, 1Ch 1:32, Gen 25:3, 1Ki 10:15, Isa 13:1, Isa 13:20, 1Ch 1:9
- 14Job 6:19, Gen 25:15, Pro 25:21, Rom 12:20, 1Pe 4:9, Isa 16:3–4, 1Ch 1:30, Jdg 8:4–8
- 15Job 6:19–20, Isa 13:14
- 16Psa 120:5, Sng 1:5, Isa 16:14, Isa 60:7, Jer 49:28, Ezk 27:21, Gen 25:13, Isa 42:11
- 17Num 23:19, Zec 1:6, Mat 24:35, Isa 1:20, Psa 107:39, Isa 17:4–5, Isa 10:18–19, Jer 44:29