Amosi 5
1 Sikia neno hili, ee nyumba ya Israeli, ombolezo hili ninalifanya kuwahusu ninyi:
2 “Bikira Israeli ameanguka, kamwe hatainuka tena, ameachwa pweke katika nchi yake, hakuna yeyote wa kumwinua.”
3 Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “Mmoja wa miji yako utakapopeleka watu elfu moja vitani kwa ajili ya Israeli, mia moja tu watarudi; wakati mji utakapopeleka mia moja, kumi tu ndio watarudi hai.”
4 Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu kwa nyumba ya Israeli: “Nitafuteni mpate kuishi;
5 msitafute Betheli, msiende Gilgali, msisafiri kwenda Beer-Sheba. Kwa maana kwa hakika Gilgali itaenda uhamishoni, na Betheli itafanywa kuwa ubatili.”
6 Mtafuteni Mwenyezi Mungu mpate kuishi, au atafagia nyumba ya Yusufu kama moto; utawateketeza, nayo Betheli haitakuwa na yeyote wa kuuzima.
7 Ninyi ambao mnageuza haki kuwa uchungu na kuiangusha haki chini
8 (yeye ambaye alifanya Kilimia na Orioni, ambaye hugeuza giza kuwa mapambazuko na mchana kuwa usiku, ambaye huyaita maji ya bahari na kuyamwaga juu ya nchi: Mwenyezi Mungu ndilo jina lake;
9 yeye hufanya maangamizi kwenye ngome na kufanya mji uliozungushiwa ngome kuwa ukiwa),
10 mnamchukia yule akemeaye mahakamani, na kumdharau yule ambaye husema kweli.
11 Mnamgandamiza maskini na kumlazimisha awape nafaka. Kwa hiyo, ingawa mmejenga majumba ya mawe ya fahari, hamtaishi ndani yake; ingawa mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu, hamtakunywa divai yake.
12 Kwa kuwa ninajua hesabu ya makosa yenu na ukubwa wa dhambi zenu. Mmewadhulumu wenye haki na kupokea rushwa na kuzuia haki ya maskini mahakamani.
13 Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza nyakati kama hizo, kwa kuwa nyakati ni mbaya.
14 Tafuteni mema, wala si mabaya, ili mpate kuishi. Ndipo Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni atakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo yupo nanyi.
15 Yachukieni maovu, yapendeni mema; dumisheni haki mahakamani. Yamkini Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, atawahurumia mabaki ya Yusufu.
16 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, yeye Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, asemalo: “Kutakuwa na maombolezo barabarani zote, na vilio vya uchungu katika njia kuu zote. Wakulima wataitwa kuja kulia, na waombolezaji waje kuomboleza.
17 Kutakuwa na kuomboleza katika mashamba yote ya mizabibu, kwa kuwa nitapita kati yenu,” asema Mwenyezi Mungu.
18 Ole wenu ninyi mnaoitamani siku ya Mwenyezi Mungu! Kwa nini mnaitamani siku ya Mwenyezi Mungu? Siku hiyo itakuwa giza, si nuru.
19 Itakuwa kama vile mtu aliyemkimbia simba kumbe akakutana na dubu, kama vile mtu aliyeingia nyumbani mwake na kuupumzisha mkono wake kwenye ukuta, kumbe akaumwa na nyoka.
20 Je, siku ya Mwenyezi Mungu haitakuwa giza, na si nuru: giza nene, bila mwali wowote?
21 “Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini; siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.
22 Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za nafaka, sitazikubali. Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani, sitazitambua.
23 Niondoleeni kelele za nyimbo zenu! Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.
24 Lakini acheni haki itiririke kama mto, na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!
25 “Je, mliniletea dhabihu na sadaka kwa miaka arobaini kule jangwani, ee nyumba ya Israeli?
26 Mmeyainua madhabahu ya Sikuthi mungu wenu mtawala, na Kiuni mungu wenu wa nyota, ambao mliwatengeneza wenyewe.
27 Kwa sababu hiyo nitawapeleka uhamishoni mbali kupita Dameski,” asema Mwenyezi Mungu, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi ya mbinguni.
Cross-references
199
- 1Ezk 19:1, Jer 9:10, Jer 7:29, Jer 9:17, Ezk 28:12, Ezk 26:17, Ezk 32:16, Ezk 27:27–32
- 2Jer 14:17, Hos 14:1, 2Ki 15:29, Jer 51:64, Lam 2:13, Amo 9:11, Lam 1:16–19, Isa 43:17
- 3Rom 9:27, Isa 10:22, Ezk 12:16, Isa 6:13, Deu 28:62, Isa 1:9, Deu 4:27, Amo 6:9
- 4Zep 2:3, 2Ch 15:2, Jer 29:12–13, Psa 14:2, Isa 55:3, Psa 105:3–4, Isa 55:6–7, Mat 7:8
- 5Hos 4:15, Amo 4:4, Amo 8:14, Gen 21:33, 1Co 1:28, 1Co 2:6, Rev 18:17, Amo 7:17
- 6Ezk 20:47–48, Ezk 33:11, Isa 55:6, Mrk 9:43–48, Amo 5:4, Zec 10:6, Amo 5:14, Gen 48:8–20
- 7Amo 6:12, Deu 29:18, Amo 5:11–12, Ezk 3:20, Hos 10:4, Zep 1:6, Isa 10:1, Ezk 33:18
- 8Amo 4:13, Job 9:9, Amo 9:6, Psa 104:20, Amo 8:9, Job 38:31–32, Job 12:22, Job 38:12–13
- 9Jer 37:10, Heb 11:34, 2Ki 13:25, Mic 5:11, 2Ki 13:17
- 10Isa 29:21, 1Ki 22:8, Jhn 8:45–47, Jer 17:16–17, Jhn 7:7, Rev 11:10, 1Ki 18:17, Jhn 15:19
- 11Mic 6:15, Deu 28:30, Zep 1:13, Jas 2:6, Rev 11:8–10, Hag 1:6, Amo 3:15–4:1, Mic 2:2
- 12Amo 2:6–7, Amo 5:10, Isa 1:23, Mal 3:5, Act 7:52, Jas 5:4, 1Sa 8:3, Psa 26:9–10
- 132Ti 3:1, Eph 5:15–16, Mic 2:3, Hos 4:4, Ecc 3:7, Isa 36:21, Mat 27:12–14, Isa 37:3
- 14Jos 1:9, Mat 6:33, Mic 6:8, Php 4:8–9, Mic 3:11, 2Ti 4:22, Psa 34:12–16, 1Ch 28:20
- 15Rom 12:9, 3Jn 1:11, Psa 97:10, Jol 2:14, 1Th 5:21–22, Mic 5:7–8, Rom 8:7, Mic 5:3
- 16Jol 1:11, Jer 9:17–20, Jer 9:10, Rev 18:19, Amo 5:27, Jer 4:31, Isa 15:8, Isa 22:12
- 17Exo 12:12, Jer 48:33, Isa 16:10, Exo 12:23, Isa 32:10–12, Nam 1:15, Nam 1:12, Zec 9:8
- 18Jol 1:15, Jol 2:1–2, Jol 2:31, Jer 30:7, Mal 4:1, Zep 1:14–15, Isa 5:30, Isa 9:19
- 19Isa 24:17–18, Jer 15:2–3, Jer 48:43–44, Act 28:4, Job 20:24–25, 1Ki 20:29–30, Amo 9:1–2
- 20Isa 13:10, Zep 1:15, Ezk 34:12, Job 10:21–22, Rev 16:10, Mat 22:13, Jud 1:13, Job 3:4–6
- 21Isa 1:11–16, Pro 28:9, Lev 26:31, Isa 66:3, Jer 6:20, Pro 15:8, Hos 8:13, Gen 8:21
- 22Mic 6:6–7, Amo 4:4–5, Isa 66:3, Lev 7:12–15, Psa 50:23, Psa 107:21–22, Psa 50:8–14, Psa 116:17
- 23Amo 6:5, Amo 8:10, Amo 8:3
- 24Mic 6:8, Jer 22:3, Pro 21:3, Mrk 12:32–34, Hos 6:6, Amo 5:14–15, Amo 5:7, Job 29:12–17
- 25Act 7:42–43, Neh 9:18, Ezk 20:8, Neh 9:21, Jos 24:14, Lev 17:7, Ezk 20:24, Ezk 20:16
- 262Ki 23:12–13, Lev 20:2–5, 1Ki 11:33, Lev 18:21
- 272Ki 17:6, Act 7:43, Amo 4:13, 2Ki 15:29
Topics in this chapter
49
Astronomy, Beer-Sheba, Beth-El, Bribery, Chiun, Colors, Constellations, Darkness, Day, Evaporation, Famine, Formalism, Gilgal, God, House, Hypocrisy, Idolatry, Infidelity, Injustice, Israel, Prophecies Concerning, Joseph, Judgments, Justice, Minister, Christian, Music, Offerings, Oppression, Orion, Persecution, Pleiades, Poor, Prayer, Prudence, Quotations and Allusions, Repentance, Reproof, Rulers, Salvation, Seekers, Seven, Sin, Speaking, Stars, Stones, Tax, War, Weeping, Wicked (People), Worship