Mathayo 26
1 Isa alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
2 “Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
3 Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
4 Wakapanga kumkamata Isa kwa siri na kumuua.
5 Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
6 Isa alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma.
7 Naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa. Akayamimina kichwani mwa Isa alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
8 Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
9 Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
10 Isa, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
11 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
12 Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
13 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
14 Kisha mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alienda kwa viongozi wa makuhani
15 na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Isa mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
16 Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Isa.
17 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimjia Isa wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
18 Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini, mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: Saa yangu imekaribia. Nitaiadhimisha Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’ ”
19 Hivyo wanafunzi wakafanya vile Isa alivyokuwa amewaelekeza, nao wakaandaa Pasaka.
20 Ilipofika jioni, Isa alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
21 Nao walipokuwa wakila, Isa akasema, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
22 Wakahuzunika sana, wakaanza kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
23 Isa akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami ndiye atakayenisaliti.
24 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu. Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa!”
25 Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, akasema, “Je, ni mimi Mwalimu?” Isa akajibu, “Naam, wewe mwenyewe umesema.”
26 Walipokuwa wanakula, Isa akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
27 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, “Nyweni nyote katika kikombe hiki.
28 Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
29 Lakini ninawaambia, tangu sasa sitakunywa tena katika uzao huu wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”
30 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
31 Kisha Isa akawaambia, “Usiku huu, ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “ ‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa hilo kundi watatawanyika.’
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
33 Petro akajibu, “Hata kama wote watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.”
34 Isa akamjibu, “Amin, nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
35 Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wanafunzi wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36 Kisha Isa akaenda pamoja na wanafunzi wake hadi kwenye bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa, nami niende kule nikaombe.”
37 Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
38 Kisha Isa akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja nami.”
39 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
40 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
41 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
42 Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
43 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
44 Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
45 Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
46 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
47 Alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, akafika. Alikuwa amefuatana na umati mkubwa wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
48 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
49 Mara Yuda akamjia Isa na kumsalimu, “Salamu, Mwalimu!” Akambusu.
50 Isa akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Isa.
51 Ghafula mmoja wa wale waliokuwa na Isa alipoona hivyo, akaushika upanga wake, akauchomoa na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
52 Ndipo Isa akamwambia, “Rudisha upanga wako alani mwake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga.
53 Je, unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54 Lakini je, yale Maandiko yanayotabiri kwamba ni lazima itendeke hivi yatatimiaje?”
55 Wakati huo, Isa akaambia wale umati wa watu, “Je, mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang’anyi? Siku kwa siku niliketi Hekaluni nikifundisha, mbona hamkunikamata?
56 Lakini haya yote yametukia ili maandiko ya manabii yapate kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
57 Wale waliomkamata Isa wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa Torati pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.
58 Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.
59 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Isa ili wapate kumuua.
60 Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo
61 na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’ ”
62 Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Isa, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
63 Lakini Isa akakaa kimya. Ndipo kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai. Tuambie kama wewe ndiwe Al-Masihi, Mwana wa Mungu.”
64 Isa akajibu, “Wewe umenena. Lakini ninawaambia nyote: Siku za baadaye, mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
65 Ndipo kuhani mkuu akararua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia alivyokufuru.
66 Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
67 Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
68 na kusema, “Tutabirie, wewe Al-Masihi! Ni nani aliyekupiga?”
69 Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mjakazi mmoja akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Isa wa Galilaya.”
70 Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
71 Alipotoka nje kufika kwenye lango, mjakazi mwingine alimwona, akawaambia watu waliokuwako, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Isa Al-Nasiri.”
72 Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
73 Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
74 Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
75 Ndipo Petro akakumbuka lile neno Isa alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
Cross-references
528
- 1Mat 7:28, Mat 19:1
- 2Mrk 14:1–2, Luk 22:1–2, Mat 20:18–19, Jhn 13:1–2, Luk 24:6–7, Jhn 18:2, Mat 17:22, Mat 26:24–25
- 3Jhn 18:24, Jhn 11:47–53, Mrk 14:54, Act 4:5–6, Act 4:25–28, Jhn 11:57, Jhn 18:28, Mat 21:45–46
- 4Mat 12:14, Act 13:10, Psa 2:2, Act 7:19, Gen 3:1, Mat 23:33, 2Co 11:3
- 5Mat 27:24, Mat 21:26, Mat 14:5, Mrk 14:2, Isa 46:10, Mrk 14:27, Mrk 14:12, Pro 21:30
- 6Mrk 14:3–9, Jhn 12:1–8, Luk 7:37–39, Jhn 11:1–2, Mat 21:17, Mrk 11:12
- 7Jhn 12:2–3, Luk 7:46, Luk 7:37–38, Ecc 9:8, Isa 57:9, Psa 133:2, Sng 1:3, Exo 30:23–33
- 8Jhn 12:4–6, Mrk 14:4, Exo 5:17, Hag 1:2–4, 1Sa 17:28–29, Amo 8:5, Ecc 4:4, Mal 1:7–10
- 9Mrk 14:5, Jhn 12:5–6, 1Sa 15:9, 1Sa 15:21, 2Ki 5:20, Jos 7:20–21, 2Pe 2:15
- 10Tit 3:8, Heb 13:21, 1Ti 3:1, Tit 1:16, 2Ti 2:21, 1Ti 5:10, Tit 3:14, Tit 3:1
- 11Deu 15:11, Mrk 14:7, Jhn 12:8, Jhn 16:28, Jhn 14:19, Jhn 13:33, Jhn 16:5, Act 3:21
- 12Jhn 12:7, Mrk 14:8, 2Ch 16:14, Mrk 16:1, Luk 23:56–24:1, Jhn 19:39–40
- 13Mrk 14:9, Mat 24:14, Psa 112:6, Isa 52:9, 1Sa 2:30, Psa 98:2–3, Mrk 16:15, Col 1:6
- 14Luk 22:3–6, Mat 10:4, Mrk 14:10–11, Jhn 6:70–71, Mat 26:47, Jhn 13:30, Act 1:16, Jhn 13:2
- 15Zec 11:12–13, Gen 37:26–28, Exo 21:32, 1Ti 6:9–10, 2Pe 2:3, Jdg 16:5, 1Ti 3:3, Jdg 18:19–20
- 16Mrk 14:11, Luk 22:6
- 17Luk 22:7–13, Exo 12:18–20, Mrk 14:12–16, Exo 12:6, Exo 13:6–8, Mat 3:15, Mat 26:19, Mat 17:24–25
- 18Mrk 14:13–16, Jhn 7:6, Jhn 13:1, Jhn 17:1, Jhn 7:8, Jhn 7:30, Luk 22:10–13, Luk 22:53
- 19Jhn 15:14, Mat 21:6, Jhn 2:5, Exo 12:4–8, 2Ch 35:10–11
- 20Mrk 14:17–21, Jhn 13:21, Exo 12:11, Sng 1:12, Luk 22:14–16
- 21Jhn 13:21, Jhn 6:70–71, Heb 4:13, Psa 55:12–14, Rev 2:23, Mat 26:2, Mat 26:14–16, Luk 22:21–23
- 22Luk 22:23, Jhn 13:22–25, Mrk 14:19–20, Jhn 21:17
- 23Jhn 13:18, Psa 41:9, Jhn 13:26–28, Luk 22:21
- 24Luk 24:46, Act 26:22–23, Mat 18:7, Dan 9:26, 1Co 15:3, Zec 12:10, Mat 26:54, Jhn 17:12
- 25Mat 26:64, Mat 27:11, Luk 22:70, Jhn 18:37, 2Ki 5:25, Mat 26:49, Pro 30:20, Mat 23:7
- 261Co 11:23–29, Luk 22:18–20, 1Co 10:16–17, Jhn 6:33–35, 1Co 10:4, Mrk 14:22–25, Act 20:7, Jhn 6:47–58
- 271Co 10:16, Isa 25:6, Psa 116:13, Sng 5:1, Isa 55:1, Luk 22:20, 1Co 11:28, Sng 7:9
- 28Heb 10:4–14, Heb 9:14–22, Lev 17:11, Mat 20:28, Exo 24:7–8, Rev 7:14, 1Jn 2:2, 1Co 11:25
- 29Heb 12:2, Rev 7:17, Mrk 14:25, Luk 22:29–30, Psa 40:3, Luk 22:15–18, Act 10:41, Jhn 17:13
- 30Mrk 14:26–31, Eph 5:19–20, Luk 22:39, Mat 21:1, Luk 21:37, Col 3:16–17, Jhn 14:31, Jhn 18:1–4
- 31Zec 13:7, Mrk 14:27–28, Jhn 16:32, Ezk 34:5–6, Psa 69:20, Psa 38:11, Mat 24:9–10, Lam 1:19
- 32Mat 28:10, Luk 18:33–34, Mat 28:16, Mat 20:19, Mat 16:21, Mrk 14:28, Mat 27:63–64, Mrk 16:7
- 33Luk 22:33, 1Pe 5:5–6, Pro 28:25–26, Jhn 13:36–38, Psa 17:5, Rom 12:10, Php 2:3, Mrk 14:29
- 34Jhn 13:38, Luk 22:34, Mat 26:75, Mrk 14:30–31
- 35Jhn 13:37, Rom 11:20, Pro 28:14, 1Co 10:12, Exo 19:8, Pro 29:23, Php 2:12, 1Pe 1:17
- 36Mrk 14:32–42, Luk 22:39–46, Mat 26:42, Mat 26:39, Heb 5:7, Psa 69:13–15, Psa 22:1–2, Psa 69:1–3
- 37Mat 4:21, Mat 17:1, Mrk 5:37, Mrk 14:33–34, Luk 22:44, Mat 4:18, Jhn 12:27, Mat 20:20
- 38Jhn 12:27, 1Pe 3:18, 1Pe 2:24, Mat 26:40–41, 1Pe 4:7, Isa 53:10, Gal 3:13, Rom 8:32
- 39Jhn 6:38, Php 2:8, Mat 26:42, Luk 22:41–42, Jhn 5:30, Heb 5:7, Mrk 14:35–36, Jhn 12:27–28
- 40Mrk 14:37, Luk 22:45, Mat 26:43, Luk 9:32, Mat 25:5, Mat 26:35, Mat 26:38, Jdg 9:33
- 41Luk 22:46, Mrk 14:38, Eph 6:18, Mat 6:13, Gal 5:16–17, Rev 16:15, Luk 21:36, 1Co 16:13
- 42Mat 26:39, Mrk 14:39–40, Heb 4:15, Psa 88:1–2, Heb 5:7–8, Psa 69:17–18, Psa 22:1–2, Psa 69:1–3
- 43Luk 9:32, Pro 23:34, Jon 1:6, Act 20:9, Rom 13:1, 1Th 5:6–8
- 442Co 12:8, Luk 18:1, Dan 9:17–19, Mat 6:7
- 45Jhn 13:1, Jhn 17:1, Luk 22:53, Jhn 12:27, Mrk 14:41–42, Mat 26:18, Mat 26:2, Mat 26:14–15
- 46Jhn 14:31, Luk 9:51, Act 21:13, Luk 12:50, 1Sa 17:48, Luk 22:15
- 47Mat 26:55, Act 1:16, Mat 26:14, Luk 22:47–53, Mrk 14:43–50, Jhn 18:1–11
- 48Mrk 14:44, 2Sa 20:9–10, Psa 28:3, Psa 55:20–21, 2Sa 3:27
- 49Mat 26:25, 1Th 5:26, Luk 7:45, 2Sa 20:9, Mrk 15:18, Pro 27:6, 1Sa 10:1, Jhn 19:3
- 50Mat 20:13, Mat 22:12, 2Sa 16:17, Luk 22:48, Psa 41:9, Psa 55:13–14
- 512Co 10:4, Jhn 18:36, Mrk 14:47, Luk 22:49–51, Mat 26:35, Luk 22:36–38, Jhn 18:10–11, Luk 9:55
- 52Rev 13:10, Gen 9:6, Rom 12:19, 1Pe 2:21–23, 1Pe 3:9, Rev 16:6, Mat 23:34–36, Ezk 35:5–6
- 532Ki 6:17, Mat 4:11, Luk 8:30, Dan 7:10, 2Th 1:7, Mat 25:31, Jud 1:14, Mat 10:1–2
- 54Zec 13:7, Mat 26:24, Luk 24:25–26, Act 1:16, Jhn 10:35, Isa 53:1–12, Psa 22:1–31, Luk 24:44–46
- 55Jhn 8:2, Mrk 12:35, Jhn 18:20–21, Jhn 7:14, Jhn 7:28, Luk 21:37–38, Mrk 14:48–50, Luk 22:52–53
- 56Zec 13:7, Jhn 16:32, Mrk 14:50–52, 2Ti 4:16, Mat 26:31, Mat 26:54, Act 1:16, Jhn 18:15–16
- 57Mat 26:3, Luk 22:54–55, Jhn 11:49, Jhn 18:19–24, Psa 56:5–6, Mrk 14:53–65, Jhn 18:12–14
- 58Jhn 7:32, Jhn 18:15–16, Jhn 18:25, Jhn 7:45
- 59Act 6:11–13, Deu 19:16–21, Mrk 14:55–56, Psa 94:20–21, Mat 5:22, 1Ki 21:8–13, Act 24:1–13, Psa 27:12
- 60Deu 19:15, Psa 35:11, Psa 27:12, Mrk 14:57–59, Dan 6:4–5, Tit 2:8, 1Pe 3:16
- 61Jhn 2:19–21, Mat 27:40, Mrk 15:29, Psa 22:6–7, Isa 49:7, Act 18:13, Isa 53:3, Gen 19:9
- 62Jhn 19:9–11, Jhn 18:19–24, Luk 23:9, Mat 27:12–14, Mrk 14:60
- 63Lev 5:1, Isa 53:7, Mat 16:16, Mat 27:12, Jhn 6:69, 1Sa 14:26, Jhn 1:34, Mat 27:54
- 64Dan 7:13, Mrk 14:62, Psa 110:1, Heb 1:3, Rev 1:7, Luk 21:27, Mat 24:30, Mat 16:27
- 65Jhn 10:33, Mrk 14:63–64, Jhn 10:36, Num 14:6, Mat 9:3, Jer 36:24, Lev 21:20, 2Ki 18:37–19:3
- 66Jhn 19:7, Act 7:52, Jas 5:6, Act 13:27–28, Lev 24:11–16
- 67Isa 50:6, Isa 53:3, Jhn 18:22, Mat 27:30, Mat 5:39, Mrk 14:65, Lam 3:30, Heb 12:2
- 68Luk 22:63–65, Mrk 14:65, 1Pe 2:4–8, Mat 27:28–29, Jhn 19:14–15, Jhn 19:2–3, Gen 37:19–20, Mrk 15:18–19
- 69Mat 26:71, 1Ki 19:13, Jhn 18:16–18, Act 5:37, Jhn 7:52, Mrk 14:66–72, 1Ki 19:9, Psa 1:1
- 701Co 10:12, Rev 21:8, Jer 17:9, Mat 26:58, Isa 57:11, Pro 28:26, Mat 26:56, Mat 26:51
- 71Mrk 14:68–69, Luk 22:58, Jhn 18:25–27
- 72Act 5:3–4, Mat 5:34–36, Exo 20:7, Mat 26:74, Isa 48:1, Mal 3:5, Zec 8:17, Luk 22:34
- 73Jdg 12:6, Jhn 18:26–27, Luk 22:59–60, Neh 13:24
- 74Rev 3:19, Mat 10:28, 1Co 16:22, Mrk 14:71–72, Jhn 18:27, Act 23:12–14, 1Sa 14:24–28, Luk 22:60
- 75Mat 26:34, Rom 7:18–20, Jhn 13:38, Luk 22:31–34, Luk 22:61–62, Gal 6:1, Mat 27:3–5, 1Pe 1:5
Parallel passages
5
- The Anointing at BethanyMat 26:6–13, Mrk 14:3–9, Jhn 12:1–8
- The Last SupperMat 26:26–30, Mrk 14:22–26, Luk 22:14–23
- The Agony in GethsemaneMat 26:36–46, Mrk 14:32–42, Luk 22:39–46
- The Arrest of JesusMat 26:47–56, Mrk 14:43–52, Luk 22:47–53, Jhn 18:1–11
- Peter's DenialMat 26:69–75, Mrk 14:66–72, Luk 22:54–62, Jhn 18:15–27
Topics in this chapter
127
Accusation, False, Afflictions and Adversities, Alabaster, Angel (A Spirit), Anointing, Apostasy, Arrest, Assault and Battery, Atonement, Backsliders, Bethany, Betrayal, Blasphemy, Blood, Box, Bread, Bribery, Caiaphas, Chiding, Church, Cock Crowing, Confidence, Conscience, Conspiracy, Contingencies, Court, Covetousness, Cowardice, Craftiness, Cruelty, Cup, Curiosity, Dead (People), Eucharist (the Lord's Supper), False Confidence, Falsehood, False Teachers, Feasts, Fellowship, Food, Friends, Galilee, Gethsemane, God, Government, Homicide, Hypocrisy, Indecision, Indictments, James, Jesus, the Christ, John, Judas (Jude), Judge, Kiss, Language, Legion, Love, Lukewarmness, Malchus, Malice, Man, Mary, Master, Meekness, Millennium, Minister, Christian, Mocking, Month, Mourning, Oath, Obedience, Ointment, Olives, Mount of, Opinion, Public, Parsimony (Stinginess), Passover, Perjury, Persecution, Peter, Pleading, Poor, Praise, Prayer, Predestination, Presumption, Priest, Prisoners, Probation, Prophecy, Quotations and Allusions, Rabbi, Remorse, Rending, Repentance, Resignation, Rulers, Salutations, Scribe (S), Self-Control, Self-Examination, Sheep, Shepherd, Silver, Simon, Sin, Slander, Song, Sorrow, Spitting, Staves (Long Poles), Submission, Sword, Symbols and Similitudes, Temple, Temptation, Testament, Thankfulness, Traitor, Types, Verdict, Watchfulness, Weeping, Wicked (People), Will, Wine, Women