1 Samweli 12
1 Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
2 Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu hadi siku hii ya leo.
3 Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni dhidi yangu mbele za Mwenyezi Mungu na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Nimemdhulumu nani? Nimepokea rushwa kutoka kwa nani ili nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, nitawarudishia.”
4 Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutudhulumu. Hujapokea chochote kutoka mkono wa mtu yeyote.”
5 Samweli akawaambia, “Mwenyezi Mungu ni shahidi dhidi yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
6 Kisha Samweli akawaambia watu, “Mwenyezi Mungu ndiye alimchagua Musa na Haruni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
7 Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Mwenyezi Mungu wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Mwenyezi Mungu kwenu na kwa baba zenu.
8 “Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Mwenyezi Mungu awasaidie, naye Mwenyezi Mungu akawatuma Musa na Haruni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
9 “Lakini wakamsahau Mwenyezi Mungu, Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
10 Wakamlilia Mwenyezi Mungu na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Mwenyezi Mungu na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
11 Ndipo Mwenyezi Mungu akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
12 “Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, alikuwa mfalme wenu.
13 Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Mwenyezi Mungu amemweka mfalme juu yenu.
14 Mkimcha Mwenyezi Mungu, na kumtumikia na kumtii, nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayewatawala mkimfuata Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
15 Lakini kama hamkumtii Mwenyezi Mungu, nanyi mkaasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
16 “Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Mwenyezi Mungu anaenda kulifanya mbele ya macho yenu!
17 Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Mwenyezi Mungu ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Mwenyezi Mungu mlipoomba mfalme.”
18 Kisha Samweli akamwomba Mwenyezi Mungu, na siku ile ile Mwenyezi Mungu akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Mwenyezi Mungu na Samweli.
19 Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Mwenyezi Mungu, Mungu wako, kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
20 Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Mwenyezi Mungu, bali mtumikieni Mwenyezi Mungu kwa moyo wote.
21 Msigeukie sanamu batili. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
22 Kwa ajili ya jina lake kuu Mwenyezi Mungu hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Mwenyezi Mungu kuwafanya watu wake mwenyewe.
23 Lakini iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Mwenyezi Mungu kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na nyoofu.
24 Lakini hakikisheni mnamcha Mwenyezi Mungu na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
25 Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”
Cross-references
178
- 11Sa 10:24, 1Sa 11:14–15, 1Sa 10:1, 1Sa 8:5–8, 1Sa 8:19–22
- 21Sa 8:5, 1Sa 8:20, 1Sa 8:1, Num 27:17, 1Sa 8:3, 1Sa 3:19–20, 1Sa 3:13, Isa 46:3–4
- 3Act 20:33, Num 16:15, 1Sa 24:6, Deu 16:19, 1Pe 5:2, 1Th 2:10, 1Sa 12:5, Exo 23:8
- 4Dan 6:4, 3Jn 1:12, Psa 37:5–6
- 5Exo 22:4, Act 23:9, Act 24:20, 1Co 4:4, 2Co 1:12, 1Sa 26:9, Psa 17:3, Job 31:35–40
- 6Mic 6:4, Exo 6:26, Psa 99:6, Psa 77:19–20, Psa 105:41, Psa 105:26, Psa 78:12–72, Hos 12:13
- 7Isa 1:18, Ezk 18:25–30, Act 17:3, Mic 6:1–5, Isa 5:3–4, Jdg 5:11
- 8Exo 4:14–16, Exo 2:23–24, Exo 14:30–31, Psa 78:54–55, Exo 3:9–10, Exo 6:26, Exo 12:51, Jos 1:6
- 9Jdg 10:7, Jdg 13:1, Jdg 3:12, Jdg 4:2, Deu 32:18, Psa 106:21, Isa 50:1–2, Isa 63:10
- 10Jdg 2:13, Jdg 10:10, Jdg 3:7, Jdg 3:9, Jdg 10:15–16, Isa 26:16, Luk 1:74–75, Jdg 4:3
- 11Jdg 6:32, Jdg 4:6, Jdg 8:29, Jdg 8:35, Jdg 6:14, 1Sa 7:13, Jdg 11:1–33, Jdg 13:1–16
- 12Jdg 8:23, 1Sa 8:5–7, 1Sa 10:19, 1Sa 11:1–2, Gen 17:7, Jdg 9:18, Jdg 9:56–57, Num 23:21
- 13Hos 13:11, 1Sa 10:24, 1Sa 8:5, 1Sa 11:15, Psa 78:29–31, 1Sa 9:20, Act 13:21
- 14Jos 24:14, Deu 28:1–14, Psa 81:12–15, Isa 3:10, Jos 24:20, Lev 20:1–13, Rom 2:7
- 15Jos 24:20, Isa 1:20, Isa 3:11, Lev 26:14–30, Deu 28:15–68, Rom 2:8–9, 1Sa 12:9, 1Sa 5:9
- 16Exo 14:13, Exo 14:31, 1Sa 12:7, 1Sa 15:16
- 171Sa 8:7, 1Sa 7:9–10, Pro 26:1, Jas 5:16–18, Jos 10:12, Psa 99:6, Jer 15:1
- 18Exo 14:31, Exo 9:23–25, Ezr 10:9, Psa 106:12–13, Rev 11:5–6
- 19Exo 9:28, 1Jn 5:16, 1Sa 12:23, Exo 10:17, Isa 26:16, Jer 15:1, Gen 20:7, Act 8:24
- 20Deu 11:16, Psa 101:3, Jos 23:6, Psa 125:5, Exo 20:19–20, Deu 31:29, 1Pe 3:16, Jer 3:1
- 21Hab 2:18, Jer 10:15, Jer 16:19, Deu 11:16, Jer 14:22, Isa 44:9–10, Jon 2:8, Isa 45:20
- 22Deu 14:2, Psa 106:8, Deu 7:7–8, Php 1:6, 1Ki 6:13, Jer 14:21, Rom 11:29, Jos 7:9
- 23Col 1:9, Rom 1:9, 2Ti 1:3, 1Th 3:10, 1Ki 8:36, Act 12:5, Psa 34:11, Jer 6:16
- 24Deu 10:21, Pro 1:7, Heb 12:29, Psa 126:2–3, Isa 5:12, Psa 111:10, Ecc 12:13, Psa 119:80
- 25Jos 24:20, 1Sa 31:1–5, Hos 10:3, Isa 3:11, Deu 28:36, Deu 32:15–44
Topics in this chapter
32
Aaron, Afflictions and Adversities, Ashtoreth, Bedan, Decision, Fear, God, Hazor, Idolatry, Integrity, Intercession, Israel, Jacob, Meteorology and Celestial Phenomena, Minister, Christian, Miracles, Obedience, Obligation, Prayer, Predestination, Rain, Repentance, Rulers, Samuel, Self-Denial, Sisera, Symbols and Similitudes, Theocracy, Thunder, Truth, Wicked (People), Zeal, Religious