Zekaria 11
1 Fungua milango yako, ee Lebanoni, ili moto uteketeze mierezi yako!
2 Piga yowe, ee msunobari, kwa kuwa mwerezi umeanguka; miti ya fahari imeharibiwa! Piga yowe, enyi mialoni ya Bashani, msitu mnene umefyekwa!
3 Sikiliza yowe la wachungaji; malisho yao manono yameangamizwa! Sikia ngurumo za simba; kichaka kilichostawi sana cha Yordani kimeharibiwa!
4 Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu, Mungu wangu: “Lilishe kundi lililokusudiwa kuchinjwa.
5 Wanunuzi wake huwachinja na kuondoka pasipo kuadhibiwa. Wale wanaowauza husema, ‘Ahimidiwe Mwenyezi Mungu, mimi ni tajiri!’ Wachungaji wao wenyewe hawawahurumii.
6 Kwa kuwa sitawahurumia tena watu wa nchi,” asema Mwenyezi Mungu. “Nitawakabidhi kila mtu mkononi mwa jirani yake na mfalme wake. Wataitenda jeuri nchi, nami sitawaokoa kutoka mikononi mwao.”
7 Kwa hiyo nikalilisha kundi lililotiwa alama kwa kuchinjwa, hasa kundi lililodhulumiwa sana. Kisha nikachukua fimbo mbili, moja nikaiita Fadhili na nyingine Umoja, nami nikalilisha kundi.
8 Katika mwezi mmoja nikawaondoa wachungaji watatu. Kundi la kondoo likanichukia, nami nikachoshwa nao,
9 nikasema, “Sitakuwa mchungaji wenu. Waache wanaokufa wafe na wanaoangamia waangamie. Wale waliobakia kila mmoja na ale nyama ya mwenzake.”
10 Kisha nikachukua fimbo yangu inayoitwa Fadhili nikaivunja, kutangua agano nililofanya na mataifa yote.
11 Likatanguka siku hiyo; kwa hiyo wale waliodhulumiwa katika kundi, waliokuwa wakiniangalia wakajua kuwa hilo lilikuwa neno la Mwenyezi Mungu.
12 Nikawaambia, “Mkiona kuwa ni vyema, nipeni ujira wangu, la sivyo, basi msinipe.” Kwa hiyo wakanilipa vipande thelathini vya fedha.
13 Naye Mwenyezi Mungu akaniambia, “Mtupie mfinyanzi,” hiyo bei nzuri waliyonithaminia! Kwa hiyo nikachukua hivyo vipande thelathini vya fedha na kumtupia huyo mfinyanzi katika nyumba ya Mwenyezi Mungu.
14 Kisha nikaivunja fimbo yangu ya pili iitwayo Umoja, kuvunja undugu kati ya Yuda na Israeli!
15 Kisha Mwenyezi Mungu akaniambia, “Vitwae tena vifaa vya mchungaji mpumbavu.
16 Kwa maana ninaenda kumwinua mchungaji juu ya nchi ambaye hatamjali aliyepotea, wala kuwatafuta wale wachanga au kuwaponya waliojeruhiwa, wala kuwalisha wenye afya, lakini atakula nyama ya kondoo wanono na kuzirarua kwato zao.
17 “Ole wa mchungaji asiyefaa, anayeliacha kundi! Upanga na uupige mkono wake na jicho lake la kuume! Mkono wake na unyauke kabisa, jicho lake la kuume lipofuke kabisa!”
Cross-references
133
- 1Jer 22:23, Jer 22:6–7, Luk 21:23–24, Hab 2:8, Deu 32:22, Zec 10:10, Mat 24:1–2, Luk 19:41–44
- 2Luk 23:31, Ezk 31:17, Amo 6:1, Ezk 20:46, Isa 10:33–34, Nam 3:8–19, Ezk 31:2–3, Isa 32:15–19
- 3Jer 50:44, Jer 25:34–36, Jer 7:4, Hos 1:9–10, Jer 26:6, Psa 22:21, Zec 11:15–17, Jer 2:30
- 4Zec 11:7, Mat 23:37, Rom 15:8, Isa 49:4–5, Ezk 34:23–24, Eph 1:3, Mat 15:24, Mic 5:4
- 5Jer 50:7, 1Ti 6:5–10, Hos 12:8, 2Ki 4:1, Mat 23:13, Gen 37:26–28, Deu 29:19–21, 2Pe 2:3
- 6Jer 13:14, Heb 10:26–31, Isa 9:19–21, Mic 5:8, Mat 22:7, Psa 50:22, Mat 18:33–35, Zec 8:10
- 7Zec 11:4, Zec 11:14, Isa 11:4, Ezk 37:16–23, Eph 2:13–16, Psa 23:4, Zec 11:10–11, Zep 3:12
- 8Jhn 7:7, Jhn 15:18, Isa 49:7, Mat 23:34–36, Jhn 15:23–25, Hos 5:7, Luk 19:14, Psa 106:40
- 9Jer 43:11, Mat 13:10–11, Rev 22:11, Mat 15:14, Jhn 12:35, Jhn 8:24, Mat 21:43, Jer 23:33
- 10Zec 11:7, Psa 89:39, Heb 8:8–13, Jer 14:21, Jer 31:31–32, 1Sa 2:30, Luk 21:5–6, Heb 7:17–22
- 11Zep 3:12, Jas 2:5–6, Lam 3:25–26, Isa 40:31, Zec 11:6–7, Mic 7:7, Luk 7:22, Isa 26:8–9
- 12Mat 26:15, Exo 21:32, Luk 22:3–6, Mrk 14:10–11, Jhn 13:27–30, Gen 37:28, 1Ki 21:2, Jhn 13:2
- 13Mat 27:3–10, Act 1:18–19, Isa 53:2–3, Isa 54:7–10, Act 4:11, Mat 27:12
- 14Isa 9:21, Jas 3:16, Zec 11:9, Ezk 37:16–20, Gal 5:15, Isa 11:13, Act 23:7–10, Jas 4:1–3
- 15Jer 2:26–27, Lam 2:14, Isa 6:10–12, Ezk 13:3, Luk 11:40, Mat 15:14, Mat 23:17
- 16Jhn 10:12–13, Jer 23:2, Ezk 34:2–6, Jhn 10:1, Luk 12:45–46, Ezk 34:21, Ezk 34:10, Mat 23:2–4
- 17Jer 23:1, Ezk 13:3, 1Co 8:4, Ezk 34:2, Mat 23:16, Isa 42:19–20, 1Co 10:19–20, Amo 8:9–10