Hosea 8
1 “Wekeni tarumbeta midomoni mwenu! Tai yuko juu ya nyumba ya Mwenyezi Mungu kwa sababu watu wamevunja agano langu, wameasi dhidi ya sheria yangu.
2 Israeli ananililia, ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’
3 Lakini Israeli amekataa lile lililo jema, adui atamfuatia.
4 Wanaweka wafalme bila idhini yangu, wamechagua wakuu bila kibali changu. Kwa fedha zao na dhahabu wamejitengenezea sanamu kwa ajili ya maangamizi yao wenyewe.
5 Ee Samaria, tupilieni mbali sanamu yenu ya ndama! Hasira yangu inawaka dhidi yao. Watakuwa najisi hadi lini?
6 Zimetoka katika Israeli! Ndama huyu: ametengenezwa na fundi, si Mungu. Atavunjwa vipande vipande, yule ndama wa Samaria.
7 “Wanapanda upepo na kuvuna kisulisuli. Bua halina suke, halitatoa unga. Kama lingetoa nafaka, wageni wangeila yote.
8 Israeli amemezwa; sasa yupo miongoni mwa mataifa kama kitu kisicho na thamani.
9 Kwa kuwa wamepanda kwenda Ashuru kama punda-mwitu anayetangatanga peke yake. Efraimu amejiuza mwenyewe kwa wapenzi.
10 Ingawa wamejiuza wenyewe miongoni mwa mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wataanza kudhoofika chini ya uonevu wa mfalme mwenye nguvu.
11 “Ingawa Efraimu alijenga madhabahu nyingi kwa ajili ya sadaka za dhambi, hizi zimekuwa madhabahu za kufanyia dhambi.
12 Niliwaandikia mambo mengi yaliyohusu sheria yangu, lakini waliziangalia kama kitu kigeni.
13 Wanatoa dhabihu nilizopewa mimi nao wanakula hiyo nyama, lakini Mwenyezi Mungu hapendezwi nao. Sasa ataukumbuka uovu wao na kuadhibu dhambi zao: Watarudi Misri.
14 Israeli amemsahau Muumba wake na kujenga majumba ya kifalme, Yuda amejengea miji mingi ngome. Lakini nitatuma moto kwenye miji yao utakaoteketeza ngome zao.”
Cross-references
110
- 1Hos 6:7, Deu 28:49, Jer 4:13, Hos 5:8, Heb 8:8–13, Hab 1:8, 2Ki 18:27, Zec 9:14
- 2Mat 7:21, Tit 1:16, 2Ki 10:29, Jer 7:4, Isa 48:1–2, Psa 78:34–37, Hos 7:13–14, 1Jn 2:4
- 3Lam 3:66, Psa 81:10–11, Amo 1:11, Lev 26:36, Lam 4:19, Deu 28:25, 1Ti 5:12, Psa 36:3
- 4Hos 13:9–10, 2Ki 15:10–30, Hos 2:8, Jhn 10:14, 1Ki 12:16–20, Hos 13:2, 1Ki 16:31, 1Ki 12:28
- 5Hos 10:5, Jer 13:27, Pro 1:22, Act 7:41, 2Ki 17:21–23, 2Ki 17:16–18, Deu 32:22, Hos 8:6
- 6Hab 2:18, Psa 135:15–18, 2Ki 23:19, Psa 115:4–8, Isa 44:9–20, Jer 50:2, 2Ki 23:15, Act 19:26
- 7Pro 22:8, Job 4:8, Gal 6:7, Nam 1:3, Hos 10:12–13, Jdg 6:3–6, Hos 7:9, Jer 12:13
- 8Jer 22:28, Jer 51:34, 2Ti 2:20–21, Jer 48:38, 2Ki 18:11, Deu 28:25, Jer 50:17, Lev 26:33
- 9Jer 2:24, Hos 7:11, Hos 5:13, Ezk 16:33–34, Isa 30:6, 2Ki 15:19, Hos 2:5–7, Hos 2:10
- 10Ezk 16:37, Ezk 26:7, Hag 2:6, Jer 42:2, Ezk 23:22–26, Hos 10:10, Isa 10:8, 2Ki 14:26
- 11Hos 12:11, Deu 4:28, Hos 10:8, Hos 10:1–2, Jer 16:13, Isa 10:10–11
- 12Rom 7:12, Deu 4:6–8, Isa 30:9, Pro 22:20, 2Ki 17:15–16, Neh 9:13–14, Psa 119:18, Hos 4:6
- 13Hos 9:6, Hos 9:9, Amo 5:22, Amo 8:7, Hos 9:3–4, Exo 20:3, Isa 1:11, Hos 11:5
- 14Deu 32:18, Jer 17:27, Isa 17:10, Amo 2:5, Hos 13:6, Psa 106:21, Jer 2:32, Amo 1:10