Isaya 19
1 Neno la unabii kuhusu Misri: Tazama, Mwenyezi Mungu amepanda juu ya wingu liendalo kwa haraka naye anakuja Misri. Sanamu za Misri zinatetemeka mbele yake, nayo mioyo ya Wamisri inayeyuka ndani yao.
2 “Nitamchochea Mmisri dhidi ya Mmisri, ndugu atapigana dhidi ya ndugu, jirani dhidi ya jirani, mji dhidi ya mji, ufalme dhidi ya ufalme.
3 Wamisri watakufa moyo, na nitaibatilisha mipango yao. Watatafuta ushauri kwa sanamu na kwa roho za waliokufa, kwa waaguzi na kwa wale waongeao na mizimu.
4 Nitawatia Wamisri mikononi mwa bwana mkatili na mfalme mkali atawatawala,” asema Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni.
5 Maji ya mito yatakauka, chini ya mto kutakauka kwa jua.
6 Mifereji itanuka; vijito vya Misri vitapungua na kukauka. Matete na nyasi vitanyauka,
7 pia mimea iliyo kando ya Mto Naili, pale mto unapomwaga maji baharini. Kila shamba lililopandwa kando ya Mto Naili litakauka, litapeperushwa na kutoweka kabisa.
8 Wavuvi watalia na kuomboleza, wote watupao ndoana katika Mto Naili, na watupao nyavu katika maji watadhoofika kwa majonzi.
9 Wale watu wafanyao kazi ya kitani kilichochambuliwa watakata tamaa, wafumaji wa kitani safi watavunjika moyo.
10 Wafanyao kazi ya kufuma nguo watahuzunishwa, nao vibarua wataugua moyoni.
11 Maafisa wa Soani ni wapumbavu kabisa, washauri wa Farao wenye busara wanatoa ushauri wa kijinga. Unawezaje kumwambia Farao, “Mimi ni mmoja wa watu wenye hekima, mwanafunzi wa wafalme wa zamani”?
12 Wako wapi sasa watu wako wenye hekima? Wao wakuoneshe na kukufahamisha ni nini Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni amepanga dhidi ya Misri.
13 Maafisa wa Soani wamekuwa wapumbavu, viongozi wa Memfisi wamedanganyika, walio mawe ya pembe ya taifa lake wameipotosha Misri.
14 Mwenyezi Mungu amewamwagia roho ya kizunguzungu; wanaifanya Misri iyumbayumbe katika yale yote inayoyafanya, kama vile mlevi ayumbayumbavyo katika kutapika kwake.
15 Misri haiwezi kufanya kitu chochote, cha kichwa wala cha mkia, cha tawi la mtende wala cha tete.
16 Katika siku ile Wamisri watakuwa kama wanawake. Watatetemeka kwa hofu mbele ya mkono wa Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni anaoinua dhidi yao.
17 Nayo nchi ya Yuda itawatia hofu Wamisri, kila mmoja atakayetajiwa Yuda ataingiwa na hofu, kwa sababu ya kile ambacho Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni anapanga dhidi yao.
18 Katika siku hiyo miji mitano ya Misri, itazungumza lugha ya Kanaani, na kuapa kumtii Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni. Mji mmoja utaitwa Mji wa Uharibifu.
19 Katika siku hiyo patakuwa na madhabahu ya Mwenyezi Mungu katikati ya Misri na mnara wa kumbukumbu kwa Mwenyezi Mungu kwenye mpaka wa Misri.
20 Itakuwa alama na ushahidi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni katika nchi ya Misri. Watakapomlilia Mwenyezi Mungu kwa sababu ya watesi wao, Mungu atawapelekea mwokozi na mtetezi, naye atawaokoa.
21 Hivyo Mwenyezi Mungu atajijulisha mwenyewe kwa Wamisri, nao katika siku hiyo watamkubali Mwenyezi Mungu. Wataabudu kwa kumtolea dhabihu na sadaka za nafaka, watamwekea Mwenyezi Mungu nadhiri na kuzitimiza.
22 Mwenyezi Mungu ataipiga Misri kwa tauni; atawapiga na kuwaponya. Watamgeukia Mwenyezi Mungu, naye atayasikia maombi yao na kuwaponya.
23 Katika siku hiyo kutakuwa na njia kuu kutoka Misri hadi Ashuru. Waashuru wataenda Misri, na Wamisri wataenda Ashuru. Wamisri na Waashuru wataabudu pamoja.
24 Katika siku hiyo Israeli itakuwa ya tatu, pamoja na Misri na Ashuru, nao watakuwa baraka kwa dunia.
25 Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni atawabariki, akisema, “Baraka iwe kwa Misri watu wangu, kwa Ashuru kazi ya mikono yangu, na kwa Israeli urithi wangu.”
Cross-references
172
- 1Exo 12:12, Rev 1:7, Ezk 30:13, Jol 3:19, Jos 2:11, Jer 51:44, Ezk 29:1–21, Isa 13:1
- 2Jdg 7:22, 1Sa 14:20, Mat 10:36, Ezk 38:21, Rev 17:12–17, Mat 12:25, Mat 10:21, 2Ch 20:22–23
- 3Isa 8:19, Dan 2:2, 1Ch 10:13, Isa 44:25, Pro 21:30, Job 5:12–13, Isa 14:27, Dan 4:6–7
- 4Isa 20:4, Ezk 29:19, Jer 46:26, Isa 19:2, 1Sa 23:7, Psa 31:8
- 5Jer 51:36, Ezk 30:12, Zec 14:18, Zec 10:11
- 6Isa 37:25, Exo 7:18, Exo 2:3, 2Ki 19:24, Job 8:11, Isa 15:6, Isa 18:2
- 7Jol 1:17–18, Isa 23:3, Jer 14:4, Ezk 19:13, Isa 32:20
- 8Hab 1:15, Ezk 47:10, Num 11:5, Exo 7:21
- 9Ezk 27:7, Pro 7:16, 1Ki 10:28
- 10Exo 8:5, Exo 7:19, Deu 11:10
- 11Num 13:22, Isa 30:4, Psa 78:43, Act 7:22, 1Ki 4:30, Gen 41:38–39, Psa 78:12, Jer 10:14
- 121Co 1:20, Isa 47:10–13, Rom 9:17, Isa 14:24, Isa 44:7, Isa 40:13–14, Job 11:6–7, Isa 5:21
- 13Ezk 30:13, Jer 2:16, Jer 46:19, Zec 10:4, Jer 46:14, Isa 19:11, Rom 1:22, 1Sa 14:38
- 142Th 2:11, 1Ki 22:20–23, Ezk 14:7–9, Job 12:25, Jer 25:27, Isa 47:10–11, Isa 29:9–10, Isa 19:2
- 15Isa 9:14–15, 1Th 4:11–12, Psa 128:2, Pro 14:23, Hab 3:17, Hag 1:11
- 16Nam 3:13, Jer 51:30, Isa 11:15, Jer 50:37, Jer 30:5–7, Zec 2:9, Isa 10:32, Isa 30:17
- 17Isa 14:24, Dan 4:35, Jer 43:8–13, Isa 36:1, Jer 25:19, Jer 25:27–31, Ezk 29:6–7, Isa 20:2–5
- 18Zep 3:9, Isa 19:21, Zec 2:11, Jer 12:16, Isa 11:11, Isa 45:23–24, Isa 19:19, Isa 2:11
- 19Gen 28:18, Jos 22:10, Exo 24:4, Jos 22:26, Gen 12:7, Zec 6:15, Isa 66:23, Heb 13:10
- 20Psa 50:15, Tit 2:13, Luk 2:11, Isa 45:21–22, Exo 3:7, Isa 37:36, Isa 19:4, Jos 24:26–27
- 21Mal 1:11, Isa 11:9, Hab 2:14, Psa 67:2, Isa 55:5, Isa 44:5, Zep 3:10, 1Ki 8:43
- 22Heb 12:11, Deu 32:39, Hos 14:1, Hos 5:15, Isa 45:14, Amo 4:6–12, Job 5:18, Hos 6:2
- 23Isa 11:16, Isa 27:13, Eph 2:18–22, Isa 40:3–5, Eph 3:6–8, Isa 35:8–10
- 24Isa 65:8, Gen 12:2, Isa 65:22, Deu 32:43, Isa 66:19–21, Isa 6:13, Isa 66:12, Zec 8:13
- 25Isa 29:23, Hos 2:23, Rom 9:24–25, Psa 115:15, Psa 138:8, Deu 32:9, Isa 61:9, Num 6:27